Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

3

1Todėl, šventieji broliai, dangiškojo pašaukimo dalininkai, įsižiūrėkite mūsų išpažinimo Apaštalą ir vyriausiąjį Kunigą Jėzų Kristų,
1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2kuris buvo ištikimas Jį paskyrusiam, kaip ir Mozė visuose Jo namuose.
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3Juk Jis yra pripažintas vertu didesnės šlovės už Mozę, kaip didesnės pagarbos vertas statytojas už namą.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4Mat kiekvienas namas kažkieno pastatytas, o viską pastatęs yra Dievas.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5Ir Mozė buvo ištikimas visuose Jo namuose kaip tarnas, kad paliudytų tai, kas ateity turėjo būti pasakyta.
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6O Kristus kaip Sūnus viešpatauja Jo namuose, ir tie namai esame mes, jei pasitikėjimą ir tvirtą vilties pasigyrimą išsaugosime iki galo.
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7Todėl, kaip Šventoji Dvasia sako: “Jei šiandien išgirsite Jo balsą,
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8neužkietinkite savo širdžių, kaip per maištą, gundymo dieną dykumoje,
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9kur jūsų tėvai gundė mane, mėgino ir matė mano darbus per keturiasdešimt metų.
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10Todėl Aš užpykau ant tos kartos ir pasakiau: ‘Visada jie klysta savo širdyje ir nepažino mano kelių’.
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11Taigi Aš prisiekiau savo rūstybėje: ‘Jie neįeis į mano poilsį!’ ”
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
12Žiūrėkite, broliai, kad kuris iš jūsų nebūtų piktos, netikinčios širdies, atitolusios nuo gyvojo Dievo.
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13Verčiau raginkite vieni kitus kasdien,­kol dar sakoma “šiandien”,­kad kurio iš jūsų neužkietintų nuodėmės klasta.
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14Juk mes esame tapę Kristaus dalininkais,­jei tik išlaikysime tvirtą pradinį pasitikėjimą iki galo,
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15kol yra sakoma: “Šiandien, jei išgirsite Jo balsą, neužkietinkite savo širdžių kaip per maištą”.
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
16Kas gi buvo tie, kurie išgirdę maištavo? Ar ne visi Mozės išvestieji iš Egipto?
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17Ant ko Jis buvo užpykęs per keturiasdešimt metų? Ar ne ant nusidėjusių, kurių lavonai krito dykumoje?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18O kam prisiekė, jog neįeis į Jo poilsį, jei ne tiems, kurie nepakluso?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19Taigi matome, kad jie negalėjo įeiti dėl netikėjimo.
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.