Lithuanian

Swahili: New Testament

Ephesians

2

1Ir jūs buvote mirę nusikaltimais ir nuodėmėmis,
1Ninyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa na dhambi zenu.
2kuriuose kadaise gyvenote pagal šio pasaulio būdą, paklusdami kunigaikščiui, viešpataujančiam ore, dvasiai, kuri dabar veikia neklusnumo vaikuose.
2Wakati ule mliishi kufuatana na mtindo mbaya wa ulimwengu huu, mkawa mnamtii mtawala wa pepo wenye nguvu wa anga, pepo ambao huwatawala sasa watu wasiomtii Mungu.
3Tarp jų kadaise ir mes visi gyvenome, sekdami savo kūno geiduliais, vykdydami kūno ir minčių troškimus, ir iš prigimties buvome rūstybės vaikai kaip ir kiti.
3Na hata sisi sote tulikuwa kama wao; tuliishi kufuatana na tamaa zetu za kidunia na kufanya tu mambo yale yaliyoipendeza miili na akili zetu. Kidunia, sisi kama vile pia wao, tulistahili ghadhabu ya Mungu.
4Bet Dievas, apstus gailestingumo, iš savo didžios meilės, kuria mus pamilo,
4Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa mapendo yasiyopimika,
5mus, mirusius nusikaltimais, atgaivino kartu su Kristumi,­malone jūs esate išgelbėti,­
5hata, ingawa tulikuwa tumekufa kwa sababu ya dhambi, alitufanya hai pamoja na Kristo. Kwa neema ya Mungu ninyi mmeokolewa.
6kartu prikėlė ir pasodino danguje Kristuje Jėzuje,
6Kwa kuungana na Kristo Yesu, Mungu alitufufua pamoja naye, tukatawale pamoja naye mbinguni.
7kad ateinančiais amžiais savo gerumu parodytų mums beribius savo malonės turtus Kristuje Jėzuje.
7Ndivyo alivyopenda kuonyesha kwa watu wa nyakati za baadaye, ukuu wa neema yake aliyotujalia kwa ukarimu katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.
8Nes jūs esate išgelbėti malone per tikėjimą, ir tai ne iš jūsų­tai Dievo dovana,
8Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu.
9ir ne dėl darbų, kad kas nors nesigirtų.
9Wala halitokani na matendo yenu wenyewe, asije mtu akajivunia kitu.
10Mes esame Jo kūrinys, sukurti Kristuje Jėzuje geriems darbams, kuriuos Dievas iš anksto paskyrė mums atlikti.
10Sisi ni viumbe vyake Mungu, na kwa kuungana na Kristo Yesu, alituumba kwa ajili ya kuishi maisha ya matendo mema aliyotutayarishia tuyatende.
11Todėl atsiminkite, kad jūs kadaise buvote kūnu pagonys, kuriuos vadino neapipjaustytais vadinamieji apipjaustytieji, apipjaustyti kūne rankomis.
11Ninyi mlio kwa asili watu wa mataifa mengine--mnaoitwa, "wasiotahiriwa" na Wayahudi ambao hujiita, "Waliotahiriwa," (kwa sababu ya kile wanachoifanyia miili yao) --kumbukeni mlivyokuwa zamani.
12Tuo metu jūs buvote be Kristaus, atskirti nuo Izraelio bendruomenės, svetimi pažado sandoroms, be vilties ir be Dievo pasaulyje.
12Wakati ule ninyi mlikuwa bila Kristo; mlikuwa nje ya jamii ya Israeli; mlikuwa wageni na hamkuwa na sehemu yoyote katika lile agano la zile ahadi. Mlikuwa bila matumaini Mungu hapa duniani.
13Bet dabar Kristuje Jėzuje jūs, kadaise buvusieji toli, per Kristaus kraują tapote artimi.
13Lakini sasa, kwa kuungana na Kristo Yesu, ninyi ambao hapo awali mlikuwa mbali, mmekaribishwa kwa njia ya damu yake Kristo.
14Nes mūsų sutaikinimas yra Jis, iš abejų padaręs viena ir sugriovęs mus skyrusią sieną,
14Maana Kristo mwenyewe ametuletea amani kwa kuwafanya Wayahudi na watu wa mataifa mengine kuwa jamii moja. Kwa mwili wake yeye mwenyewe aliubomoa ule ukuta uliowatenganisha na kuwafanya maadui.
15savo kūnu panaikinęs priešybę­ įsakymų Įstatymą su jo potvarkiais,­kad iš dviejų sutvertų savyje naują žmogų ir atneštų taiką.
15Aliiondoa ile Sheria ya Wayahudi pamoja na amri zake na kanuni zake, ili kutokana na jamii hizo mbili aumbe jamii moja mpya katika umoja naye na hivyo kuleta amani.
16Jis viename kūne abejus sutaikino su Dievu per kryžių, kuriuo ir sugriovė priešiškumą.
16Kwa mwili wake, Kristo aliuangamiza uadui wao; kwa msalaba wake aliziunganisha jamii hizo kuwa moja na kuzipatanisha na Mungu.
17Atėjęs Jis skelbė taiką jums, kurie buvote toli, ir tiems, kurie buvo arti,
17Basi, Kristo alikuja akahubiri Habari Njema ya amani kwenu ninyi watu wa mataifa mengine mliokuwa mbali na Mungu, na pia kwa Wayahudi ambao walikuwa karibu na Mungu.
18nes per Jį vieni ir kiti galime prieiti prie Tėvo viena Dvasia.
18Hivyo, kwa njia yake, sisi sote, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, tunaweza kumwendea Baba katika Roho mmoja.
19Todėl jūs jau nebesate pašaliniai nei svetimšaliai, bet šventųjų bendrapiliečiai ir Dievo namiškiai,
19Basi, ninyi si wageni tena, wala si watu wa nje; ninyi ni raia pamoja na watu wa Mungu, na ni watu wa jamaa ya Mungu.
20pastatyti ant apaštalų ir pranašų pamato, turintys kertiniu akmeniu patį Jėzų Kristų,
20Mmejengwa juu ya msingi uliowekwa na mitume na manabii, naye Kristo mwenyewe ndiye jiwe kuu la msingi.
21ant kurio darniai auga visas pastatas į šventą šventyklą Viešpatyje,
21Yeye ndiye mwenye kulitengeneza jengo lote na kulikuza hata liwe hekalu takatifu kwa ajili ya B wana.
22ant kurio ir jūs esate drauge statomi kaip Dievo buveinė Dvasioje.
22Katika kuungana naye, ninyi pia mnajengwa pamoja na wote wengine, muwe makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.