Lithuanian

Swahili: New Testament

Acts

6

1Tomis dienomis, mokinių skaičiui augant, tarp graikiškai kalbančiųjų kilo nepasitenkinimas vietiniais žydais, nes kasdieniniame aprūpinime būdavo aplenkiamos jų našlės.
1Baadaye, idadi ya wanafunzi ilipokuwa inazidi kuongezeka, kulitokea manung'uniko kati ya wanafunzi waliosema Kigiriki na wale waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigiriki walinung'unika kwamba wajane wao walikuwa wanasahauliwa katika ugawaji wa mahitaji ya kila siku.
2Tuomet dvylika sušaukė mokinių susirinkimą ir tarė: “Nedera mums palikus Dievo žodį tarnauti prie stalų.
2Kwa hiyo, mitume kumi na wawili waliita jumuiya yote ya wanafunzi, wakasema, "Si vizuri sisi tuache kulihubiri neno la Mungu ili tushughulikie ugawaji wa mahitaji.
3Todėl, broliai, išsirinkite iš savųjų septynis vyrus, turinčius gerą vardą, kupinus Šventosios Dvasios ir išminties. Mes juos paskirsime tam darbui,
3Hivyo, ndugu zetu, chagueni miongoni mwenu watu saba wenye sifa njema, waliojawa na Roho na wenye hekima; nasi tutawakabidhi jukumu hilo.
4o patys toliau atsidėsime maldai ir žodžio tarnavimui”.
4Sisi, lakini, tutashughulika na sala na kazi ya kuhubiri neno la Mungu."
5Šis pasiūlymas patiko visam susirinkimui, ir jie išsirinko Steponą, vyrą pilną tikėjimo ir Šventosios Dvasios, Pilypą, Prochorą, Nikanorą, Timoną, Parmeną ir Mikalojų, prozelitą iš Antiochijos.
5Jambo hilo likaipendeza jumuiya yote ya waumini. Wakawachagua Stefano, mtu mwenye imani kubwa na mwenye kujawa na Roho Mtakatifu, Filipo, Prokoro, Nikanora, Timona, Parmena na Nikolao wa Antiokia ambaye hapo awali alikuwa ameongokea dini ya Kiyahudi.
6Juos pastatė prieš apaštalus, o šie melsdamiesi uždėjo ant jų rankas.
6Wakawaweka mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono.
7Dievo žodis klestėjo, ir mokinių skaičius Jeruzalėje smarkiai augo. Ir didelis kunigų būrys pakluso tikėjimui.
7Neno la Mungu likazidi kuenea na idadi ya waumini huko Yerusalemu ikaongezeka zaidi, na kundi kubwa la makuhani wakaipokea imani.
8Steponas, pilnas tikėjimo ir jėgos, darė žmonėse didžių stebuklų ir ženklų.
8Mungu alimjalia Stefano neema tele, akampa nguvu nyingi hata akawa anatenda miujiza na maajabu kati ya watu.
9Tuomet pakilo kai kurie iš vadinamosios libertinų sinagogos, iš kirėniečių, aleksandriečių ir iš Kilikijos bei Azijos ir ėmė ginčytis su Steponu.
9Lakini watu fulani wakatokea ili wabishane na Stefano. Baadhi ya watu hao walikuwa wa sunagogi moja lililoitwa "Sunagogi la Watu Huru", nao walitoka Kurene na Aleksandria; wengine walitoka Kilikia na Asia.
10Tačiau jie negalėjo atsispirti išminčiai ir Dvasiai, kurios įkvėptas jis kalbėjo.
10Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya yule Roho aliyeongoza maneno yake.
11Tada jie papirko keletą vyrų, kad tie sakytų: “Mes girdėjome jį piktžodžiaujant Mozei ir Dievui”.
11Kwa hiyo waliwahonga watu kadhaa waseme: "Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kumkashifu Mose na kumkashifu Mungu."
12Taip jie sukurstė minią, vyresniuosius bei Rašto žinovus, užpuolę sučiupo jį ir nusivedė į sinedrioną.
12Kwa namna hiyo, waliwachochea watu, wazee na walimu wa Sheria. Basi, wakamjia Stefano, wakamkamata na kumleta mbele ya Baraza kuu.
13Ten pastatė melagingus liudytojus, kurie tvirtino: “Šitas žmogus nesiliauja kalbėjęs prieš šventąją vietą ir Įstatymą.
13Walileta Barazani mashahidi wa uongo ambao walisema, "Mtu huyu haachi kamwe kusema maneno ya kupakashifu mahali hapa patakatifu na Sheria ya Mose.
14Mes girdėjome jį sakant, kad Jėzus iš Nazareto išgriaus šią vietą ir pakeis Mozės perduotus mums papročius”.
14Kwa maana tulikwisha msikia akisema eti huyo Yesu wa Nazareti atapaharibu kabisa mahali hapa na kufutilia mbali desturi zile tulizopokea kutoka kwa Mose."
15Visi sėdintys sinedrione įsmeigė į jį akis ir matė jo veidą tarytum angelo veidą.
15Wote waliokuwa katika kile kikao cha Baraza walimkodolea macho Stefano, wakauona uso wake umekuwa kama wa malaika.