1Kiek vėliau buvo žydų šventė, ir Jėzus nukeliavo į Jeruzalę.
1Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu.
2Jeruzalėje, prie Avių vartų, yra maudyklė, žydiškai vadinama Betezda, turinti penkias stogines.
2Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao.
3Jose gulėdavo daugybė ligonių aklų, luošų, paralyžiuotų, kurie laukė vandens sujudant.
3Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: vipofu, viwete na waliopooza. Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe,
4Mat kartkartėmis maudyklėn nusileisdavo angelas ir sujudindavo vandenį. Kas, vandeniui pajudėjus, pirmas įlipdavo į tvenkinį, pagydavo, kad ir kokia liga sirgdavo.
4maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.
5Ten buvo vienas žmogus, išsirgęs trisdešimt aštuonerius metus.
5Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane.
6Pamatęs jį gulintį ir sužinojęs jį labai seniai sergant, Jėzus paklausė: “Ar nori pasveikti?”
6Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo, akatambua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, "Je, wataka kupona?"
7Ligonis Jam atsakė: “Viešpatie, aš neturiu žmogaus, kuris, vandeniui sujudėjus, mane įkeltų į tvenkinį. O kol pats einu, kitas įlipa greičiau už mane”.
7Naye akajibu, "Mheshimiwa, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia."
8Jėzus jam tarė: “Kelkis, imk savo gultą ir vaikščiok!”
8Yesu akamwambia, "Inuka, chukua mkeka wako utembee."
9Žmogus bematant išgijo, pasiėmė gultą ir pradėjo vaikščioti. O toji diena buvo sabatas.
9Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.
10Todėl žydai sakė išgydytajam: “Šiandien sabatas, tau negalima nešti gulto”.
10Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, "Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako."
11Jis jiems atsakė: “Tas, kuris mane išgydė, man liepė: ‘Imk savo gultą ir vaikščiok!’ ”
11Lakini yeye akawaambia, "Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: Chukua mkeka wako, tembea."
12Jie klausinėjo: “O kas Tas žmogus, kuris tau liepė: ‘Imk savo gultą ir vaikščiok’?”
12Nao wakamwuliza, "Huyo mtu aliyekwambia: Chukua mkeka wako, tembea, ni nani?"
13Išgydytasis nežinojo, kas Jis, kadangi Jėzus pasitraukė, miniai susirinkus toje vietoje.
13Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu.
14Vėliau Jėzus jį sutiko šventykloje ir tarė: “Štai tu esi pasveikęs. Daugiau nebenusidėk, kad neatsitiktų tau kas blogesnio!”
14Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa Hekaluni, akamwambia, "Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi."
15Žmogus nuėjo ir pranešė žydams, kad jį išgydė Jėzus.
15Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.
16Žydai dėl to persekiojo Jėzų ir norėjo Jį nužudyti, kad Jis taip darė per sabatą.
16Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
17O Jėzus jiems atsakė: “Mano Tėvas darbuojasi lig šiolei, ir Aš darbuojuosi”.
17Basi, Yesu akawaambia, "Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi."
18Dėl to žydai dar labiau ieškojo progos Jį nužudyti, nes Jis ne tik laužė sabatą, bet ir vadino Dievą savo Tėvu, lygindamas save su Dievu.
18Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumwua Yesu: si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
19Jėzus jiems atsakė: “Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: Sūnus nieko negali daryti iš savęs, o vien tai, ką mato darant Tėvą; nes ką Jisai daro, lygiai daro ir Sūnus.
19Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
20Nes Tėvas myli Sūnų ir rodo Jam visa, ką pats daro. Ir Jam parodys dalykų, dar didesnių už šituos, kad jūs stebėsitės.
20Baba ampenda Mwana, na humwonyesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonyesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
21Kaip Tėvas prikelia numirusius ir juos atgaivina, taip ir Sūnus grąžina gyvybę, kam nori.
21Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uzima wale anaopenda.
22Ir Tėvas nieko neteisia, bet visą teismą pavedė Sūnui,
22Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,
23kad visi gerbtų Sūnų, kaip gerbia Tėvą. Kas negerbia Sūnaus, tas negerbia Jį siuntusio Tėvo.
23ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.
24Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: kas mano žodžių klauso ir mane atsiuntusį tiki, tas turi amžinąjį gyvenimą ir nepateks į teismą, nes iš mirties yra perėjęs į gyvenimą.
24"Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.
25Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: ateina valanda,ir dabar jau yra, kada mirusieji išgirs Dievo Sūnaus balsą, ir kurie išgirs, tie atgis.
25Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi.
26Nes kaip Tėvas turi gyvybę pats savyje, taip davė ir Sūnui turėti gyvybę pačiam savyje,
26Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanawe kuwa asili ya uhai.
27ir taip pat suteikė Jam valdžią teisti, nes JisŽmogaus Sūnus.
27Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu.
28Nesistebėkite tuo, nes ateina valanda, kai visi, esantys kapuose, išgirs Jo balsą.
28Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake,
29Ir tie, kurie darė gera, išeis gyvenimo prisikėlimui, o kurie darė blogateismo prisikėlimui.
29nao watafufuka: wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.
30Iš savęs Aš nieko negaliu daryti. Aš teisiu, kaip girdžiu, ir mano teismas teisingas, nes Aš ieškau ne savo valios, bet valios Tėvo, kuris mane siuntė”.
30"Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.
31“Jei Aš pats apie save liudiju, mano liudijimas nėra tikras.
31Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli.
32Bet apie mane liudija kitas, ir Aš žinau, kad Jo liudijimas, kuriuo Jis liudija apie mane, yra tikras.
32Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli.
33Jūs buvote nusiuntę pas Joną, ir jis paliudijo tiesą.
33Ninyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli.
34Aš neieškau žmogaus liudijimo, bet šitai kalbu tam, kad būtumėte išgelbėti.
34Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.
35Jonas buvo degantis ir šviečiantis žiburys, tačiau jūs panorėjote tik valandėlę jo šviesa pasidžiaugti.
35Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo.
36O Aš turiu aukštesnį liudijimą negu Jono: tie darbai, kuriuos man skyrė nuveikti Tėvas,patys darbai, kuriuos Aš darau,liudija apie mane, kad mane siuntė Tėvas.
36Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.
37Ir mane pasiuntęs Tėvas pats paliudijo apie mane. Bet jūs niekad nesate girdėję Jo balso, nei regėję Jo pavidalo,
37Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake,
38ir neturite Jo žodžio, jumyse pasiliekančio, nes netikite Tuo, kurį Jis siuntė.
38na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.
39Jūs tyrinėjate Raštus, nes manote juose turį amžinąjį gyvenimą. O Raštai liudija apie mane,
39Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia!
40bet jūs nenorite ateiti pas mane, kad turėtumėte gyvenimą”.
40Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
41“Šlovės iš žmonių Aš nepriimu.
41"Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
42Aš žinau, kad neturite savyje Dievo meilės.
42Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
43Aš atėjau savo Tėvo vardu, o jūs manęs nepriimate. Jei kitas ateitų savo vardu, tą jūs priimtumėte.
43Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea.
44Kaipgi jūs galite tikėti, jeigu vienas iš kito priimate šlovę, o tos šlovės, kuri iš vieno Dievo ateina, neieškote?
44Mwawezaje kuamini, hali ninyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu ninyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?
45Nemanykite, kad Aš jus kaltinsiu Tėvui! Jūsų kaltintojas yra Mozė, į kurį esate savo viltis sudėję.
45Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye ninyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.
46Jeigu jūs tikėtumėte Moze, tai tikėtumėte ir manimi, nes jis rašė apie mane.
46Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia; maana Mose aliandika juu yangu.
47Bet jeigu jūs netikite jo raštais, kaipgi patikėsite mano žodžiais?!”
47Lakini hamuyaamini yale aliyoandika, mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?"