Lithuanian

Swahili: New Testament

Ephesians

6

1Jūs, vaikai, klausykite Viešpatyje savo tėvų, nes tai teisinga.
1Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2“Gerbk savo tėvą ir motiną”,­ tai pirmasis įsakymas su pažadu:
2"Waheshimu Baba na mama yako," hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3“Kad tau gerai sektųsi ir ilgai gyventum žemėje”.
3"Upate fanaka na miaka mingi duniani."
4Ir jūs, tėvai, neerzinkite savo vaikų, bet auklėkite juos drausmindami ir mokydami Viešpatyje.
4Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5Jūs, vergai, klausykite savo žemiškųjų šeimininkų su baime ir drebėjimu, nuoširdžiai kaip Kristaus,
5Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6ne dėl akių tarnaudami, lyg žmonėms įtinkantys, bet kaip Kristaus vergai, iš širdies vykdantys Dievo valią.
6Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7Noriai tarnaukite kaip Viešpačiui, o ne žmonėms,
7Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8žinodami, jog kiekvienas, tiek vergas, tiek laisvasis, jei daro ką gera, gaus atlyginimą iš Viešpaties.
8Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9Ir jūs, šeimininkai, tą patį darykite jiems. Liaukitės grasinę, žinodami, kad ir jiems, ir jums yra Viešpats danguje ir Jis nedaro skirtumo tarp asmenų.
9Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10Pagaliau, mano broliai, būkite stiprūs Viešpatyje ir Jo galybės jėga.
10Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11Apsirenkite visa Dievo ginkluote, kad galėtumėte pasipriešinti prieš velnio klastas.
11Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12Nes mes grumiamės ne su kūnu ir krauju, bet su kunigaikštystėmis, valdžiomis, šio amžiaus tamsybių valdovais ir dvasinėmis blogio jėgomis danguje.
12Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza.
13Todėl imkitės visų Dievo ginklų, kad galėtumėte piktą dieną pasipriešinti ir, visa atlaikę, išstovėti.
13Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14Tad stovėkite susijuosę savo strėnas tiesa, apsivilkę teisumo šarvais
14Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15ir apsiavę kojas pasiruošimu skelbti taikos Evangeliją.
15na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16O svarbiausia, pasiimkite tikėjimo skydą, su kuriuo užgesinsite visas liepsnojančias piktojo strėles.
16Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17Pasiimkite ir išgelbėjimo šalmą bei Dvasios kalaviją, tai yra Dievo žodį,
17Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18visada melsdamiesi Dvasioje visokeriopomis maldomis ir prašymu. Ištvermingai budėkite, malda užtardami visus šventuosius
18Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19ir mane, kad, man atvėrus lūpas, būtų duotas žodis drąsiai atskleisti Evangelijos paslaptį,
19Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20kurios pasiuntinys esu ir būdamas kalinys,­kad turėčiau drąsos kalbėti taip, kaip privalau kalbėti.
20Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21Kad ir jūs sužinotumėte, kaip man einasi ir ką veikiu, visa papasakos jums Tichikas, mylimas brolis ir ištikimas tarnas Viešpatyje.
21Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22Aš tam jį ir pasiunčiau, kad jūs sužinotumėte apie mus ir kad jis paguostų jūsų širdis.
22Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23Broliams ramybė ir meilė su tikėjimu nuo Dievo Tėvo ir Viešpaties Jėzaus Kristaus.
23Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24Malonė visiems, kurie nuoširdžiai myli mūsų Viešpatį Jėzų Kristų! Amen.
24Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.