Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

12

1Tuo tarpu, kai susirinko nesuskaičiuojama minia, kad net vieni kitus trypė, Jėzus pradėjo kalbėti pirmiausia savo mokiniams: “Saugokitės fariziejų raugo, tai yra veidmainystės!
1Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, "Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2Nėra nieko uždengto, kas nebus atidengta, ir nieko paslėpto, kas nepasidarys žinoma.
2Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3Todėl ką kalbėjote tamsoje, skambės šviesoje, ir ką šnibždėjote į ausį kambariuose, bus skelbiama nuo stogų.
3Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4Sakau jums, savo draugams: nebijokite tų, kurie žudo kūną ir paskui nebegali daugiau nieko padaryti.
4"Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5Aš parodysiu jums, ko turite bijoti: bijokite to, kuris nužudęs, turi galią įmesti į pragarą. Taip, sakau jums, šito bijokite!
5Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo.
6Argi ne penki žvirbliai parduodami už du skatikus? Tačiau nė vienas iš jų nėra Dievo pamirštas.
6Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7O jūsų net visi galvos plaukai suskaičiuoti. Tad nebijokite! Jūs vertesni už daugybę žvirblių.
7Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8Aš jums sakau: kas išpažins mane žmonių akivaizdoje, tą Žmogaus Sūnus išpažins Dievo angelų akivaizdoje.
8"Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9O kas manęs išsigins žmonių akivaizdoje, to bus išsiginta Dievo angelų akivaizdoje.
9Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10Kas tars žodį prieš Žmogaus Sūnų, tam bus atleista, o kas piktžodžiaus Šventajai Dvasiai, tam nebus atleista.
10"Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11Kai jie ves jus į sinagogas, pas valdininkus ar vyresnybes, nesirūpinkite, kaip ar ką atsakysite ir ką kalbėsite,
11"Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12nes Šventoji Dvasia tą pačią valandą pamokys jus, ką kalbėti”.
12Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema."
13Vienas iš minios Jam tarė: “Mokytojau, liepk mano broliui, kad pasidalytų su manimi palikimą”.
13Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, "Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba."
14Jis atsakė: “Žmogau, kas gi mane skyrė jūsų teisėju ar dalytoju?”
14Yesu akamjibu, "Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?"
15Jis pasakė jiems: “Žiūrėkite, saugokitės godumo, nes žmogaus gyvybė nepriklauso nuo jo turto gausos”.
15Basi, akawaambia wote, "Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo."
16Jis pasakė jiems palyginimą: “Vieno turtingo žmogaus laukai davė gausų derlių.
16Kisha akawaambia mfano: "Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17Jis ėmė sau vienas svarstyti: ‘Ką man dabar daryti? Neturiu kur sukrauti derliaus’.
17Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18Pagaliau jis tarė: ‘Štai ką padarysiu: nugriausiu savo klojimus, statysiuos didesnius ir į juos sugabensiu visus javus ir visas gėrybes.
18Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19Tuomet sakysiu savo sielai: ‘Siela, tu turi daug gėrybių, sukrautų ilgiems metams. Ilsėkis, valgyk, gerk ir linksminkis!’
19Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20O Dievas jam tarė: ‘Kvaily, dar šiąnakt bus pareikalauta tavo sielos. Kam gi atiteks, ką susikrovei?’
20Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?"
21Taip yra tam, kuris krauna turtus sau, bet nesirūpina tapti turtingas pas Dievą”.
21Yesu akamaliza kwa kusema "Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu."
22Tada Jėzus kalbėjo savo mokiniams: “Todėl sakau jums: nesirūpinkite savo gyvybe, ką valgysite, nė kūnu, ką vilkėsite.
22Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23Gyvybė svarbesnė už maistą, o kūnas už drabužį.
23Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24Įsižiūrėkite į varnus. Jie nei sėja, nei pjauna, neturi nei sandėlių, nei kluonų, ir Dievas juos maitina. Jūs nepalyginamai vertesni už paukščius!
24Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25Kas gi iš jūsų galėtų savo rūpesčiu bent per sprindį pridėti sau ūgio?
25Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26Jei tad jūs nesugebate padaryti net mažmožio, tai kam rūpinatės kitais dalykais?
26Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27Įsižiūrėkite, kaip auga lelijos. Jos nesidarbuoja ir neaudžia, bet sakau jums: nė Saliamonas visoje savo šlovėje nebuvo taip pasipuošęs kaip kiekviena iš jų.
27Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28Jeigu Dievas taip aprengia laukų žolę, šiandien žaliuojančią, o rytoj metamą į krosnį, tai dar labiau pasirūpins jumis, mažatikiai!
28Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29Ir neklausinėkite, ką valgysite ar gersite, ir nesirūpinkite!
29"Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30Visų tų dalykų ieško šio pasaulio pagonys. O jūsų Tėvas žino, kad viso to jums reikia.
30Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31Verčiau ieškokite Jo karalystės, o visa tai bus jums pridėta.
31Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32Nebijok, mažoji kaimene: jūsų Tėvas panorėjo duoti jums karalystę!”
32"Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33“Parduokite savo turtą ir aukokite gailestingumo aukas. Įsitaisykite sau piniginių, kurios nesusidėvi, kraukite nenykstantį turtą danguje, kur joks vagis neprieina ir kandys nesuėda.
33Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34Nes kur jūsų turtas, ten ir jūsų širdis”.
34Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35“Tebūna jūsų strėnos sujuostos ir žiburiai uždegti,
35"Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36ir būkite panašūs į žmones, kurie laukia savo šeimininko, grįžtančio iš vestuvių, kad kai tik jis parvyks ir pasibels, tuojau atidarytų.
36muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37Palaiminti tie tarnai, kuriuos sugrįžęs šeimininkas ras budinčius. Iš tiesų sakau jums: jis susijuos, susodins juos prie stalo ir priėjęs patarnaus jiems.
37Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38Jeigu jis grįžtų antrosios ar trečiosios nakties sargybos metu ir rastų juos budinčius, palaiminti tie tarnai!
38Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39Įsidėmėkite: jei šeimininkas žinotų, kurią valandą ateis vagis, budėtų ir neleistų jam įsilaužti į savo namus.
39Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40Todėl ir jūs būkite pasirengę, nes Žmogaus Sūnus ateis tą valandą, kurią nesitikėsite”.
40Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
41Tada Petras paklausė: “Viešpatie, ar šį palyginimą sakai tik mums, ar visiems?”
41Petro akamwambia, "Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?"
42Viešpats atsakė: “Kas yra tas ištikimas ir sumanus ūkvedys, kurį šeimininkas paskirs vadovauti šeimynai ir deramu laiku duoti jiems skirtą maisto dalį?
42Bwana akajibu, "Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43Palaimintas tarnas, kurį sugrįžęs šeimininkas ras taip darantį.
43Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44Sakau jums tiesą: jis paskirs jį valdyti visų savo turtų.
44Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45Bet jeigu anas tarnas tartų savo širdyje: ‘Mano šeimininkas neskuba grįžti’, ir imtų mušti tarnus bei tarnaites, valgyti, gerti ir girtuokliauti,
45Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46tai to tarno šeimininkas sugrįš tą dieną, kai jis nelaukia, ir tą valandą, kurią jis nesitiki. Jis perkirs jį pusiau ir paskirs jam dalį su neištikimaisiais.
46bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47Tarnas, kuris žino savo šeimininko valią, bet nėra pasiruošęs ir pagal jo valią nedaro, bus smarkiai nuplaktas.
47Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48O kuris nežino ir baustinai elgiasi, bus mažai plakamas. Iš kiekvieno, kuriam daug duota, bus daug pareikalauta, ir kam daug patikėta, iš to bus daug ir išieškota”.
48Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49“Aš atėjau uždegti žemėje ugnies ir taip noriu, kad ji jau liepsnotų!
49"Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50Bet Aš turiu būti pakrikštytas krikštu ir kaip esu slegiamas, kol tai išsipildys!”
50Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51“Gal manote, kad atėjau atnešti žemėn ramybės? Ne, sakau jums, ne ramybės, o nesantaikos.
51Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52Nuo dabar penki vienuose namuose bus pasidaliję: trys prieš du ir du prieš tris.
52Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53Tėvas stos prieš sūnų, o sūnus prieš tėvą, motina prieš dukterį, o duktė prieš motiną; anyta prieš marčią, ir marti prieš anytą”.
53Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake."
54Jėzus pasakė ir minioms: “Matydami debesį, kylantį vakaruose, tuoj pat sakote: ‘Ateina lietus’, ir taip atsitinka.
54Yesu akayaambia tena makundi ya watu, "Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55Pučiant pietų vėjui, tvirtinate: ‘Bus karšta’, ir taip būna.
55Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56Veidmainiai! Jūs mokate atpažinti žemės ir dangaus veidą, tai kodėl gi neatpažįstate šio laiko?
56Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57Kodėl patys nenusprendžiate, kas teisu?
57"Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58Kai eini su kaltintoju pas valdininką, pasistenk dar kelyje su juo susitarti, kad jis tavęs nenusitemptų pas teisėją, teisėjas neatiduotų teismo vykdytojui, o teismo vykdytojas neįmestų tavęs į kalėjimą.
58Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59Sakau tau: iš ten neišeisi, kol neatsiteisi ligi paskutinio skatiko”.
59Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho."