1Tad noriu, kad jūs žinotumėte, kaip įnirtingai kovoju už jus, už laodikiečius ir visus, kurie nėra matę mano kūno veido,
1Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
2kad būtų paguostos visų širdys, kad, meile suvienyti, visi pasiektų pažinimo pilnatvės turtus ir pažintų paslaptį Dievo—Tėvo ir Kristaus,
2Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
3kuriame slypi visi išminties ir pažinimo turtai.
3Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
4Jums tai sakau, kad niekas jūsų nesuvedžiotų įtikinančia kalba.
4Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
5Nors kūnu esu toli nuo jūsų, tačiau dvasia su jumis ir džiaugiuosi, matydamas jūsų tvarką ir jūsų tikėjimo Kristumi tvirtumą.
5Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
6Taigi, kaip esate priėmę Viešpatį Jėzų Kristų, taip ir gyvenkite Jame,
6Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
7įsišakniję bei statydindamiesi Jame ir įsitvirtinę tikėjime, kaip esate išmokyti, kupini dėkingumo.
7Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
8Žiūrėkite, kad kas jūsų nepavergtų filosofija ir tuščia apgaule, kuri remiasi žmonių tradicijomis ir pasaulio pradmenimis, o ne Kristumi.
8Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
9Jame kūniškai gyvena visa Dievybės pilnatvė,
9Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
10ir jūs esate tobuli Jame, kuris yra kiekvienos kunigaikštystės ir valdžios galva.
10nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
11Jame jūs taip pat esate apipjaustyti ne rankomis atliktu apipjaustymu, bet kūno nuodėmių, kūniškumo nusirengimuKristaus apipjaustymu.
11Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
12Su Juo palaidoti krikšte, kuriame jūs buvote ir prikelti, tikėdami jėga Dievo, prikėlusio Jį iš numirusių.
12Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
13Ir jus, mirusius nusikaltimais ir jūsų kūno neapipjaustymu, Jis atgaivino kartu su Juo, atleisdamas visus nusikaltimus.
13Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
14Jis ištrynė skolos raštą su mus kaltinančiais reikalavimais, raštą, kuris buvo prieš mus, ir panaikino jį, prikaldamas prie kryžiaus.
14alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
15Jis nuginklavo kunigaikštystes bei valdžias ir viešai jas pažemino, triumfuodamas prieš jas ant kryžiaus.
15Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
16Taigi niekas tenesmerkia jūsų dėl valgio ar gėrimo, dėl švenčių, jauno mėnulio ar sabato dienų.
16Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
17Visa tai tėra būsimųjų dalykų šešėlis, o kūnas yra Kristaus.
17Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
18Niekas teneatima jūsų atlygio, pamėgęs tariamą nusižeminimą ir angelų garbinimą, pasinėręs į tai, ko nėra matęs, be pagrindo pasipūtęs savo kūniškais samprotavimais,
18Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
19nesijungdamas su Galva, iš kurios visas kūnas, sąnariais ir raiščiais aprūpinamas bei jungiamas vienybėn, auga Dievo teikiamu ūgiu.
19na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
20Jei su Kristumi mirėte pasaulio pradmenims, tai kodėl gi, tarsi tebegyvendami pasaulyje, pasiduodate nuostatoms
20Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
21(“Neliesk! Neragauk! Neimk!”
21"Msishike hiki," "Msionje kile," "Msiguse kile!"
22visa tai vartojama dingsta.) pagal žmonių priesakus bei doktrinas?
22Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
23Tiesa, tai atrodo išmintingai dėl susikurto pamaldumo, tariamo nusižeminimo ir kūno varginimo, tačiau neturi jokios vertės ir pasotina kūniškumą.
23Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.