Lithuanian

Swahili: New Testament

Galatians

2

1Paskui, po keturiolikos metų, vėl nuvykau į Jeruzalę kartu su Barnabu, pasiėmęs ir Titą.
1Baada ya miaka kumi na minne, nilikwenda tena Yerusalemu pamoja na Barnaba; nilimchukua pia Tito pamoja nami.
2Nuvykau, apreiškimo paskatintas, ir jiems išdėsčiau Evangeliją, kurią skelbiu pagonims, atskirai išsiaiškindamas su įžymesniais asmenimis, kad kartais nebėgčiau ar nebūčiau bėgęs veltui.
2Kwenda kwangu kulitokana na ufunuo alionipa Mungu. Katika kikao cha faragha niliwaeleza hao viongozi ujumbe wa Habari Njema niliohubiri kwa watu wa mataifa. Nilifanya hivyo kusudi kazi yangu niliyokuwa nimefanya, na ile ninayofanya sasa isije ikawa bure.
3Jie nevertė apsipjaustyti nė mano palydovo Tito, kuris buvo graikas.
3Lakini, hata mwenzangu Tito, ambaye ni Mgiriki, hakulazimika kutahiriwa,
4Tačiau netikriems broliams, paslapčia įslinkusiems iššnipinėti mūsų laisvę, kurią turime Kristuje Jėzuje, ir norėjusiems mus pavergti,­
4ingawa kulikuwa na ndugu wengine wa uongo waliotaka atahiriwe. Watu hawa walijiingiza kwa ujanja na kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika kuungana na Kristo Yesu, ili wapate kutufanya watumwa.
5jiems nė valandėlei nepasidavėme, kad Evangelijos tiesa pasiliktų su jumis.
5Hatukukubaliana nao hata kidogo ili ukweli wa Habari Njema ubaki nanyi daima.
6O dėl tariamai įžymesniųjų asmenų,­kas jie bebuvo, man nesvarbu, nes Dievas nėra žmonėms šališkas,­man įžymesnieji asmenys nieko nepridėjo.
6Lakini watu hawa wanaosemekana kuwa ni viongozi--kama kweli walikuwa hivyo au sivyo, kwangu si kitu, maana Mungu hahukumu kwa kuangalia mambo ya nje--watu hawa hawakuwa na kitu cha kuongeza katika Habari hii Njema kama niihubirivyo.
7Atvirkščiai, pamatę, jog man patikėta skelbti Evangeliją neapipjaustytiesiems kaip Petrui apipjaustytiesiems
7Badala yake, walitambua kwamba Mungu alikuwa amenituma kuhubiri Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kama vile Petro alivyokuwa ametumwa kuihubiri kwa Wayahudi.
8(nes Tas, kuris veikė su Petru jam apaštalaujant apipjaustytiesiems, veikė taip pat su manimi tarp pagonių)
8Maana, yule aliyemwezesha Petro kuwa mtume kwa Wayahudi, ndiye aliyeniwezesha nami pia kuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine.
9ir pastebėję man suteiktą malonę, Jokūbas, Kefas ir Jonas, kurie laikomi šulais, padavė man ir Barnabui dešines draugystės ženklan, kad eitume pas pagonis, o jie pas apipjaustytuosius;
9Basi, Yakobo, Kefa na Yohane, ambao waonekana kuwa viongozi wakuu, walitambua kwamba Mungu alinijalia neema hiyo, wakatushika sisi mkono, yaani Barnaba na mimi, iwe ishara ya ushirikiano. Sisi ilitupasa tukafanye kazi kati ya watu wa mataifa mengine, na wao kati ya Wayahudi.
10tik mes turėjome prisiminti vargšus,­o aš ir stengiausi tai daryti.
10Wakatuomba lakini kitu kimoja: tuwakumbuke maskini; jambo ambalo nimekuwa nikijitahidi kutekeleza.
11Kai Petras atvyko į Antiochiją, aš jam pasipriešinau į akis, nes jis nusižengė.
11Lakini Kefa alipofika Antiokia nilimpinga waziwazi maana alikuwa amekosea.
12Mat prieš atvykstant kai kuriems nuo Jokūbo, jis valgydavo su pagonimis; bet kai tie atvyko, jis atsitraukė ir vengė jų, bijodamas apipjaustytųjų.
12Awali, kabla ya watu kadhaa waliokuwa wametumwa na Yakobo kuwasili hapo, Petro alikuwa akila pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini, baada ya hao watu kufika, aliacha kabisa kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa kuogopa kikundi cha waliosisitiza tohara.
13Kartu su juo veidmainiavo ir kiti žydai, netgi Barnabas pasidavė veidmainystei.
13Hata ndugu wengine Wayahudi walimuunga mkono Petro katika kitendo hiki cha unafiki, naye Barnaba akakumbwa na huo unafiki wao.
14Pamatęs, kad jie nukrypsta nuo Evangelijos tiesos, pasakiau Petrui visų akivaizdoje: “Jei tu, būdamas žydas, gyveni pagoniškai, o ne žydiškai, tai kodėl verti pagonis gyventi taip, kaip žydai?”
14Basi, nilipoona kuwa msimamo wao kuhusu ukweli wa Habari Njema haukuwa umenyooka, nikamwambia Kefa mbele ya watu wote: "Ingawa wewe ni Myahudi, unaishi kama watu wa mataifa mengine na si kama Myahudi! Unawezaje, basi kujaribu kuwalazimisha watu wa mataifa mengine kuishi kama Wayahudi?"
15Nors iš prigimties esame žydai ir ne pagonių kilmės nusidėjėliai,
15Kweli, sisi kwa asili ni Wayahudi, na si watu wa mataifa mengine hao wenye dhambi!
16žinome, jog žmogus neišteisinamas įstatymo darbais, bet tikėjimu į Jėzų Kristų. Mes įtikėjome Kristų Jėzų, kad būtume išteisinti Kristaus tikėjimu, o ne įstatymo darbais; nes įstatymo darbais nebus išteisintas nė vienas žmogus.
16Lakini, tunajua kwa hakika kwamba mtu hawezi kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, bali tu kwa kumwamini Yesu Kristo. Na sisi pia tumemwamini Yesu Kristo ili tupate kukubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani yetu kwa Kristo, na si kwa kuitii Sheria.
17Bet, ieškant mums išteisinimo per Kristų, paaiškėja, kad mes patys esame nusidėjėliai. Ar Kristus dėl to yra nuodėmės tarnas? Jokiu būdu!
17Sasa, ikiwa katika kutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu kwa kuungana na Kristo sisi tunaonekana kuwa wenye dhambi, je, jambo hili lina maana kwamba Kristo anasaidia utendaji wa dhambi? Hata kidogo!
18Nes jeigu aš vėl atstatau, ką buvau išgriovęs, tai tampu nusikaltėliu.
18Lakini ikiwa ninajenga tena kile nilichokwisha bomoa, basi nahakikisha kwamba mimi ni mhalifu.
19Aš per įstatymą numiriau įstatymui, kad gyvenčiau Dievui.
19Maana, kuhusu Sheria hiyo, mimi nimekufa; Sheria yenyewe iliniua, nipate kuishi kwa ajili ya Mungu. Mimi nimeuawa pamoja na Kristo msalabani,
20Esu nukryžiuotas su Kristumi. Ir daugiau ne aš gyvenu, o gyvena manyje Kristus. Ir dabar, gyvendamas kūne, gyvenu tikėjimu į Dievo Sūnų, kuris pamilo mane ir paaukojo save už mane.
20na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu.
21Neatstumiu Dievo malonės, nes jei teisumas įgyjamas įstatymu, tuomet Kristus mirė veltui.
21Sipendi kuikataa neema ya Mungu. Kama mtu huweza kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya Sheria, basi, Kristo alikufa bure!