1O neprotingi galatai! Kas jus, kuriems akivaizdžiai buvo nupieštas Jėzus Kristus tarsi pas jus nukryžiuotas, apkerėjo, kad nepaklustumėte tiesai?
1Enyi Wagalatia, mmekuwa wajinga kweli! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kusulubiwa kwake Yesu Kristo ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.
2Noriu jus paklausti tiktai vieno dalyko: ar jūs gavote Dvasią įstatymo darbais, ar klausydami tikėjimo?
2Napenda kujua tu kitu kimoja kutoka kwenu: Je, mlipokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kutimiza matakwa ya Sheria ama kwa sababu ya kuisikia na kuiamini Habari Njema?
3Nejaugi jūs tokie neprotingi, kad, pradėję Dvasia, dabar užbaigsite kūnu?
3Je, mu wajinga kiasi hicho? Ninyi mlianza yote kwa msaada wa Roho je, mnataka sasa kumaliza kwa nguvu zenu wenyewe?
4Ar tiek daug iškentėjote veltui? Jei iš tiesų būtų veltui!
4Je, mambo yale yote yaliyowapata ninyi yamekuwa bure tu? Haiwezekani!
5Ar Tas, kuris jums teikia Dvasią ir pas jus daro stebuklus, tai daro per įstatymo darbus, ar dėl tikėjimo klausymo?
5Je, Mungu huwajalia Roho na kutenda miujiza kati yenu ati kwa sababu mnatimiza yanayotakiwa na sheria, ama kwa sababu mnasikia Habari Njema na kuiamini?
6Taip “Abraomas patikėjo Dievu, ir tai jam buvo įskaityta teisumu”.
6Chukueni kwa mfano habari za Abrahamu: yeye alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.
7Todėl supraskite, kad Abraomo sūnūs yra tie, kurie tiki.
7Sasa basi jueni kwamba watu wenye kumwamini ndio walio watoto halisi wa Abrahamu.
8Ir Raštas, numatydamas, kad Dievas tikėjimu išteisins pagonis, iš anksto paskelbė Abraomui Evangeliją: “Tavyje bus palaimintos visos tautos”.
8Maandiko Matakatifu yalionyesha kabla kwamba Mungu atawakubali watu wa mataifa kuwa waadilifu kwa njia ya imani. Hivyo Maandiko Matakatifu yalitangulia kumtangazia Abrahamu Habari Njema: "Katika wewe mataifa yote yatabarikiwa."
9Taip tikintys susilaukia palaiminimo kartu su tikinčiuoju Abraomu.
9Basi, wale walio na imani wanabarikiwa pamoja na Abrahamu aliyeamini.
10Visi, kurie remiasi įstatymo darbais, yra prakeikimo galioje, nes parašyta: “Prakeiktas kiekvienas, kuris nuolatos nesilaiko visko, kas įstatymo knygoje parašyta, ir to nevykdo”.
10Lakini wote wanaotegemea tu kutimiza yanayotakiwa na Sheria, wako chini ya laana. Maana, Maandiko Matakatifu yasema: "Yeyote asiyeshika na kutimiza yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria, yuko chini ya laana."
11Kad įstatymu niekas neišteisinamas Dievo akyse, aišku, nes “teisusis gyvens tikėjimu”.
11Ni dhahiri kwamba Sheria haiwezi kumfanya mtu akubaliwe kuwa mwadilifu; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Mwadilifu kwa imani ataishi."
12O įstatymas nėra kilęs iš tikėjimo, bet “kas juos vykdo, tas gyvens jais”.
12Lakini Sheria haitegemei imani, ila Maandiko yasema: "Mwenye kutimiza yanayotakiwa na Sheria ataishi."
13Kristus mus atpirko iš įstatymo prakeikimo, tapdamas už mus prakeikimu, nes parašyta: “Prakeiktas kiekvienas, kuris kybo ant medžio”,
13Kristo alitukomboa kutoka katika laana ya Sheria kwa kujitwalia laana hiyo kwa ajili yetu; maana Maandiko yanasema: "Yeyote aliyetundikwa msalabani amelaaniwa."
14kad Abraomo palaiminimas Jėzuje Kristuje atitektų pagonims ir mes tikėjimu gautume pažadėtąją Dvasią.
14Jambo hili lilifanyika kusudi ile baraka aliyopewa Abrahamu iwashukie watu wa mataifa mengine kwa njia ya Kristo, na ili kwa imani, tumpokee yule Roho ambaye Mungu alituahidia.
15Broliai, kalbu, kaip įprasta žmonėms: net žmogaus testamento, kuris patvirtintas, niekas neatmeta ir nepapildo.
15Ndugu, nitawapeni mfano kutoka maisha yetu ya kila siku. Fikirini juu ya mkataba kati ya watu wawili. Mkataba ukisha fanyika na kutiwa sahihi hapana mtu anayeuweka kando au kuuongezea kitu.
16Pažadai buvo duoti Abraomui ir jo palikuoniui. Jis nesako “ir palikuonims”, ne daugeliui, bet kaip apie vieną: “ir tavo palikuoniui”, kuris yra Kristus.
16Basi, Abrahamu alipewa ahadi, yeye pamoja na mzawa wake. Maandiko hayasemi: "Na wazawa wake," yaani wengi, bali yasema, "Na mzawa wake," yaani mmoja, naye ndiye Kristo.
17Noriu pasakyti, kad Dievo Kristuje anksčiau patvirtinto testamento negali panaikinti po keturių šimtų trisdešimties metų atsiradęs įstatymas, ir jis negali pažado paversti negaliojančiu.
17Ninachotaka kusema ni hiki: Mungu alifanya agano lake akalithibitisha; Sheria ambayo ilitokea miaka mia nne na thelathini baadaye, haiwezi kulitangua hilo agano wala kuibatilisha hiyo ahadi.
18Jei paveldėjimas būtų iš įstatymo, tai jau nebe iš pažado, o Dievas davė tai Abraomui pažadu.
18Maana, kama urithi ya Mungu inategemea Sheria, basi, haiwezi kutegemea tena ahadi ya Mungu. Kumbe, lakini Mungu alimkirimia Abrahamu kwa sababu aliahidi.
19Tad kam gi reikalingas įstatymas? Jis buvo pridėtas dėl nusižengimų, kol ateis palikuonis, kuriam buvo skirtas pažadas; įstatymas buvo perduotas per angelus, tarpininko ranka.
19Ya nini basi, Sheria? Iliongezwa hapo ili kuonyesha uhalifu ni kitu gani, mpaka atakapokuja yule mzawa wa Abrahamu aliyepewa ile ahadi. Sheria ililetwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20Tarpininkas neatstovauja vienai pusei, bet Dievas yra vienas.
20Ama hakika, mpatanishi hahitajiwi ikiwa jambo lenyewe lamhusu mtu mmoja; na Mungu ni mmoja.
21Tad gal įstatymas priešingas Dievo pažadams? Anaiptol! Jei būtų duotas įstatymas, galintis suteikti gyvenimą, tai iš tikrųjų teisumas būtų iš įstatymo.
21Je, Sheria inapingana na ahadi za Mungu? Hata kidogo! Maana, kama kungalitolewa sheria ambayo ingeweza kuwapa watu uzima, basi, tungeweza kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya Sheria.
22Bet Raštas viską apjuosė nuodėme, kad pažadas dėl tikėjimo Jėzumi Kristumi tektų tiems, kurie tiki.
22Lakini sivyo; Maandiko Matakatifu yamekwisha sema kwamba ulimwengu wote upo chini ya utawala wa dhambi; na hivyo, kwa kumwamini Yesu Kristo, wenye kuamini watimiziwe ile ahadi.
23Prieš ateinant tikėjimui, buvome įstatymo įkalinti, kad lauktume apsireiškiant tikėjimo.
23Kabla ya kujaliwa imani, Sheria ilitufanya wafungwa mpaka imani hiyo iliyokuwa inakuja ifunuliwe.
24Todėl įstatymas buvo mūsų auklėtojas, vedęs į Kristų, kad būtume tikėjimu išteisinti.
24Basi, hiyo Sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani, tukubaliwe kuwa waadilifu.
25Bet, tikėjimui atėjus, jau nesame auklėtojo globoje.
25Tangu kufika kwa hiyo imani, Sheria si mlezi wetu tena.
26Juk jūs visi esate Dievo sūnūs per tikėjimą Jėzumi Kristumi.
26Kwa njia ya imani, ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika kuungana na Kristo.
27Ir visi, kurie esate pakrikštyti Kristuje, apsivilkote Kristumi.
27Ninyi nyote mliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaa Kristo.
28Nebėra nei žydo, nei graiko; nebėra nei vergo, nei laisvojo; nebėra nei vyro, nei moters: visi esate viena Kristuje Jėzuje!
28Hivyo, hakuna tena tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki, mtumwa na mtu huru, mwanamume na mwanamke. Nyote ni kitu kimoja katika kuungana na Kristo Yesu.
29O jeigu esate Kristaus, tai esate Abraomo palikuonys ir paveldėtojai pagal pažadą.
29Ikiwa ninyi ni wa Kristo, basi ni wazawa wa Abrahamu, na mtapokea yale aliyoahidi Mungu.