1Pirmąją savaitės dieną, labai anksti, dar neišaušus, Marija Magdalietė atėjo prie kapo ir pamatė, kad akmuo nuo kapo nuristas.
1Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
2Ji nubėgo pas Simoną Petrą ir kitą mokinį, kurį Jėzus mylėjo, ir pranešė jiems: “Paėmė Viešpatį iš kapo, ir nežinome, kur Jį padėjo”.
2Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, "Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka."
3Petras ir tas kitas mokinys nuskubėjo prie kapo.
3Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4Bėgo abu kartu, bet tasai kitas mokinys pralenkė Petrą ir pirmas pasiekė kapą.
4Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5Pasilenkęs jis pamatė numestas drobules, tačiau į vidų nėjo.
5Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6Netrukus iš paskos atbėgo ir Simonas Petras. Jis įėjo į rūsį ir pamatė numestas drobules
6Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7ir skarą, buvusią ant Jėzaus galvos, ne su drobulėmis paliktą, bet suvyniotą ir atskirai padėtą.
7na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8Tada įėjo ir kitas mokinys, kuris pirmas buvo atbėgęs prie kapo. Jis pamatė ir įtikėjo.
8Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9Mat jie dar nebuvo supratę Rašto, kad Jis turėsiąs prisikelti iš numirusių.
9(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10Paskui mokiniai vėl sugrįžo namo.
10Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11O Marija stovėjo lauke prie kapo ir verkė. Verkdama ji pasilenkė, pažvelgė į kapo vidų
11Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12ir pamatė du angelus baltais drabužiais sėdinčiusvieną galvūgalyje, kitą kojų vietojeten, kur būta Jėzaus kūno.
12akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
13Jie paklausė ją: “Moterie, ko verki?” Ji atsakė: “Paėmė mano Viešpatį ir nežinau, kur Jį padėjo”.
13Hao malaika wakamwuliza, "Mama, kwa nini unalia?" Naye akawaambia, "Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!"
14Tai tarusi, ji atsisuko ir pamatė stovintį Jėzų, bet nepažino, kad tai Jėzus.
14Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
15Jėzus jai tarė: “Moterie, ko verki? Ko ieškai?” Ji, manydama, jog tai sodininkas, atsakė: “Gerbiamasis, jei tamsta Jį išnešei, pasakyk man, kur Jį padėjai. Aš Jį pasiimsiu”.
15Yesu akamwuliza, "Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?" Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, "Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua."
16Jėzus jai sako: “Marija!” Ji atsigręžė ir sušuko: “Rabuni!” (Tai reiškia: “Mokytojau”).
16Yesu akamwambia, "Maria!" Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, "Raboni" (yaani "Mwalimu").
17Jėzus jai tarė: “Neliesk manęs! Aš dar neįžengiau pas savo Tėvą. Eik pas mano brolius ir pasakyk jiems: ‘Aš žengiu pas savo Tėvą ir jūsų Tėvą, pas savo Dievą ir jūsų Dievą’ ”.
17Yesu akamwambia, "Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu."
18Marija Magdalietė nuėjo ir pranešė mokiniams, kad mačiusi Viešpatį ir ką Jis jai sakęs.
18Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
19Tos pirmosios savaitės dienos vakare, durims, kur buvo susirinkę mokiniai, dėl žydų baimės esant užrakintoms, atėjo Jėzus, atsistojo viduryje ir tarė: “Ramybė jums!”
19Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, "Amani kwenu!"
20Tai pasakęs, Jis parodė jiems rankas ir šoną. Mokiniai nudžiugo, išvydę Viešpatį.
20Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
21Jėzus vėl tarė: “Ramybė jums! Kaip mane siuntė Tėvas, taip ir Aš jus siunčiu”.
21Yesu akawaambia tena, "Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi."
22Tai pasakęs, Jis kvėpė į juos ir tarė: “Priimkite Šventąją Dvasią.
22Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, "Pokeeni Roho Mtakatifu.
23Kam atleisite nuodėmes, tiems jos bus atleistos, o kam sulaikysite,sulaikytos”.
23Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi."
24Vieno iš dvylikosTomo, vadinamo Dvyniu,nebuvo su jais, kai Jėzus atėjo.
24Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
25Tad kiti mokiniai jam kalbėjo: “Mes matėme Viešpatį!” O jis atsakė: “Jeigu aš nepamatysiu Jo rankose vinių dūrio ir neįleisiu piršto į vinių vietą, ir jeigu ranka nepaliesiu Jo šononetikėsiu”.
25Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, "Tumemwona Bwana." Thoma akawaambia, "Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki."
26Po aštuonių dienų Jo mokiniai vėl buvo kambaryje, ir Tomas su jais. Jėzus atėjo, durims esant užrakintoms, atsistojo viduryje ir prabilo: “Ramybė jums!”
26Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, "Amani kwenu!"
27Paskui kreipėsi į Tomą: “Įleisk čia pirštą ir pažiūrėk į mano rankas. Pakelk ranką ir paliesk mano šoną; nebūk netikintisbūk tikintis”.
27Kisha akamwambia Thoma, "Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!"
28Tomas atsakė Jam: “Mano Viešpats ir mano Dievas!”
28Thoma akamjibu, "Bwana wangu na Mungu wangu!"
29Jėzus jam tarė: “Tomai, tu įtikėjai, nes mane pamatei. Palaiminti, kurie tiki nematę!”
29Yesu akamwambia, "Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini."
30Savo mokinių akivaizdoje Jėzus padarė ir daug kitų ženklų, kurie nesurašyti šitoje knygoje.
30Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
31O šitie yra surašyti, kad tikėtumėte, jog Jėzus yra Kristus, Dievo Sūnus, ir kad tikėdami turėtumėte gyvenimą per Jo vardą.
31Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.