Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

2

1Todėl turime būti labai dėmesingi tam, ką girdėjome, kad nepraplauktume pro šalį.
1Kwa sababu hiyo tunapaswa kuzingatia kwa makini zaidi yote tuliyosikia, ili tusije tukapotoshwa.
2Nes jei per angelus paskelbtas žodis buvo tvirtas ir kiekvienas nusižengimas bei neklusnumas susilaukdavo teisėto atlygio,
2Ujumbe ule waliopewa wazee wetu na malaika ulionyeshwa kuwa kweli, hata mtu yeyote ambaye hakuufuata au hakuutii aliadhibiwa kama alivyostahili.
3tai kaipgi pabėgsime mes, nepaisydami tokio didžio išgelbėjimo? Jis, prasidėjęs Viešpaties skelbimu, buvo mums patvirtintas tų, kurie Jį girdėjo,
3Basi, sisi tutaokokaje kama hatuujali wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu, na wale waliomsikia walituthibitishia kwamba ni kweli.
4Dievui liudijant ženklais ir stebuklais, visokiais galingais darbais ir Šventosios Dvasios dovanomis, paskirstytomis Jo valia.
4Mungu pia aliongeza hapo ushahidi wake kwa kufanya kila namna ya miujiza na maajabu, na kwa kuwagawia watu vipaji vya Roho Mtakatifu kadiri ya mapenzi yake.
5Ne angelams Jis pajungė ateities pasaulį, apie kurį kalbame.
5Mungu hakuwaweka malaika wautawale ulimwengu ujao, yaani ulimwengu ule tunaoongea habari zake.
6Bet kažkas kažkur paliudijo, sakydamas: “Kas yra žmogus, kad jį atsimeni, ar žmogaus sūnus, kad juo rūpiniesi?
6Tena yasemwa mahali fulani katika Maandiko: "Mtu ni nini ee Mungu, hata umfikirie; mwanaadamu ni nini hata umjali?
7Padarei jį trumpam laikui žemesnį už angelus, šlove ir garbe jį apvainikavai ir pastatei jį virš savo rankų darbų,
7Ulimfanya kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8visa paklojai po jo kojomis”. Jeigu jau visa paklojo, tai nepaliko nieko, kas nebūtų jam paklota. Vis dėlto dabar mes dar nematome, jog visa jam paklota.
8ukaweka kila kitu chini ya miguu yake, avitawale." Yasemwa kwamba Mungu alimweka mtu kuwa mtawala wa vitu vyote yaani bila kuacha hata kimoja. Hata hivyo, hatuoni bado mtu akivitawala vitu vyote sasa.
9Bet matome Tą, trumpam laikui padarytą žemesnį už angelus­Jėzų, už mirties kentėjimus apvainikuotą šlove ir garbe. Reikėjo, kad Dievo malone už kiekvieną Jis paragautų mirties.
9Lakini twamwona Yesu ambaye alifanywa kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika, ili kwa neema ya Mungu afe kwa ajili ya watu wote. Sasa tunamwona ametawazwa kwa utukufu na heshima kwa sababu ya kifo alichoteseka.
10Nes Tam, dėl kurio ir iš kurio yra viskas, priderėjo, vedant daugybę vaikų į garbę, kentėjimais ištobulinti jų išgelbėjimo Vadovą.
10Ilikuwa haki tupu kwamba Mungu, ambaye huumba na kutegemeza vitu vyote, alimfanya Yesu kuwa mkamilifu kabisa kwa njia ya mateso, ili awalete watoto wengi waushiriki utukufu wake. Maana Yesu ndiye anayewaongoza kwenye wokovu.
11Juk šventintojas ir šventinamieji­visi kyla iš vieno. Todėl Jis nesigėdija juos vadinti broliais,
11Yeye anawatakasa watu dhambi zao, naye pamoja na wale waliotakaswa, wote wanaye Baba mmoja. Ndiyo maana Yesu haoni aibu kuwaita hao ndugu zake;
12sakydamas: “Aš paskelbsiu Tavo vardą savo broliams, vidury susirinkimo Tave šlovinsiu giesme”.
12kama asemavyo: "Ee Mungu, nitawatangazia ndugu zangu matendo yako. Nitakusifu katika kusanyiko lao."
13Ir vėl: “Aš Juo pasitikėsiu”. Ir vėl: “Štai Aš ir mano vaikai, kuriuos man davė Dievas”.
13Tena asema: "Nitamwekea Mungu tumaini langu." Na tena: "Mimi niko hapa pamoja na watoto alionipa Mungu."
14Kadangi vaikų kraujas ir kūnas bendri, tai ir Jis lygiomis juos prisiėmė, kad mirtimi sunaikintų tą, kuris turėjo mirties jėgą, tai yra velnią,
14Basi, kwa vile watoto hao, kama awaitavyo, ni watu wenye mwili na damu, Yesu mwenyewe akawa kama wao na kushiriki ubinadamu wao. Alifanya hivyo ili kwa njia ya kifo chake amwangamize Ibilisi, ambaye ana mamlaka juu ya kifo,
15ir išvaduotų tuos, kurie, bijodami mirties, visam gyvenimui buvo patekę į vergiją.
15na hivyo awaokoe wale waliokuwa watumwa maisha yao yote kwa sababu ya hofu yao ya kifo.
16Iš tiesų Jam rūpėjo ne angelai, o Abraomo palikuonys.
16Maana ni wazi kwamba yeye hakuja kwa ajili ya kuwasaidia malaika, bali kama yasemavyo Maandiko; "Anawasaidia wazawa wa Abrahamu."
17Todėl Jis turėjo visu kuo tapti panašus į brolius, kad būtų gailestingas ir ištikimas Dievui vyriausiasis Kunigas ir permaldautų už žmonių nuodėmes.
17Ndiyo maana ilimbidi awe kama ndugu zake kwa kila namna, ili awe Kuhani Mkuu wao aliye mwaminifu na mwenye huruma katika kumtumikia Mungu, ili dhambi za watu ziondolewe.
18Pats iškentęs gundymus, Jis gali padėti tiems, kurie yra gundomi.
18Na, anaweza sasa kuwasaidia wale wanaojaribiwa na kuteswa.