Lithuanian

Swahili: New Testament

Ephesians

5

1Taigi būkite Dievo sekėjai, kaip mylimi vaikai,
1Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2ir gyvenkite mylėdami, kaip ir Kristus pamilo mus ir atidavė už mus save kaip atnašą ir kvapią auką Dievui.
2Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3Todėl ištvirkavimas, visoks netyrumas ar godumas tenebūna net minimi pas jus, kaip pridera šventiesiems;
3Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4taip pat nešvankumas, kvaila šneka ar juokų krėtimas jums netinka, verčiau tebūna dėkojimas.
4Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5Nes jūs žinote, kad joks ištvirkėlis, netyras ar gobšas, kuris yra stabmeldys, nepaveldės Kristaus ir Dievo karalystės.
5Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6Tegul niekas neapgauna jūsų tuščiais plepalais; už tokius dalykus Dievo rūstybė ištinka neklusnumo vaikus.
6Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7Todėl nebūkite jų bendrai!
7Basi, msishirikiane nao.
8Juk kadaise buvote tamsa, o dabar esate šviesa Viešpatyje. Elkitės kaip šviesos vaikai,­
8Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9nes Dvasios vaisius reiškiasi visokeriopu gerumu, teisumu ir tiesa,­
9maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10ištirdami, kas patinka Viešpačiui.
10Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11Ir neprisidėkite prie nevaisingų tamsos darbų, o verčiau atskleiskite juos.
11Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12Nes ką jie slapčia daro, gėda net sakyti.
12Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13Bet viskas, kas atskleidžiama, tampa šviesos apšviesta, o kas tik apšviesta, yra šviesa.
13Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14Todėl sakoma: “Pabusk, kuris miegi, kelkis iš numirusių, ir apšvies tave Kristus”.
14na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: "Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza."
15Todėl rūpestingai žiūrėkite, kaip elgiatės: kad nebūtumėte kaip kvailiai, bet kaip išmintingi,
15Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16branginantys laiką, nes dienos yra piktos.
16Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17Nebūkite tad neprotingi, bet supraskite, kokia yra Viešpaties valia.
17Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18Ir nepasigerkite vynu, kuriame pasileidimas, bet būkite pilni Dvasios,
18Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19kalbėdami vieni kitiems psalmėmis, himnais bei dvasinėmis giesmėmis, giedodami ir šlovindami savo širdyse Viešpatį,
19Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20visada ir už viską dėkodami Dievui Tėvui mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus vardu,
20Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21paklusdami vieni kitiems Dievo baimėje.
21Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22Jūs, žmonos, būkite klusnios savo vyrams lyg Viešpačiui,
22Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23nes vyras yra žmonos galva, kaip ir Kristus yra galva bažnyčios,­Jis kūno gelbėtojas.
23Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24Todėl kaip bažnyčia paklūsta Kristui, taip ir žmonos visame kame teklauso savo vyrų.
24Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25Jūs, vyrai, mylėkite savo žmonas, kaip ir Kristus pamilo bažnyčią ir atidavė už ją save,
25Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26kad ją pašventintų, apvalydamas vandens nuplovimu ir žodžiu,
26Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27kad pristatytų sau šlovingą bažnyčią, neturinčią dėmės nei raukšlės, nei nieko tokio, bet šventą ir nesuteptą.
27kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28Taip ir vyrai turi mylėti savo žmonas kaip savo kūnus. Kas myli savo žmoną, myli save patį.
28Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29Juk niekas niekada nėra nekentęs savo kūno, bet jį maitina ir globoja kaip ir Kristus bažnyčią.
29(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30Mes gi esame Jo kūno nariai, iš Jo kūno ir kaulų.
30maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31“Todėl žmogus paliks tėvą bei motiną ir susijungs su savo žmona, ir du taps vienu kūnu”.
31Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
32Tai didelė paslaptis,­aš tai sakau, žvelgdamas į Kristų ir bažnyčią.
32Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33Taigi kiekvienas iš jūsų tegul myli savo žmoną taip, kaip save patį, o žmona tegerbia savo vyrą.
33Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.