1Buvo vienas fariziejus, vardu Nikodemas, žydų vyresnysis.
1Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
2Jis atėjo naktį pas Jėzų ir kreipėsi į Jį: “Rabi, mes žinome, kad esi mokytojas, atėjęs nuo Dievo, nes niekas negalėtų daryti tokių ženklų, kokius Tu darai, jeigu Dievas nebūtų su juo”.
2Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, "Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye."
3Jėzus jam atsakė: “Iš tiesų, iš tiesų sakau tau: jei kas negims iš naujo, negalės regėti Dievo karalystės”.
3Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu."
4Nikodemas paklausė: “Bet kaip gali gimti žmogus, būdamas senas? Argi jis gali antrą kartą įeiti į savo motinos įsčias ir gimti?”
4Nikodemo akamwuliza, "Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!"
5Jėzus atsakė: “Iš tiesų, iš tiesų sakau tau: jei kas negims iš vandens ir Dvasios, negalės įeiti į Dievo karalystę.
5Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
6Kas gimė iš kūno, yra kūnas, o kas gimė iš Dvasios, yra dvasia.
6Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
7Nesistebėk, jog pasakiau tau: jums būtina gimti iš naujo.
7Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
8Vėjas pučia, kur nori; jo ošimą girdi, bet nežinai, iš kur ateina ir kurlink nueina. Taip yra su kiekvienu, kuris gimė iš Dvasios”.
8Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho."
9Nikodemas atsiliepė: “Kaip tai gali būti?”
9Nikodemo akamwuliza, "Mambo haya yanawezekanaje?"
10Jėzus jam atsakė: “Tu esi Izraelio mokytojas ir šito nesupranti?
10Yesu akamjibu, "Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
11Iš tiesų, iš tiesų sakau tau: mes kalbame, ką žinome, ir liudijame, ką matėme, o jūs nepriimate mūsų liudijimo.
11Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
12Jei netikite man kalbant apie žemiškuosius dalykus, tai kaipgi tikėsite, jei kalbėsiu jums apie dangiškuosius?
12Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
13Niekas nėra pakilęs į dangų, kaip tik Tas, kuris nužengė iš dangaus,Žmogaus Sūnus, esantis danguje.
13Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
14Kaip Mozė dykumoje iškėlė gyvatę, taip turi būti iškeltas Žmogaus Sūnus,
14"Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
15kad kiekvienas, kuris Jį tiki, nepražūtų, bet turėtų amžinąjį gyvenimą”.
15ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele.
16Nes Dievas taip pamilo pasaulį, jog atidavė savo viengimį Sūnų, kad kiekvienas, kuris Jį tiki, nepražūtų, bet turėtų amžinąjį gyvenimą.
16Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
17Dievas gi nesiuntė savo Sūnaus į pasaulį, kad Jis pasaulį pasmerktų, bet kad pasaulis per Jį būtų išgelbėtas.
17Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
18Kas Jį tiki, tas neteisiamas, o kas netiki, jau yra pasmerktas už tai, kad netiki viengimio Dievo Sūnaus vardo.
18"Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
19O teismo nuosprendis yra toks: šviesa atėjo į pasaulį, bet žmonės labiau pamilo tamsą nei šviesą, nes jų darbai buvo pikti.
19Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
20Kiekvienas, kuris daro bloga, neapkenčia šviesos ir neina į šviesą, kad jo darbai nebūtų atskleisti.
20Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
21O kas vykdo tiesą, tas eina į šviesą, kad pasirodytų, jog jo darbai atlikti Dieve.
21Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu."
22Paskui Jėzus su savo mokiniais atėjo į Judėjos kraštą ir, ten su jais būdamas, krikštijo.
22Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
23Taip pat ir Jonas krikštijo Enone, netoli Salimo, nes ten buvo daug vandens ir žmonės ten ateidavo ir buvo krikštijami.
23Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
24Tada Jonas dar nebuvo įmestas į kalėjimą.
24(Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
25Tarp Jono mokinių ir vieno žydo kilo ginčas dėl apsivalymo.
25Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
26Tad jie atėjo pas Joną ir pranešė: “Rabi, Tas kuris buvo su tavimi anapus Jordano, apie kurį tu paliudijai,štai Jis krikštija, ir visi eina pas Jį”.
26Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, "Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea."
27Jonas atsakė: “Žmogus nieko negali pasiimti, jeigu jam neduota iš dangaus.
27Yohane akawaambia, "Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
28Jūs patys galite man paliudyti, jog sakiau: aš ne Kristus! Aš siųstas būti tik Jo pirmtaku.
28Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
29Kas turi sužadėtinę, tas sužadėtinis, o sužadėtinio bičiulis, kuris šalia stovi ir jį girdi, džiaugte džiaugiasi jaunikio balsu. Todėl šiam mano džiaugsmui jau nieko netrūksta.
29Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
30Jis turi augti, o ašmažėti”.
30Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
31Kas iš aukštybių ateina, Tas už visus viršesnis, o kas iš žemės, žemiškas yra ir žemiškai kalba. Kas iš dangaus ateina, Tas už visus viršesnis.
31"Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
32Jis liudija, ką matė ir girdėjo, tik niekas Jo liudijimo nepriima.
32Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
33O kas Jo liudijimą priima, tas pripažįsta, jog Dievas teisus,
33Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
34juk ką Dievas yra siuntęs, Tas kalba Dievo žodžius, nes Dievas teikia Dvasią be saiko.
34Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
35Tėvas myli Sūnų ir visa yra atidavęs į Jo rankas.
35Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
36Kas tiki Sūnų, turi amžinąjį gyvenimą, o kas netiki Sūnumigyvenimo nematys: ant jo pasilieka Dievo rūstybė.
36Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake."