1O vienas vyras, vardu Ananijas, su savo žmona Sapfyra pardavė nuosavybę
1Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
2ir, žmonai pritariant, pasiliko dalį gautų pinigų, o kitą dalį atnešė ir padėjo prie apaštalų kojų.
2Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
3Petras paklausė: “Ananijau, kodėl šėtonas užvaldė tavo širdį, kad tu pamelavai Šventajai Dvasiai, pasilikdamas dalį už žemę gautų pinigų?
3Basi, Petro akamwuliza, "Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
4Argi nebuvo tavo tai, ką turėjai, ir ką gavai pardavęs, argi nebuvo tavo žinioje? Tai kodėl gi taip sumanei savo širdyje? Tu pamelavai ne žmonėms, bet Dievui!”
4Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!"
5Išgirdęs tuos žodžius, Ananijas krito ant žemės ir mirė. Didelė baimė apėmė visus tai girdėjusius.
5Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
6Keli jaunuoliai pakilo, suvyniojo jį marškomis, išnešė ir palaidojo.
6Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
7Po kokių trijų valandų atėjo jo žmona, kuri nežinojo, kas buvo atsitikę.
7Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
8Petras ją paklausė: “Pasakyk man, ar už tiek pardavėte sklypą?” “Taip, už tiek”,atsakė ji.
8Petro akamwambia, "Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?" Yeye akamjibu, "Naam, ni kiasi hicho."
9Tada Petras jai tarė: “Kodėl susitarėte mėginti Viešpaties Dvasią? Štai ties durimis skamba žingsniai tų, kurie palaidojo tavo vyrą. Jie ir tave išneš”.
9Naye Petro akamwambia, "Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia."
10Bematant ji susmuko jam po kojų ir mirė. Atėję jaunuoliai rado ją negyvą, nunešė ir palaidojo šalia vyro.
10Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
11Didelė baimė apėmė visą bažnyčią ir visus, kurie apie tai išgirdo.
11Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
12Per apaštalų rankas žmonėse vyko daug ženklų ir stebuklų. Visi jie vieningai rinkdavosi Saliamono stoginėje.
12Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
13Iš kitų nė vienas neišdrįsdavo prie jų prisidėti. Žmonės juos labai gerbė.
13Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
14Ir vis labiau augo būrys vyrų ir moterų, įtikėjusių Viešpatį.
14Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
15Net į gatves nešdavo ligonius ir guldydavo ant neštuvų bei lovų, kad, Petrui praeinant pro šalį, bent jo šešėlis kristų ant gulinčiųjų.
15Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16Taip pat ir iš aplinkinių miestų daugybė žmonių keliaudavo į Jeruzalę, gabendami sergančius ir netyrųjų dvasių kankinamus, ir visi jie būdavo pagydomi.
16Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
17Tuomet sujudo vyriausiasis kunigas ir visi jo šalininkai iš sadukiejų partijos. Degdami pavydu,
17Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
18jie suėmė apaštalus ir įmetė juos į viešą kalėjimą.
18Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
19Bet Viešpaties angelas naktį atidarė kalėjimo vartus, išvedė juos ir tarė:
19Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
20“Eikite ir, atsistoję šventykloje, skelbkite žmonėms visus šio Gyvenimo žodžius”.
20"Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya."
21Tai išgirdę, jie auštant nuėjo į šventyklą ir ėmė mokyti. Tuo metu vyriausiasis kunigas ir jo šalininkai sukvietė sinedrioną bei visą Izraelio tautos vyresniųjų tarybą ir nusiuntė į kalėjimą tarnus atvesti apaštalų.
21Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
22Bet tarnai nuėję nerado jų kalėjime ir sugrįžę pranešė:
22Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
23“Kalėjimą radome saugiai užrakintą ir sargybinius stovinčius prie vartų. Bet atidarę nieko viduje neradome!”
23wakisema, "Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani."
24Išgirdę tokį pranešimą, vyriausiasis kunigas, šventyklos apsaugos viršininkas ir aukštieji kunigai suglumo, nesuprasdami, ką tai galėtų reikšti.
24Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
25Tuomet kažkas atėjęs pranešė: “Tie vyrai, kuriuos buvote uždarę kalėjime, stovi šventykloje ir moko žmones”.
25Akafika mtu mmoja, akawaambia, "Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu."
26Tada viršininkas su tarnais nuėjo ir atsivedė juos be prievartos, nes bijojo žmonių, kad neužmėtytų akmenimis.
26Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
27Taigi atsivedę apaštalus, pastatė juos sinedrione. Vyriausiasis kunigas jiems tarė:
27Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
28“Argi mes jums drauste neuždraudėme mokyti tuo vardu, o štai jūs užtvindėte Jeruzalę savo mokymu ir dar norite ant mūsų užtraukti to žmogaus kraują”.
28"Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo."
29Petras ir apaštalai atsakė: “Dievo reikia klausyti labiau negu žmonių.
29Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, "Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
30Mūsų tėvų Dievas prikėlė Jėzų, kurį jūs nužudėte, pakabindami ant medžio.
30Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
31Dievas išaukštino Jį savo dešine kaip Karalių ir Išgelbėtoją, kad suteiktų Izraeliui atgailą ir nuodėmių atleidimą.
31Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
32Mes esame Jo ir tų įvykių liudytojai, taip pat ir Šventoji Dvasia, kurią Dievas suteikė tiems, kurie Jam paklūsta”.
32Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo."
33Girdėdami šituos žodžius, jie baisiai įtūžo ir ketino juos užmušti.
33Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
34Tuomet sinedrione pakilo vienas fariziejus, vardu Gamalielis, visos tautos gerbiamas Įstatymo mokytojas. Jis įsakė trumpam išvesti apaštalus
34Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
35ir tarė susirinkusiems: “Vyrai izraelitai! Gerai pagalvokite, kaip pasielgti su šitais žmonėmis.
35Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, "Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
36Juk prieš kiek laiko buvo iškilęs Teudas, kuris laikė save kažkuo nepaprastu. Prie jo prisidėjo apie keturis šimtus vyrų, bet jis buvo užmuštas, visi šalininkai išsisklaidė ir nuėjo niekais.
36Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
37Po jo, gyventojų surašymo dienomis, atsirado Judas Galilėjietis ir patraukė nemažai žmonių paskui save. Jis taip pat žuvo, o visi jo sekėjai buvo išblaškyti.
37Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
38Todėl dabar jums sakau: palikite šituos žmones ramybėje ir paleiskite juos. Jei šis sumanymas ir ši veikla iš žmonių,jie žlugs savaime,
38Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
39o jeigu tai iš Dievo, tai jūs nepajėgsite jų sunaikinti. Žiūrėkite, kad nepasirodytumėte kovojantys prieš Dievą!” Jie paklausė jo patarimo.
39Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu." Basi, wakakubaliana naye.
40Pasišaukę apaštalus, nuplakdino juos, uždraudė kalbėti Jėzaus vardu ir paleido.
40Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
41O tie ėjo iš sinedriono džiaugdamiesi, kad buvo palaikyti vertais dėl Jėzaus vardo iškęsti paniekinimą.
41Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
42Kiekvieną dieną šventykloje ir po namus jie nesiliovė mokyti bei skelbti Jėzų Kristumi.
42Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.