Lithuanian

Swahili: New Testament

Colossians

1

1Paulius, Dievo valia Kristaus Jėzaus apaštalas, ir brolis Timotiejus,­
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2šventiesiems ir ištikimiesiems broliams Kristuje, gyvenantiems Kolosuose: malonė ir ramybė jums nuo Dievo, mūsų Tėvo, ir mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus!
2tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3Nuolat melsdamiesi už jus, dėkojame Dievui, mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Tėvui,
3Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4nes girdime apie jūsų tikėjimą Kristumi Jėzumi ir jūsų meilę visiems šventiesiems
4Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5dėl vilties, kuri jums paruošta danguje. Apie ją jūs esate girdėję Evangelijos tiesos žodyje,
5Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6kuris pasiekė jus ir panašiai kaip visame pasaulyje, taip ir pas jus neša vaisių ir auga nuo tos dienos, kada išgirdote ir pažinote Dievo malonę tiesoje.
6Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7To jūs išmokote iš mūsų mylimojo bendradarbio Epafro, kuris jums yra ištikimas Kristaus tarnas.
7Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8Jis ir davė žinią mums apie jūsų meilę Dvasioje.
8Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9Todėl ir mes nuo tos dienos, kada tai išgirdome, nesiliaujame už jus meldę ir prašę, kad jūs būtumėte pilni Dievo valios pažinimo su visa išmintimi ir dvasiniu supratimu,
9Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10kad elgtumėtės, kaip verta Viešpaties, ir Jam tobulai patiktumėte, nešdami vaisių gerais darbais ir augdami Dievo pažinimu;
10Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11kad, sustiprinti visokeriopa jėga iš Jo šlovės galios didžiai kantrybei ir ištvermei, su džiaugsmu
11Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12dėkotumėte Tėvui, kuris padarė mus tinkamus paveldėti šventųjų dalį šviesoje,
12Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13kuris išlaisvino mus iš tamsybių valdžios ir perkėlė į savo mylimojo Sūnaus karalystę.
13Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14Jame mes turime atpirkimą Jo krauju ir nuodėmių atleidimą.
14ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15Jis yra neregimojo Dievo atvaizdas, visos kūrinijos pirmagimis,
15Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16nes Juo sutverta visa, kas yra danguje ir žemėje, kas regima ir neregima; ar sostai, ar viešpatystės, ar kunigaikštystės, ar valdžios,­visa sutverta per Jį ir Jam.
16Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17Jis yra pirma visų daiktų, ir visa Juo laikosi.
17Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18Ir Jis yra kūno­bažnyčios galva. Jis­pradžia, pirmagimis iš mirusiųjų, kad visame kame turėtų pirmenybę.
18Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19Nes Tėvui patiko Jame apgyvendinti visą pilnatvę
19Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20ir per Jį visa sutaikinti su savimi, darant Jo kryžiaus krauju taiką,­per Jį sutaikinti visa, kas yra žemėje ir danguje.
20Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21Taip pat ir jus, kurie kadaise buvote svetimi ir priešiški savo protuose piktais darbais, Dievas dabar sutaikino
21Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22mirtimi Jo žemiškajame kūne, kad pasirodytumėte Jo akyse šventi, tyri ir nekalti,
22Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23jei tik pasiliekate tikėjime įsitvirtinę bei nepajudinami ir neatsitraukiate nuo Evangelijos vilties, kurią išgirdote, kuri paskelbta visai kūrinijai po dangumi ir kurios tarnu aš, Paulius, tapau.
23Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24Dabar aš džiaugiuosi savo kentėjimais už jus ir savo kūne papildau, ko dar trūksta Kristaus vargams dėl Jo kūno­bažnyčios.
24Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25Jos tarnu aš tapau Dievo patvarkymu, kuris duotas man dėl jūsų, kad išpildyčiau Dievo žodį,
25Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26tą paslaptį, kuri buvo paslėpta amžiams ir kartoms, o dabar apreikšta Jo šventiesiems.
26ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake.
27Jiems Dievas panorėjo atskleisti, kokie šios paslapties šlovės turtai skirti pagonims, būtent Kristus jumyse­šlovės viltis.
27Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28Mes Jį skelbiame, įspėdami kiekvieną žmogų ir mokydami kiekvieną žmogų su visokeriopa išmintimi, kad kiekvieną žmogų padarytume tobulą Kristuje.
28Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29Dėl to aš ir darbuojuos, grumdamasis Jo suteikta jėga, kuri galingai veikia manyje.
29Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.