Lithuanian

Swahili: New Testament

John

10

1“Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: kas neįeina pro vartus į avių gardą, bet įlipa pro kur kitur, tas vagis ir plėšikas.
1Yesu alisema "Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang'anyi.
2O kas pro vartus įeina, tas avių ganytojas.
2Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.
3Jam sargas atidaro, ir avys klauso jo balso. Jis šaukia savąsias avis vardais ir jas išveda.
3Mngoja mlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake, naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake na kuwaongoza nje.
4Išsivaręs savąsias avis, jis eina priešakyje, o avys paskui jį seka, nes pažįsta jo balsą.
4Akisha watoa nje huwatangulia mbele nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake.
5O paskui svetimą jos neseks, bet nuo jo bėgs, nes nepažįsta svetimųjų balso”.
5Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake."
6Jėzus pasakė jiems tą palyginimą, bet jie nesuprato, ką tai reiškia.
6Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.
7Tuomet Jėzus kalbėjo jiems toliau: “Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: Aš­avių vartai.
7Basi, akasema tena, "Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.
8Visi, kurie pirma manęs atėjo, buvo vagys ir plėšikai, todėl avys jų neklausė.
8Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyang'anyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.
9Aš esu vartai. Jei kas įeis per mane, bus išgelbėtas. Jis įeis ir išeis ir ganyklą sau ras.
9Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.
10Vagis ateina tik vogti, žudyti ir naikinti. Aš atėjau, kad jie turėtų gyvenimą,­kad apsčiai jo turėtų.
10Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uzima--uzima kamili.
11Aš esu gerasis ganytojas. Geras ganytojas už avis guldo savo gyvybę.
11"Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.
12O samdinys, ne ganytojas, kuriam avys ne savos, pamatęs sėlinantį vilką, palieka avis ir pabėga, o vilkas griebia jas ir išsklaido.
12Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.
13Samdinys pabėga, nes jis samdinys, jam avys nerūpi.
13Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.
14Aš esu gerasis ganytojas: Aš pažįstu savąsias, ir manosios pažįsta mane.
14Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi,
15Kaip mane pažįsta Tėvas, taip ir Aš pažįstu Tėvą ir už avis guldau savo gyvybę.
15kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.
16Ir kitų avių turiu, kurios ne iš šios avidės; ir jas man reikia atvesti; jos girdės mano balsą, ir bus viena kaimenė, vienas ganytojas.
16Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
17Todėl Tėvas myli mane, kad Aš guldau savo gyvybę, jog ir vėl ją pasiimčiau.
17"Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
18Niekas neatima jos iš manęs, bet Aš pats ją atiduodu. Aš turiu galią ją atiduoti ir turiu galią vėl ją pasiimti; tokį įsakymą gavau iš savo Tėvo”.
18Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye."
19Tarp žydų vėl kilo nesutarimas dėl šitų žodžių.
19Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20Daugelis iš jų sakė: “Jis turi demoną ir šėlsta. Kodėl Jo klausote?”
20Wengi wao wakasema, "Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?"
21Kiti tvirtino: “Tai ne demono apsėstojo kalbos. Argi gali demonas atverti neregiui akis?!”
21Wengine wakasema, "Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?"
22Jeruzalėje buvo Šventyklos pašventinimo šventė. Buvo žiema.
22Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya Kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi.
23Jėzus vaikščiojo šventykloje, po Saliamono stoginę.
23Naye Yesu akawa anatembea Hekaluni katika ukumbi wa Solomoni.
24Ten Jį apstojo žydai ir ėmė klausinėti: “Kaip ilgai laikysi mus abejonėse? Jeigu esi Kristus, pasakyk mums atvirai!”
24Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, "Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, basi, tuambie wazi."
25Jėzus jiems atsakė: “Aš jums sakiau, bet jūs netikite. Darbai, kuriuos darau savo Tėvo vardu, liudija apie mane.
25Yesu akawajibu, "Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.
26Bet jūs netikite, nes jūs­ne iš manųjų avių, kaip jums ir sakiau.
26Lakini ninyi hamsadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
27Manosios avys girdi mano balsą; Aš jas pažįstu, ir jos seka paskui mane.
27Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.
28Aš duodu joms amžinąjį gyvenimą; jos nepražus per amžius, ir niekas jų neišplėš iš mano rankos.
28Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.
29Mano Tėvas, kuris man jas davė, yra aukščiau už viską, ir niekas negali jų išplėšti iš mano Tėvo rankos.
29Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wale hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.
30Aš ir Tėvas esame viena”.
30Mimi na Baba, tu mmoja."
31Tada žydai vėl stvėrėsi akmenų, norėdami Jį užmėtyti.
31Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.
32O Jėzus paklausė jų: “Daug gerų darbų esu jums parodęs iš savo Tėvo. Už kurį gi darbą užmėtysite mane akmenimis?”
32Yesu akawaambia, "Nimewaonyesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?"
33Žydai Jam atsakė: “Ne už gerą darbą užmėtysime Tave akmenimis, bet už piktžodžiavimą ir kad Tu, būdamas žmogus, dediesi Dievu”.
33Wayahudi wakamjibu, "Hatukupigi mawe kwa ajili ya tendo jema, ila kwa sababu ya kukufuru! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu."
34Jėzus jiems atsakė: “Argi jūsų Įstatyme nėra parašyta: ‘Aš tariau: jūs esat dievai’?
34Yesu akawajibu, "Je, haikuandikwa katika Sheria yenu: Mimi nimesema, ninyi ni miungu?
35Jeigu Jis vadina dievais tuos, kuriems skirtas Dievo žodis (o Raštas negali būti panaikintas),
35Mungu aliwaita miungu wale waliopewa neno lake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima.
36kaip tad jūs galite sakyti Tam, kurį Tėvas pašventino ir pasiuntė į pasaulį: ‘Tu piktžodžiauji’, kai Jis pasakė: ‘Aš esu Dievo Sūnus!’?
36Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: Unakufuru, eti kwa sababu nilisema: Mimi ni Mwana wa Mungu?
37Jei Aš nedarau savo Tėvo darbų,­ netikėkite manimi!
37Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini.
38O jeigu darau ir manimi netikite,­tikėkite darbais, kad pažintumėte ir patikėtumėte, jog Tėvas manyje ir Aš Jame”.
38Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."
39Tuomet jie vėl norėjo Jį suimti, bet Jis ištrūko jiems iš rankų.
39Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao.
40Jėzus vėl pasitraukė anapus Jordano, kur pirma Jonas krikštijo, ir apsistojo ten.
40Yesu akaenda tena ng'ambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko.
41Daugelis atėjo pas Jį ir kalbėjo: “Jonas nepadarė nė vieno ženklo, bet ką jis sakė apie šį žmogų, yra teisybė”.
41Watu wengi walimwendea wakasema, "Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa."
42Ir daugelis tenai Jį įtikėjo.
42Watu wengi mahali hapo wakamwamini.