Lithuanian

Swahili: New Testament

John

11

1Buvo vienas ligonis, Lozorius iš Betanijos kaimo, kur gyveno Marija ir jos sesuo Morta.
1Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2Marija buvo ta pati moteris, kuri patepė Viešpatį kvepalais ir nušluostė savo plaukais Jo kojas. Jos brolis Lozorius sirgo.
2Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3Todėl seserys nusiuntė Jam žinią: “Viešpatie! Tas, kurį Tu myli, serga!”
3Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: "Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!"
4Tai išgirdęs, Jėzus tarė: “Šita liga ne mirčiai, bet Dievo šlovei, kad per ją būtų pašlovintas Dievo Sūnus”.
4Yesu aliposikia hivyo akasema, "Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe."
5Jėzus mylėjo Mortą, jos seserį ir Lozorių.
5Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6Taigi išgirdęs, kad tasai serga, Jis dar dvi dienas užtruko ten, kur buvo.
6Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7Po to pasakė mokiniams: “Eikime vėl į Judėją!”
7Kisha akawaambia wanafunzi wake, "Twendeni tena Yudea!"
8Mokiniai Jam atsakė: “Rabi, ką tik žydai kėsinosi užmėtyti Tave akmenimis, o Tu vėl ten eini?”
8Wanafunzi wakamwambia, "Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?"
9Jėzus tarė: “Argi ne dvylika valandų turi diena? Kas vaikščioja dieną, tas nesuklumpa, nes mato šio pasaulio šviesą.
9Yesu akajibu, "Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10O kas vaikščioja naktį, suklumpa, nes jame nėra šviesos”.
10Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake."
11Tai pasakęs, pridūrė: “Mūsų bičiulis Lozorius užmigo, bet Aš einu jo pažadinti”.
11Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, "Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha."
12Jo mokiniai atsiliepė: “Viešpatie, jeigu jis miega, pasveiks”.
12Wanafunzi wake wakamwambia, "Bwana, ikiwa amelala, basi atapona."
13Tačiau Jėzus kalbėjo apie jo mirtį, o jie manė, kad Jis kalba apie poilsio miegą.
13Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14Pagaliau Jėzus atvirai jiems pasakė: “Lozorius mirė.
14Basi, Yesu akawaambia waziwazi, "Lazaro amekufa;
15Ir Aš džiaugiuosi, kad ten nebuvau,­dėl jūsų, kad tikėtumėte. Tad eikime pas jį”.
15Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake."
16Tuomet Tomas, vadinamas Dvyniu, tarė kitiems mokiniams: “Eikime ir mes numirti su Juo!”
16Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, "Twendeni nasi tukafe pamoja naye!"
17Atėjęs Jėzus rado Lozorių jau keturias dienas išgulėjusį kape.
17Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18O Betanija buvo arti Jeruzalės, maždaug penkiolika stadijų atstu.
18Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19Daug žydų buvo atėję pas Mortą ir Mariją paguosti jų dėl brolio.
19Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20Morta, išgirdusi ateinant Jėzų, išėjo Jo pasitikti. Marija sėdėjo namie.
20Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21Morta tarė Jėzui: “Viešpatie, jei būtum čia buvęs, mano brolis nebūtų miręs.
21Martha akamwambia Yesu, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22Bet ir dabar žinau: ko tik prašysi Dievo, Dievas Tau duos”.
22Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa."
23Jėzus jai pasakė: “Tavo brolis prisikels!”
23Yesu akamwambia, "Kaka yako atafufuka."
24Morta atsiliepė: “Aš žinau, jog jis prisikels prisikėlime, paskutinę dieną”.
24Martha akamjibu, "Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho."
25Jėzus jai tarė: “Aš esu prisikėlimas ir gyvenimas. Kas tiki mane, nors ir mirtų, bus gyvas.
25Yesu akamwambia, "Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26Ir kiekvienas, kuris gyvena ir tiki mane, nemirs per amžius. Ar tai tiki?”
26na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?"
27Ji atsakė: “Taip, Viešpatie! Aš tikiu, jog Tu esi Kristus, Dievo Sūnus, kuris turi ateiti į šį pasaulį”.
27Martha akamwambia, "Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni."
28Tai pasakiusi, ji nuėjo ir slapčiomis pašaukė savo seserį Mariją, jai pranešdama: “Mokytojas atėjo ir šaukia tave”.
28Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, "Mwalimu yuko hapa, anakuita."
29Išgirdusi ši greitai pakilo ir nuėjo pas Jį.
29Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30Jėzus dar nebuvo įėjęs į kaimą, bet tebebuvo toje vietoje, kur Jį pasitiko Morta.
30Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31Kai žydai, buvę su ja namuose ir ją guodę, pamatė ją skubiai keliantis ir išeinant, nusekė paskui, sakydami: “Ji eina prie kapo”.
31Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32Marija, atėjusi ten, kur buvo Jėzus, ir Jį pamačiusi, puolė Jam po kojų, sakydama: “Viešpatie, jei būtum čia buvęs, mano brolis nebūtų miręs”.
32Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, "Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!"
33Jėzus, pamatęs ją ir kartu atėjusius žydus verkiančius, sudejavo dvasioje ir susijaudinęs
33Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34paklausė: “Kur jį paguldėte?” Jie atsakė: “Viešpatie, eik ir pažiūrėk”.
34Kisha akawauliza, "Mlimweka wapi?" Wakamwambia, "Bwana, njoo uone."
35Jėzus pravirko.
35Yesu akalia machozi.
36Tada žydai ėmė kalbėti: “Štai kaip Jis jį mylėjo!”
36Basi, Wayahudi wakasema, "Tazameni jinsi alivyompenda!"
37O kiti sakė: “Argi Tas, kuris atvėrė neregiui akis, negalėjo padaryti, kad šitas nemirtų?”
37Lakini baadhi yao wakasema, "Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?"
38Ir vėl dejuodamas Jėzus atėjo prie kapo. Tai buvo ola, užrista akmeniu.
38Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39Jėzus tarė: “Nuriskite akmenį!” Mirusiojo sesuo Morta įspėjo: “Viešpatie, jis jau dvokia, nes jau keturios dienos, kai jis miręs”.
39Yesu akasema, "Ondoeni hilo jiwe!" Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, "Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!"
40Jėzus jai tarė: “Argi nesakiau tau, kad jei tikėsi, pamatysi Dievo šlovę?!”
40Yesu akamwambia, "Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?"
41Jie nurito akmenį nuo ten, kur gulėjo numirėlis. Jėzus pakėlė akis aukštyn ir prabilo: “Tėve, dėkoju Tau, kad mane išgirdai.
41Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, "Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42Aš žinojau, kad visada mane girdi. Tačiau tai sakau dėl čia esančiųjų, kad jie tikėtų, jog Tu esi mane siuntęs”.
42Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma."
43Tai pasakęs, Jis galingu balsu sušuko: “Lozoriau, išeik!”
43Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: "Lazaro! Toka nje!"
44Ir numirėlis išėjo. Jo rankos ir kojos buvo apvyniotos laidojimo aprišalais, veidas aprištas drobule. Jėzus jiems liepė: “Atvyniokite jį ir leiskite jam eiti”.
44Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, "Mfungueni, mkamwache aende zake."
45Daugelis žydų, kurie buvo atėję pas Mariją ir matė, ką Jėzus padarė, įtikėjo Jį.
45Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46Bet kai kurie nuėjo pas fariziejus ir pranešė jiems, ką Jėzus padaręs.
46Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47Tada aukštieji kunigai ir fariziejai sušaukė sinedrioną ir svarstė: “Ką darysime? Šitas žmogus daro daug ženklų.
47kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, "Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48Jei taip Jį paliksime, visi įtikės Jį; ateis romėnai ir užims mūsų vietą bei tautą”.
48Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!"
49Vienas iš jų­Kajafas, tais metais vyriausiasis kunigas­jiems tarė: “Jūs nieko neišmanote
49Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, "Ninyi hamjui kitu!
50ir nepagalvojate, jog mums geriau, kad vienas žmogus mirtų už tautą, o ne visa tauta žūtų”.
50Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?"
51Jis tai pasakė ne iš savęs, bet, būdamas tų metų vyriausiasis kunigas, pranašavo, jog Jėzui reikės mirti už tautą,
51Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52ir ne tik už tautą, bet tam, kad suburtų į viena išsklaidytuosius Dievo vaikus.
52na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53Nuo tos dienos jie buvo nusprendę Jį nužudyti.
53Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54Todėl Jėzus nebevaikščiojo viešai tarp žydų, bet pasitraukė iš ten į vietovę netoli dykumos, į miestelį, vadinamą Efraimu, ir ten apsistojo kartu su savo mokiniais.
54Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55Artinosi žydų Pascha. Daugelis iš viso krašto prieš Paschą atėjo į Jeruzalę apsivalyti.
55Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56Jie ieškojo Jėzaus ir, stoviniuodami šventykloje, kalbėjosi: “Kaip jūs manote? Nejaugi Jis nebeateis į šventę?”
56Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, "Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?"
57Mat aukštieji kunigai ir fariziejai išleido įsakymą, kad žinantys praneštų, kur Jis esąs, kad galėtų Jį suimti.
57Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.