1Pirmoje knygoje, Teofiliau, aš parašiau apie viską, ką Jėzus pradėjo daryti ir mokyti
1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2iki tos dienos, kurią buvo paimtas į dangų, pirmiau per Šventąją Dvasią davęs savo išrinktiesiems apaštalams įsakymų.
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3Po savo kančios Jis pateikė jiems daugelį įrodymų, kad yra gyvas, per keturiasdešimt dienų jiems rodydamasis ir kalbėdamas apie Dievo karalystę.
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4Kartą, būdamas kartu su jais, liepė jiems nepasišalinti iš Jeruzalės, bet laukti Tėvo pažado,“apie kurį,pasakė Jis,esate girdėję iš manęs;
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5nes Jonas krikštijo vandeniu, o jūs po kelių dienų būsite pakrikštyti Šventąja Dvasia”.
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
6Susirinkusieji paklausė Jį: “Viešpatie, gal Tu šiuo metu atkursi Izraelio karalystę?”
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7Jis jiems tarė: “Ne jūsų reikalas žinoti laiką ir metą, kuriuos Tėvas nustatė savo valdžia.
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8Kai ant jūsų nužengs Šventoji Dvasia, jūs gausite jėgos ir tapsite mano liudytojais Jeruzalėje ir visoje Judėjoje bei Samarijoje ir lig pat žemės pakraščių”.
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9Tai pasakęs, jiems bežiūrint, Jėzus pakilo aukštyn, ir debesis Jį paslėpė nuo jų akių.
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10Kai jie, akių nenuleisdami, žiūrėjo į žengiantį dangun Jėzų, štai prie jų atsirado du vyrai baltais drabužiais
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11ir tarė: “Vyrai galilėjiečiai, ko stovite, žiūrėdami į dangų? Tas pats Jėzus, paimtas nuo jūsų į dangų, sugrįš taip pat, kaip Jį matėte žengiantį į dangų”.
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12Tuomet jie sugrįžo į Jeruzalę iš vadinamojo Alyvų kalno, esančio netoli Jeruzalės, tokiu atstumu, koks leidžiamas nueiti per sabatą.
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13Parėję jie susirinko aukštutiniame kambaryje, kur buvo apsistoję,Petras ir Jokūbas, Jonas ir Andriejus, Pilypas ir Tomas, Baltramiejus ir Matas, Alfiejaus sūnus Jokūbas, Simonas Uolusis ir Judas, Jokūbo brolis.
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14Jie visi ištvermingai ir vieningai atsidėjo maldai ir prašymui kartu su moterimis ir Jėzaus motina Marija bei Jo broliais.
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15Vieną dieną, atsistojęs tarp brolių,ten buvo susirinkę apie šimtą dvidešimt asmenų,Petras tarė:
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16“Vyrai broliai, turėjo išsipildyti Rašto žodžiai, kuriuos Šventoji Dvasia pranašiškai išsakė Dovydo lūpomis apie Judą, tapusį Jėzaus suėmėjų vadovu.
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17Jis juk buvo priskaitytas prie mūsų ir turėjo dalį šioje tarnystėje.
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18Bet jis nedorybės kaina įsigijo sklypą, paskui stačia galva puolė žemyn, perplyšo pusiau, ir visi jo viduriai išvirto.
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19Tai pasidarė žinoma visiems Jeruzalės gyventojams, ir anas sklypas jų kalba buvo pavadintas Hakeldamachu,tai reiškia: ‘Kraujo sklypas’.
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20Nes Psalmių knygoje parašyta: ‘Jo kiemas tepavirsta dykviete, ir tegul niekas ten nebegyvena’, ir: ‘Tegul kitas perima jo tarnystę’.
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21Taigi vienam iš vyrų, kurie drauge su mumis vaikščiojo visą laiką, kol Viešpats Jėzus buvo tarp mūsų,
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22pradedant Jono krikštu ir baigiant ta diena, kai Jis buvo paimtas iš mūsų aukštyn, reikia kartu su mumis tapti Jo prisikėlimo liudytoju”.
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
23Ir jie išskyrė du: Juozapą, vadinamą Barsabu, pravarde Justas, ir Motiejų.
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24Po to meldėsi, sakydami: “Tu, Viešpatie, kuris pažįsti visų širdis, parodyk, kurį iš šių dviejų pasirenki,
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25kad gautų dalį šioje tarnystėje ir apaštalystėje, nuo kurios nuklydo Judas, nueidamas į savąją vietą”.
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26Tada metė burtus, ir burtas krito Motiejui, ir jis buvo priskaičiuotas prie vienuolikos apaštalų.
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.