Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

7

1Vyriausiasis kunigas paklausė: “Ar tikrai taip yra?”
1Basi, Kuhani Mkuu akamwuliza, "Je, mambo haya ni kweli?"
2O Steponas prabilo: “Vyrai broliai ir tėvai, paklausykite! Šlovės Dievas apsireiškė mūsų tėvui Abraomui Mesopotamijoje, kai jis dar nebuvo persikėlęs į Charaną,
2Naye Stefano akasema, "Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
3ir pasakė jam: ‘Išeik iš savo krašto, nuo savo giminių, ir keliauk į šalį, kurią tau parodysiu’.
3Mungu alimwambia: Ondoka katika nchi yako; waache watu wa ukoo wako; nenda katika nchi nitakayokuonyesha!
4Tada jis paliko chaldėjų kraštą ir apsigyveno Charane. Iš ten, jo tėvui mirus, Dievas atvedė jį į šitą šalį, kurioje jūs dabar gyvenate.
4Kwa hivyo, Abrahamu alihama nchi ya Kaldayo, akaenda kukaa Harani. Baada ya kifo cha baba yake, Mungu alimtoa tena Harani akaja kukaa katika nchi hii mnayokaa sasa.
5Bet čia jam nedavė paveldėti nė pėdos žemės, tik pažadėjo ją atiduoti jo ir jo palikuonių nuosavybėn, nors jis dar buvo bevaikis.
5Mungu hakumpa hata sehemu moja ya nchi hii iwe mali yake; hata hivyo, alimwahidia kumpa nchi hii iwe yake na ya wazawa wake, ingawaje wakati huu hakuwa na mtoto.
6Dievas pasakė, kad jo palikuonys gyvens kaip ateiviai svetimoje žemėje ir keturis šimtus metų bus pavergti ir skriaudžiami.
6Mungu alimwambia hivi: Wazao wako watapelekwa katika nchi inayotawaliwa na watu wengine, na huko watafanywa watumwa na kutendewa vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
7‘Tačiau,­tarė Dievas,­Aš nuteisiu tautą, kuriai jie vergaus; tada jie išeis ir tarnaus man šitoje vietoje’.
7Lakini mimi nitalihukumu taifa hilo litakalowafanya watumwa. Kisha nitawatoa katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.
8Ir tuomet Jis davė jam apipjaustymo sandorą. Tada Abraomui gimė Izaokas, kurį jis apipjaustė aštuntąją dieną. Izaokui gimė Jokūbas, o Jokūbui gimė dvylika patriarchų.
8Halafu Mungu aliifanya tohara iwe ishara ya agano. Hivyo, Abrahamu alimtahiri mtoto wake Isaka, siku ya nane baada ya kuzaliwa. Na Isaka, vivyo hivyo, alimtahiri Yakobo. Naye Yakobo aliwatendea wale mababu kumi na wawili vivyo hivyo.
9Šie patriarchai iš pavydo pardavė Juozapą į Egiptą. Bet Dievas buvo su juo,
9"Wale mababu walimwonea wivu Yosefu, wakamuuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,
10išgelbėjo Juozapą iš visų jo vargų ir suteikė jam malonės bei išminties Egipto karaliaus­faraono akivaizdoje. Tas jį paskyrė Egipto ir visų savo namų valdytoju.
10akamwokoa katika taabu zake zote. Mungu alimjalia fadhili na hekima mbele ya Farao, mfalme wa Misri, hata Farao akamweka awe mkuu wa ile nchi na nyumba ya kifalme.
11Tuomet visą Egipto žemę ir Kanaaną ištiko badas bei didis vargas, ir mūsų tėvai negalėjo rasti sau maisto.
11Kisha, kulizuka njaa kubwa katika nchi yote ya Misri na Kanaani, ikasababisha dhiki kubwa. Babu zetu hawakuweza kupata chakula chochote.
12Išgirdęs, kad Egipte yra javų, Jokūbas išsiuntė ten mūsų tėvus pirmą kartą,
12Basi, Yakobo alipopata habari kwamba huko Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma watoto wake, yaani babu zetu, waende huko Misri mara ya kwanza.
13o antrą kartą Juozapas leidosi savo brolių atpažįstamas, ir faraonas sužinojo apie Juozapo giminę.
13Katika safari yao ya pili, Yosefu alijitambulisha kwa ndugu zake, na Farao akaifahamu jamaa ya Yosefu.
14Tada Juozapas pasiuntė pakviesti savo tėvo Jokūbo ir visų giminaičių­septyniasdešimt penkių sielų.
14Yosefu alituma ujumbe kwa baba yake na jamaa yote, jumla watu sabini na tano, waje Misri.
15Šitaip Jokūbas iškeliavo į Egiptą. Ten mirė jis ir mūsų tėvai.
15Hivyo, Yakobo alikwenda Misri ambako yeye na babu zetu wengine walikufa.
16Juos pargabeno į Sichemą ir palaidojo kape, kurį Abraomas už pinigus buvo nupirkęs iš sichemiečio Emoro sūnų.
16Miili yao ililetwa mpaka Shekemu, ikazikwa katika kaburi Abrahamu alilonunua kutoka kwa kabila la Hamori kwa kiasi fulani cha fedha.
17Artėjant metui pažado, dėl kurio Dievas buvo prisiekęs Abraomui, tauta išaugo ir išsiplėtė Egipte,
17"Wakati ulipotimia Mungu aitimize ahadi aliyompa Abrahamu, idadi ya wale watu kule Misri ilikwisha ongezeka na kuwa kubwa zaidi.
18kol pakilo kitas karalius, kuris nieko nežinojo apie Juozapą.
18Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.
19Jis klastingai elgėsi su mūsų gimine, versdamas mūsų tėvus išmesti savo kūdikius, kad jie neliktų gyvi.
19Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.
20Tuo metu gimė Mozė, kuris buvo mielas Dievui. Tris mėnesius jis buvo maitinamas savo tėvo namuose,
20Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,
21o kai buvo išmestas, jį pasiėmė faraono duktė ir augino kaip savo pačios sūnų.
21na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.
22Mozė buvo išmokytas visos Egipto išminties ir tapo galingas žodžiais ir darbais.
22Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.
23Kai jam sukako keturiasdešimt metų, jo širdyje kilo troškimas aplankyti savo brolius, Izraelio vaikus.
23"Alipokuwa na umri wa miaka arobaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.
24Pamatęs vieną iš jų skriaudžiamą, stojo ginti jo ir keršydamas užmušė egiptietį.
24Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri.
25Mozė tikėjosi, kad jo broliai suprasią, jog Dievas jo ranka suteiks jiems išgelbėjimą, bet jie šito nesuprato.
25(Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo.)
26Kitą dieną jis priėjo prie besimušančių tautiečių ir mėgino juos sutaikinti, sakydamas: ‘Vyrai, jūs esate broliai! Kodėl skriaudžiate vienas kitą?’
26Kesho yake, aliwaona Waisraeli wawili wakipigana, akajaribu kuwapatanisha, akisema: Ninyi ni ndugu; kwa nini basi, kutendeana vibaya ninyi kwa ninyi?
27Bet tasai, kuris skriaudė artimą, atstūmė jį, sakydamas: ‘Kas tave paskyrė mūsų valdovu ir teisėju?
27Yule aliyekuwa anampiga mwenzake alimsukuma Mose kando akisema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wa watu?
28Gal nori ir mane nužudyti, kaip vakar nužudei egiptietį?’
28Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri jana?
29Tai išgirdęs, Mozė pabėgo ir buvo ateivis Madiano krašte, kur jam gimė du sūnūs.
29Baada ya kusikia hayo Mose alikimbia, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani na huko akapata watoto wawili.
30Po keturiasdešimties metų Sinajaus kalno dykumoje jam pasirodė angelas degančio erškėčių krūmo liepsnose.
30"Miaka arobaini ilipotimia, malaika wa Bwana alimtokea Mose katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto kule jangwani karibu na mlima Sinai.
31Tai pamatęs, Mozė labai nusistebėjo reginiu. Kai jis artinosi, norėdamas geriau įsižiūrėti, jam pasigirdo Viešpaties balsas:
31Mose alistaajabu sana kuona jambo hilo hata akasogea karibu ili achungulie; lakini alisikia sauti ya Bwana:
32‘Aš esu tavo tėvų Dievas, Abraomo, Izaoko ir Jokūbo Dievas’. Tada Mozė ėmė drebėti ir nebedrįso toliau žiūrėti.
32Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo! Mose akatetemeka kwa hofu na wala hakuthubutu kutazama zaidi.
33O Viešpats jam tarė: ‘Nusiauk apavą nuo kojų, nes ta vieta, kur tu stovi, yra šventa žemė.
33Bwana akamwambia: Vua viatu vyako maana hapa unaposimama ni mahali patakatifu.
34Aš regėte regėjau savo tautos priespaudą Egipte, išgirdau jos dejones ir nužengiau jos išvaduoti. Tad ateik čia, Aš pasiųsiu tave į Egiptą’.
34Nimeyaona mabaya wanayotendewa watu wangu kule Misri. Nimesikia kilio chao, nami nimekuja kuwaokoa. Basi sasa, nitakutuma Misri.
35Tą Mozę, kurio jie atsižadėjo, sakydami: ‘Kas tave paskyrė valdovu ir teisėju?’, Dievas pasiuntė kaip vadovą ir gelbėtoją ranka angelo, kuris pasirodė jam erškėčių krūme.
35"Huyu Mose ndiye yule watu wa Israeli waliyemkataa waliposema: Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi wetu? Kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kichaka kilichokuwa kinawaka moto, Mungu alimtuma Mose huyo awe kiongozi na mkombozi.
36Jis išvedė juos, darydamas stebuklus ir ženklus Egipto žemėje, prie Raudonosios jūros ir per keturiasdešimt metų dykumoje.
36Ndiye aliyewaongoza wale watu watoke Misri kwa kufanya miujiza na maajabu katika nchi ya Misri, katika bahari ya Shamu na jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
37Tai šis Mozė pasakė Izraelio vaikams: ‘Dievas pažadins jums iš jūsų brolių Pranašą, panašiai kaip mane’.
37Mose ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: Mungu atawateulieni nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu ninyi wenyewe.
38Tai jis susirinkimo dieną dykumoje tarpininkavo tarp angelo, kalbėjusio jam Sinajaus kalne, ir mūsų tėvų. Ten jis gavo mums skirtuosius gyvenimo žodžius.
38Wakati watu wa Israeli walipokutana pamoja kule jangwani, Mose ndiye aliyekuwako huko pamoja nao. Alikuwa huko pamoja na babu zetu na yule malaika aliyeongea naye mlimani Sinai; ndiye aliyekabidhiwa yale maneno yaletayo uzima atupe sisi.
39Jam mūsų tėvai nenorėjo paklusti, atstūmė jį ir savo širdis nukreipė į Egiptą.
39"Lakini yeye ndiye babu zetu waliyemkataa kumsikiliza; walimsukuma kando, wakatamani kurudi Misri.
40Jie tarė Aaronui: ‘Padaryk mums dievų, kurie žygiuotų mūsų priekyje, nes mes nežinome, kas nutiko tam Mozei, kuris išvedė mus iš Egipto žemės’.
40Walimwambia Aroni: Tutengenezee miungu itakayotuongoza njiani, maana hatujui yaliyompata Mose huyu aliyetuongoza kutoka Misri!
41Taip anomis dienomis jie pasidirbo veršį, atnašavo stabui auką ir džiaugėsi savo rankų darbu.
41Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.
42Tada Dievas nusigręžė nuo jų ir paliko juos garbinti dangaus kariauną, kaip parašyta pranašų knygoje: ‘Ar jūs, Izraelio namai, man atnešėte aukų bei atnašų, keturiasdešimt metų būdami dykumoje?
42Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii: Enyi watu wa Israeli! Si mimi mliyenitolea dhabihu na sadaka kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani!
43Jūs pasiėmėte Molocho palapinę ir dievo Refano žvaigždę­stabus, kuriuos pasidirbote garbinti. Todėl ištremsiu jus anapus Babilono’.
43Ninyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki, na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani. Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu. Kwa sababu hiyo nitakupeleka mateka mbali kupita Babuloni!
44Mūsų tėvai dykumoje turėjo Liudijimo palapinę, kaip įsakė Tas, kuris kalbėjo Mozei, kad padarytų ją pagal regėtą jos vaizdą.
44Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema lililoshuhudia kuweko kwa Mungu. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichoonyeshwa.
45Mūsų tėvai su Jozue pasiėmė ją ir atsigabeno į žemes pagonių, kuriuos Dievas išvijo nuo mūsų tėvų akių. Taip pasiliko iki Dovydo dienų.
45Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.
46Šis susilaukė Dievo akyse malonės ir meldė, kad rastų buveinę Jokūbo Dievui.
46Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.
47Ir Saliamonas pastatė Jam namus.
47Lakini Solomoni ndiye aliyemjengea Mungu nyumba.
48Bet Aukščiausiasis negyvena rankų darbo šventyklose, kaip sako ir pranašas:
48"Hata hivyo, Mungu Mkuu haishi katika nyumba zilizojengwa na binadamu; kama nabii asemavyo:
49‘Dangus­mano sostas, o žemė­pakojis po mano kojomis. Kokius gi namus man statysite?­ klausia Viešpats,­ar kokia mano poilsio vieta?
49Bwana asema: Mbingu ni kiti changu cha enzi na dunia ni kiti changu cha kuwekea miguu.
50Argi ne mano ranka visa tai padarė?’
50Ni nyumba ya namna gani basi mnayoweza kunijengea, na ni mahali gani nitakapopumzika? Vitu hivi vyote ni mimi nimevifanya, au sivyo?
51Jūs, kietasprandžiai, neapipjaustytomis širdimis ir ausimis! Jūs, kaip ir jūsų tėvai, visuomet priešinatės Šventajai Dvasiai.
51"Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa. Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
52Kurio iš pranašų nepersekiojo jūsų tėvai? Jie užmušė iš anksto skelbusius Teisiojo atėjimą. Jo išdavėjais ir žudikais dabar esate jūs.
52Je, yuko nabii yeyote ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua hao Mungu aliowatuma watangaze kuja kwake yule Mwenye Haki. Na sasa, ninyi mmemsaliti, mkamuua.
53Jūs, kurie gavote Įstatymą, paskelbtą per angelus, bet jo nesilaikėte”.
53Ninyi mliipokea ile Sheria iliyoletwa kwenu na Malaika, lakini hamkuitii."
54Tie žodžiai jiems draskė širdį, ir jie griežė ant jo dantimis.
54Wale wazee wa Baraza waliposikia hayo, walighadhibika sana, wakamsagia meno kwa hasira.
55O Steponas, kupinas Šventosios Dvasios, žvelgė į dangų ir išvydo Dievo šlovę ir Jėzų, stovintį Dievo dešinėje.
55Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
56Jis tarė: “Štai regiu atsivėrusį dangų ir Žmogaus Sūnų, stovintį Dievo dešinėje”.
56Akasema, "Tazameni! Ninaona mbingu zimefunuliwa na Mwana wa Mtu amesimama upande wa kulia wa Mungu."
57Tada, baisiai rėkdami, jie užsikimšo ausis ir visi kaip vienas puolė jį,
57Hapo, watu wote katika kile kikao cha Baraza, wakapiga kelele na kuziba masikio yao kwa mikono yao. Kisha wakamrukia wote kwa pamoja,
58išsitempė už miesto ir užmėtė akmenimis. Liudytojai padėjo savo drabužius prie kojų vieno jauno vyro, vardu Sauliaus.
58wakamtoa nje ya mji, wakampiga mawe. Wale mashahidi wakayaweka makoti yao chini ya ulinzi wa kijana mmoja jina lake Saulo.
59Taip jie mušė akmenimis Steponą, o jis šaukė: “Viešpatie Jėzau, priimk mano dvasią!”
59Waliendelea kumpiga mawe Stefano, huku akiwa anasali: "Bwana Yesu, ipokee roho yangu!"
60Pagaliau suklupęs jis galingu balsu sušuko: “Viešpatie, neįskaityk jiems šios nuodėmės!” Ir, tai ištaręs, užmigo.
60Akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa: "Bwana, usiwalaumu kwa sababu ya dhambi hii." Baada ya kusema hivyo, akafa.