Lithuanian

Swahili: New Testament

Galatians

4

1Dabar pasakysiu: kol paveldėtojas vaikas, jis nieku nesiskiria nuo vergo, nors yra visko šeimininkas;
1Basi, nasema hivi: mrithi, akiwa bado mtoto, hawi tofauti na mtumwa ingawaje mali yote ni yake.
2jis esti globėjų ir prižiūrėtojų valdžioje iki tėvo nustatyto meto.
2Wakati huo wote yuko chini ya walezi na wadhamini mpaka wakati ule uliowekwa na baba yake.
3Taip buvo ir su mumis: kol buvome vaikai, turėjome vergauti pasaulio pradmenims.
3Hali kadhalika na sisi tulipokuwa bado watoto, tulikuwa watumwa wa pepo watawala wa ulimwengu.
4Bet, atėjus laiko pilnatvei, Dievas atsiuntė savo Sūnų, gimusį iš moters, pavaldų įstatymui,
4Lakini wakati ule maalumu ulipotimia, Mungu alimtuma Mwanawe aliyezaliwa na mwanamke, akaishi chini ya Sheria
5kad atpirktų esančius įstatymo valdžioje ir kad mes įgytume įsūnystę.
5apate kuwakomboa wale waliokuwa chini ya Sheria ili sisi tufanywe wana wa Mungu.
6O kadangi esate sūnūs, Dievas atsiuntė į mūsų širdis savo Sūnaus Dvasią, kuri šaukia: “Aba, Tėve!”
6Kwa vile sasa ninyi ni wana, Mungu amemtuma Roho wa Mwanae mioyoni mwenu, Roho ambaye hulia "Aba," yaani "Baba."
7Taigi tu jau nebe vergas, bet sūnus; o jeigu sūnus, tai ir Dievo paveldėtojas per Kristų.
7Basi, wewe si mtumwa tena, bali mwana. Na ikiwa ni mwana, basi, wewe utapokea yote Mungu aliyowawekea watoto wake.
8Kitados, dar nepažindami Dievo, jūs vergavote dievams, kurie iš tikro nėra dievai.
8Zamani hamkumjua Mungu na hivyo mkatumikia miungu isiyo miungu kweli.
9Bet dabar, pažinę Dievą arba, geriau sakant, Dievo pažinti,­ kaipgi galite grįžti prie menkų ir vargingų pradmenų, kuriems ir vėl norite vergauti?!
9Lakini sasa, kwa vile mnamjua Mungu, au tuseme mnajulikana na Mungu, mnawezaje tena kurudi kwa wale pepo maskini na dhaifu hata kutaka kuwatumikia tena?
10Jūs laikotės dienų, mėnesių, laikotarpių, metų.
10Bado mnaadhimisha siku, miezi na miaka!
11Aš baiminuosi dėl jūsų, kad kartais nebūčiau veltui dirbęs jūsų labui.
11Nahofu kwamba labda kazi niliyoifanya kwa ajili yenu imepotea bure!
12Prašau jus, broliai, tapkite tokie kaip aš, nes ir aš tapau toks kaip jūs. Jūs visai neįžeidėte manęs.
12Ndugu, nawasihi muwe kama mimi, kwa vile hata mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea ubaya wowote.
13Jūs žinote, kad jums pirmą kartą paskelbiau Evangeliją negaluodamas kūnu.
13Mnajua kwamba ugonjwa wangu ndio ulionipatia fursa ya kuwahubirieni Habari Njema kwa mara ya kwanza.
14Ir jūs nepaniekinote ir nepasipiktinote mano kūne esančiu išbandymu, bet priėmėte mane kaip Dievo angelą, kaip patį Kristų Jėzų.
14Hata hivyo, wakati ule hamkunidharau wala kunikataa kwa sababu ya udhaifu wangu ingawa mlishawishiwa kufanya hivyo; lakini mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama vile ningekuwa Kristo Yesu mwenyewe.
15Koks tai buvo palaiminimas jums! Aš galiu paliudyti, kad įmanydami būtumėte išlupę savo akis ir atidavę man.
15Mlikuwa wenye furaha; sasa kumetokea nini? Naapa kwamba wakati ule mngaliweza hata kuyang'oa macho yenu na kunipa mimi.
16Nejaugi tapau jūsų priešu, kalbėdamas jums tiesą?
16Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa sababu ya kuwaambieni ukweli?
17Jie uolūs ne jūsų labui, bet norėtų jus atskirti, kad būtumėte uolūs dėl jų.
17Hao watu wengine wanawahangaikia ninyi, lakini nia zao si njema. Wanataka kuwatenganisha nami ili ninyi muwahangaikie wao.
18Bet gerai visada būti uoliems dėl gero, o ne vien kai esu pas jus.
18Kwa kweli ni jambo jema daima kuwahangaikia wengine katika mambo mema, na si tu wakati mimi nipo pamoja nanyi.
19Mano vaikeliai, dėl jūsų aš vėl gimdymo skausmuose, kol jumyse išryškės Kristus!
19Watoto wangu, kama vile mama mja mzito anavyotaabika wakati wa kujifungua, mimi nataabika tena kwa ajili yenu mpaka hapo hali yake Kristo itakapoundwa ndani yenu.
20Norėčiau dabar būti pas jus ir prabilti kitaip, nes nežinau, ką man su jumis daryti.
20Laiti ningekuwa pamoja nanyi sasa, maana ningalipata msimamo ufaao juu yenu! Nina wasiwasi sana nanyi!
21Pasakykite man jūs, norintieji būti įstatymo valdžioje, ar negirdite įstatymo?
21Niambieni, enyi mnaopenda kutawaliwa na sheria: Je, mnasikia isemavyo Sheria?
22Juk parašyta, kad Abraomas turėjo du sūnus: vieną iš vergės, o kitą iš laisvosios.
22Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Abrahamu alikuwa na watoto wawili: mmoja kwa mwanamke mtumwa, na wa pili kwa mwanamke huru.
23Vergės sūnus buvo gimęs pagal kūną, o laisvosios­pagal pažadą.
23Yule wa mwanamke mtumwa alizaliwa kama kawaida, lakini yule wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.
24Tai pasakyta perkeltine prasme: jos­tai dvi Sandoros. Viena nuo Sinajaus kalno, gimdanti vergystei,­tai Hagara.
24Mambo hayo yamekuwa mfano; mama hao wawili ni mfano wa maagano mawili; la kwanza ni lile lililofanyika mlimani Sinai, mwakilishi wake ni Hagari, na watoto wake wanazaliwa utumwani.
25Hagara yra Sinajaus kalnas Arabijoje; ji atitinka dabartinę Jeruzalę, kuri vergauja su savo vaikais.
25Hagari anawakilisha mlima Sinai ulioko Arabia, na ni mfano wa Yerusalemu ya sasa, ulio mtumwa pamoja na watoto wake.
26Bet aukštybių Jeruzalė laisva, ji yra visų mūsų motina,
26Lakini Yerusalemu ya juu mbinguni ni mji ulio huru, nao ni mama yetu.
27nes parašyta: “Pralinksmėk, nevaisingoji, kuri negimdei! Šūkauk ir džiūgauk, nepažinusi kentėjimų! Nes apleistoji turi daug daugiau vaikų negu turinčioji vyrą”.
27Maana imeandikwa: "Furahi, ewe uliye tasa usiyezaa; paaza sauti wewe usiyepata kujifungua mtoto; maana watoto wa yule aliyeachwa ni wengi zaidi kuliko wa yule aliye na mume."
28Mes, broliai, esame pažado vaikai kaip Izaokas.
28Sasa, basi, ndugu zangu, ninyi ni watoto wa Mungu kutokana na ahadi yake kama alivyokuwa Isaka.
29Bet kaip tada gimęs pagal kūną persekiojo gimusį pagal Dvasią, taip ir dabar.
29Lakini kama vile siku zile yule mtoto aliyezaliwa kwa njia ya kawaida alimdhulumu yule aliyezaliwa kwa uwezo wa Roho wa Mungu, vivyo hivyo na siku hizi.
30O ką gi sako Raštas?­“Išvaryk vergę ir jos sūnų, nes vergės sūnus negaus palikimo kartu su laisvosios sūnumi”.
30Lakini Maandiko Matakatifu yasemaje? Yasema: "Mfukuze mama mtumwa pamoja na mwanawe; maana mtoto wa mtumwa hatarithi pamoja na mtoto wa mama huru."
31Taigi, broliai, mes nesame vergės vaikai, bet laisvosios.
31Kwa hiyo, basi, ndugu, sisi si watoto wa mtumwa bali wa mama huru.