1Paskui Jėzus vėl pasirodė mokiniams prie Tiberiados ežero. Pasirodė taip.
1Baada ya hayo Yesu aliwatokea tena wanafunzi wake kando ya ziwa Tiberia. Aliwatokea hivi:
2Buvo drauge Simonas Petras, Tomas, vadinamas Dvyniu, Natanaelis iš Galilėjos Kanos, Zebediejaus sūnūs ir dar du kiti Jėzaus mokiniai.
2Simoni Petro, Thoma (aitwaye Pacha), na Nathanieli mwenyeji wa Kana Galilaya, wana wawili wa Zebedayo na wanafunzi wake wengine wawili, walikuwa wote pamoja.
3Simonas Petras jiems sako: “Einu žvejoti”. Jie pasisiūlė: “Ir mes einame su tavimi”. Nuėję jie tuojau sulipo į valtį, tačiau tą naktį nieko nesugavo.
3Simoni Petro aliwaambia, "Nakwenda kuvua samaki." Nao wakamwambia, "Nasi tutafuatana nawe." Basi, wakaenda, wakapanda mashua, lakini usiku huo hawakupata chochote.
4Rytui auštant, ant kranto pasirodė bestovįs Jėzus. Bet mokiniai nepažino, kad tai buvo Jėzus.
4Kulipoanza kupambazuka, Yesu alisimama kando ya ziwa, lakini wanafunzi hawakujua kwamba alikuwa yeye.
5O Jėzus jiems tarė: “Vaikeliai, ar neturite ko valgyti?” Jie atsakė: “Ne”.
5Basi, Yesu akawauliza, "Vijana, hamjapata samaki wowote sio?" Wao wakamjibu, "La! Hatujapata kitu."
6Tada Jis pasakė: “Užmeskite tinklą į dešinę nuo valties, ir pagausite”. Jie užmetė ir nebeįstengė jo patraukti dėl žuvų gausybės.
6Yesu akawaambia, "Tupeni wavu upande wa kulia wa mashua nanyi mtapata samaki." Basi, wakatupa wavu lakini sasa hawakuweza kuuvuta tena kwa wingi wa samaki.
7Tuomet tasai mokinys, kurį Jėzus mylėjo, sako Petrui: “Tai Viešpats!” Išgirdęs, jog tai Viešpats, Simonas Petras persijuosė drabužį,mat buvo neapsirengęs,ir šoko į ežerą.
7Hapo yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, "Ni Bwana!" Simoni Petro aliposikia ya kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa), akarukia majini.
8Kiti mokiniai atsiyrė valtimi, nes buvo netoli krantomaždaug už dviejų šimtų mastųir atitempė tinklą su žuvimis.
8Lakini wale wanafunzi wengine walikuja pwani kwa mashua huku wanauvuta wavu uliojaa samaki; hawakuwa mbali na nchi kavu, ila walikuwa yapata mita mia moja kutoka ukingoni.
9Išlipę į krantą, jie pamatė žėrinčias žarijas, ant jų padėtą žuvį ir duonos.
9Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.
10Jėzus jiems tarė: “Atneškite ką tik pagautų žuvų”.
10Yesu akawaambia, "Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua."
11Simonas Petras nuėjo ir išvilko į krantą tinklą, pilną didelių žuvų, iš viso šimtą penkiasdešimt tris. Nors jų buvo tokia gausybė, tačiau tinklas nesuplyšo.
11Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa mia moja na hamsini na watatu. Na ingawa walikuwa wengi hivyo wavu haukukatika.
12Jėzus tarė: “Eikite šen pusryčių!” Ir nė vienas iš mokinių neišdrįso paklausti: “Kas Tu esi?”, nes jie žinojo, jog tai Viešpats.
12Yesu akawaambia, "Njoni mkafungue kinywa." Hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kumwuliza: "Wewe ni nani?" Maana walijua alikuwa Bwana.
13Jėzus priėjo, paėmė duonos ir davė jiems, taip pat ir žuvies.
13Yesu akaja, akatwaa mkate akawapa; akafanya vivyo hivyo na wale samaki.
14Tai jau trečią kartą pasirodė savo mokiniams Jėzus, prisikėlęs iš numirusių.
14Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada ya kufufuka kutoka wafu.
15Papusryčiavus Jėzus paklausė Simoną Petrą: “Simonai, Jonos sūnau, ar myli mane labiau už šituos?” Jis atsakė: “Taip, Viešpatie, Tu žinai, kad Tave myliu”. Jėzus jam tarė: “Ganyk mano avinėlius”.
15Walipokwisha kula, Yesu alimwuliza Simoni Petro, "Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi zaidi kuliko hawa?" Naye akajibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza wana kondoo wangu."
16Ir antrą kartą Jėzus paklausė: “Simonai, Jonos sūnau, ar myli mane?” Tas atsiliepė: “Taip, Viešpatie, Tu žinai, kad Tave myliu”. Jėzus jam pasakė: “Ganyk mano avis”.
16Kisha akamwambia mara ya pili, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Petro akamjibu, "Naam, Bwana; wajua kwamba nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu."
17Jėzus paklausė trečią kartą: “Simonai, Jonos sūnau, ar myli mane?” Petras nuliūdo, kad Jis trečią kartą klausia: “Ar myli mane?”, ir atsakė: “Viešpatie, Tu viską žinai. Tu žinai, kad Tave myliu”. Jėzus jam tarė: “Ganyk mano avis.
17Akamwuliza mara ya tatu, "Simoni mwana wa Yohane! Je, wanipenda?" Hapo Petro akahuzunika kwa sababu alimwuliza mara ya tatu: "Wanipenda?" akamwambia, "Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda." Yesu akamwambia, "Tunza kondoo wangu!
18Iš tiesų, iš tiesų sakau tau: kai buvai jaunas, pats susijuosdavai ir vaikščiojai, kur norėjai. O pasenęs tu ištiesi rankas, ir kitas tave perjuos ir ves, kur tu nenori”.
18Kweli nakwambia, ulipokuwa kijana ulizoea kujifunga mshipi na kwenda kokote ulikotaka. Lakini utakapokuwa mzee utanyosha mikono yako, na mtu mwingine atakufunga na kukupeleka usikopenda kwenda."
19Jis tai pasakė, nurodydamas, kokia mirtimi Petras pašlovinsiąs Dievą. Tai pasakęs, dar pridūrė: “Sek paskui mane!”
19(Kwa kusema hivyo, alionyesha jinsi Petro atakavyokufa na kumtukuza Mungu.) Kisha akamwambia, "Nifuate."
20Petras atsisukęs pamatė iš paskos einantį mokinį, kurį Jėzus mylėjo, kuris vakarienės metu buvo prisiglaudęs prie Jėzaus krūtinės ir klausė: “Viešpatie, kas Tave išduos?”
20Hapo Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda, anafuata (Huyu mwanafunzi ndiye yule ambaye wakati wa chakula cha jioni, alikaa karibu sana na Yesu na kumwuliza: "Bwana ni nani atakayekusaliti?")
21Pamatęs jį, Petras tarė Jėzui: “Viešpatie, o kas bus šitam?”
21Basi, Petro alipomwona huyo akamwuliza Yesu, "Bwana, na huyu je?"
22Jėzus atsakė: “Jei Aš noriu, kad jis pasiliktų, kol ateisiu, kas gi tau? Tu sek paskui mane!”
22Yesu akamjibu, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini? Wewe nifuate mimi."
23Todėl pasklido šis žodis tarp brolių, jog tas mokinys nemirsiąs. Bet Jėzus nesakė, kad Jis nemirs, tik: “Jei noriu, kad jis pasiliktų, kol ateisiu, kas gi tau?”
23Basi, habari hiyo ikaenea miongoni mwa wale ndugu kwamba mwanafunzi huyo hafi. Lakini Yesu hakumwambia kwamba mwanafunzi huyo hafi, ila, "Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, yakuhusu nini?"
24Tai ir yra tas mokinys, kuris liudija apie tuos dalykus ir juos aprašė, ir mes žinome, kad jo liudijimas tikras.
24Huyo ndiye yule aliyeshuhudia mambo haya na kuyaandika. Nasi twajua kwamba aliyoyasema ni kweli.
25Yra dar daug kitų dalykų, kuriuos Jėzus padarė. Jeigu juos visus atskirai aprašytume, manau, kad visas pasaulis nesutalpintų knygų, kurios būtų parašytos. Amen.
25Kuna mambo mengine mengi aliyofanya Yesu, ambayo kama yangeandikwa yote, moja baada ya lingine, nadhani hata ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.