1Paulius, Dievo valia Jėzaus Kristaus apaštalas, šventiesiems, gyvenantiems Efeze, ir ištikimiesiems Kristuje Jėzuje.
1Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2Malonė jums ir ramybė nuo Dievo, mūsų Tėvo, ir Viešpaties Jėzaus Kristaus!
2Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3Tebūna palaimintas Dievas, mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Tėvas, kuris palaimino mus Kristuje visais dvasiniais palaiminimais danguje,
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4mus išrinkdamas Jame prieš pasaulio sutvėrimą, kad būtume šventi ir nekalti meile Jo akivaizdoje.
4Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5Geros valios nutarimu Jis iš anksto paskyrė mus įsūnyti per Jėzų Kristų
5Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6Jo malonės šlovės gyriui, kuria padarė mus priimtinus Mylimajame.
6Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7Jame turime atpirkimą per Jo kraują ir nuodėmių atleidimą pagal turtus Jo malonės,
7Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8kurią Jis dosniai suteikė mums su visa išmintimi ir supratimu,
8aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9paskelbdamas mums savo valios paslaptį pagal savo palankumą, kaip nusprendė savyje,
9Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10kad, laikų pilnatvei atėjus, galėtų suvienyti Kristuje visa, kas yra tiek danguje, tiek ir žemėje.
10Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11Jame ir gavome palikimą, iš anksto paskirtą sutvarkymu To, kuris visa veikia pagal savo valios nutarimą,
11Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12kad pasitarnautume Jo šlovės gyriui mes, kurie nuo seno turėjome viltį Kristuje.
12Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13Jame ir jūs, išgirdę tiesos žodį jūsų išgelbėjimo Evangelijąir įtikėję Juo, esate užantspauduoti pažadėtąja Šventąja Dvasia,
13Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14kuri yra mūsų paveldėjimo užstatas iki nuosavybės atpirkimo Jo šlovės gyriui.
14Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15Todėl ir aš, išgirdęs apie jūsų tikėjimą Viešpačiu Jėzumi ir apie jūsų meilę visiems šventiesiems,
15Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16nesiliauju dėkojęs už jus, prisimindamas jus savo maldose,
16sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17kad mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Dievas, šlovės Tėvas, duotų jums išminties ir apreiškimo dvasią Jo pažinimui
17ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18ir apšviestų jūsų širdies akis, kad pažintumėte, kokia yra Jo pašaukimo viltis, kokie Jo palikimo šlovės turtai šventuosiuose
18Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19ir kokia beribė Jo jėgos didybė mums, kurie tikime, veikiant jo galingai jėgai.
19mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20Ja Jis veikė Kristuje, prikeldamas Jį iš numirusių ir pasodindamas savo dešinėje danguose,
20aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21aukščiau už kiekvieną kunigaikštystę, valdžią, jėgą, viešpatystę ir už kiekvieną vardą, tariamą ne tik šiame amžiuje, bet ir būsimajame,
21Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao.
22ir visa paklojo po Jo kojomis, o Jį patį pastatė viršum visko, kad būtų galva bažnyčios,
22Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23kuri yra Jo kūnas, pilnatvė To, kuris visa visame pripildo.
23Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.