Lithuanian

Swahili: New Testament

John

2

1Trečią dieną Galilėjos Kanoje buvo vestuvės. Jose dalyvavo Jėzaus motina.
1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
2Į vestuves buvo pakviestas ir Jėzus, ir Jo mokiniai.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3Pritrūkus vyno, Jėzaus motina Jam sako: “Jie nebeturi vyno”.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
4Jėzus jai atsakė: “O kas man ir tau, moterie? Dar neatėjo mano valanda”.
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
5Jo motina tarė tarnams: “Darykite, ką tik Jis jums lieps”.
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
6Ten buvo šeši akmeniniai indai žydų apsiplovimams, kiekvienas dviejų trijų saikų talpos.
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7Jėzus jiems liepė: “Pripilkite indus vandens”. Jie pripylė sklidinus.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
8Tada Jis sakė: “Dabar semkite ir neškite stalo prižiūrėtojui”. Tie nunešė.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
9Paragavęs paversto vynu vandens ir nežinodamas, iš kur tai (bet tarnai, kurie sėmė vandenį, žinojo), prižiūrėtojas pasišaukė jaunikį
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
10ir tarė jam: “Kiekvienas žmogus pirmiau stato geresnio vyno, o kai svečiai įgeria, tuomet prastesnio. O tu laikei gerąjį vyną iki šiol”.
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
11Tokią stebuklų pradžią Jėzus padarė Galilėjos Kanoje. Taip Jis parodė savo šlovę, ir mokiniai įtikėjo Jį.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
12Paskui Jis su savo motina, broliais ir mokiniais nukeliavo į Kafarnaumą. Ten jie pasiliko kelias dienas.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
13Artėjant žydų Paschai, Jėzus nukeliavo į Jeruzalę.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14Šventykloje Jis rado prekiaujančių jaučiais, avimis, karveliais ir prisėdusių pinigų keitėjų.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
15Susukęs iš virvučių rimbą, Jis išvijo juos visus iš šventyklos, išvarė avis ir jaučius, išbarstė keitėjų pinigus ir išvartė stalus.
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
16Karvelių pardavėjams Jis sakė: “Pasiimkite visa tai iš čia ir iš mano Tėvo namų nedarykite prekybos namų!”
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
17Ir Jo mokiniai prisiminė, kad yra parašyta: “Uolumas dėl Tavo namų sugrauš mane”.
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
18Tada žydai kreipėsi į Jį, sakydami: “Kokį ženklą mums parodysi, jog turi teisę taip daryti?”
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
19Jėzus atsakė: “Sugriaukite šitą šventyklą, ir per tris dienas Aš ją atstatysiu!”
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
20Tada žydai sakė: “Keturiasdešimt šešerius metus šventyklą statė, o Tu atstatysi ją per tris dienas?!”
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
21Bet Jis kalbėjo apie savo kūno šventyklą.
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
22Todėl, Jam prisikėlus iš numirusių, Jo mokiniai prisiminė Jį apie tai kalbėjus ir jie įtikėjo Raštu ir Jėzaus pasakytu žodžiu.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
23Per Paschos šventę, Jam būnant Jeruzalėje, daugelis įtikėjo Jo vardą, matydami Jo daromus ženklus.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
24Bet Jėzus, gerai visus pažindamas, jais nepasitikėjo.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
25Jam nereikėdavo, kad kas paliudytų apie žmogų, nes Jis pats žinojo, kas yra žmoguje.
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.