1Tuo pačiu metu atėjo keli žmonės ir papasakojo Jam apie galilėjiečius, kurių kraują Pilotas sumaišė su jų aukomis.
1Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
2Jėzus, atsakydamas jiems, tarė: “Ar manote, kad tie galilėjiečiai buvo didesni nusidėjėliai už visus kitus galilėjiečius ir todėl taip nukentėjo?
2Naye Yesu akawaambia, "Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
3Ne, sakau jums! Bet jei neatgailausite, visi taip pat pražūsite.
3Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
4Arba anie aštuoniolika, kuriuos užgriuvo bokštas prie Siloamo ir užmušė; jūs manote, kad jie buvo kaltesni už visus kitus Jeruzalės gyventojus?
4Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
5Ne, sakau jums, bet jei neatgailausite, visi taip pat pražūsite”.
5Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao."
6Jis pasakė palyginimą: “Žmogus turėjo savo vynuogyne pasisodinęs figmedį. Kartą jis atėjo pažiūrėti jo vaisių, bet nerado.
6Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: "Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
7Ir tarė sodininkui: ‘Jau treji metai, kai ateinu ieškoti šio figmedžio vaisių ir vis nerandu. Nukirsk jį, kam dar žemę alina!’
7Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
8Anas jam atsakė: ‘Šeimininke, palik dar jį šiais metais. Aš jį apkasiu ir patręšiu.
8Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9Jei jis duos vaisių, gerai. O jei ne, tai iškirsk jį!’ ”
9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata."
10Sabato dieną Jėzus mokė vienoje sinagogoje.
10Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11Čia buvo moteris, aštuoniolika metų turinti ligos dvasią. Ji buvo sutraukta ir visiškai negalėjo išsitiesti.
11Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12Jėzus, pamatęs ją, pasišaukė ir tarė: “Moterie, esi išvaduota iš savo ligos!”
12Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, "Mama, umeponywa ugonjwa wako."
13Jis uždėjo ant jos rankas, toji bematant atsitiesė ir ėmė garbinti Dievą.
13Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
14Tada sinagogos vyresnysis, supykęs, kad Jėzus išgydė ją sabato dieną, pasakė miniai: “Dirbamos yra šešios dienos. Ateikite jomis ir gydykitės, o ne per sabatą!”
14Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, "Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato."
15Viešpats jam atsakė: “Veidmainy! Argi kas iš jūsų neatriša per sabatą nuo ėdžių savo jaučio ar asilo ir nenuveda pagirdyti?
15Hapo Bwana akamjibu, "Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
16Argi šios Abraomo dukters, kurią šėtonas laikė surišęs jau aštuoniolika metų, nereikėjo išvaduoti iš pančių sabato dieną?”
16Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?"
17Kai Jis tai kalbėjo, visi Jo priešininkai liko sugėdinti, o minia džiaugėsi visais šlovingais Jo atliktais darbais.
17Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
18Jis tarė: “Į ką panaši Dievo karalystė, ir su kuo ją palyginsiu?
18Yesu akauliza: "Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
19Ji panaši į garstyčios grūdą, kurį ėmė žmogus ir pasėjo savo darže. Ji išaugo į aukštą medelį ir padangių paukščiai susisuko lizdus jo šakose”.
19NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake."
20Jis vėl tarė: “Su kuo palyginsiu Dievo karalystę?
20Tena akauliza: "Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
21Ji panaši į raugą, kurį ėmusi moteris įmaišė į tris saikus miltų, ir nuo jo viskas įrūgo”.
21Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote."
22Jėzus ėjo mokydamas per miestelius bei kaimus ir keliavo į Jeruzalę.
22Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
23Kažkas paklausė Jį: “Viešpatie, ar maža bus išgelbėtųjų?” Jis atsakė jiems:
23Mtu mmoja akamwuliza, "Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?"
24“Stenkitės įeiti pro siaurus vartus. Sakau jums, daugelis bandys įeiti, bet neįstengs.
24Yesu akawaambia, "Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
25Kai namų Šeimininkas atsikels ir užrakins duris, jūs, stovėdami lauke, pradėsite belsti į duris ir prašyti: ‘Viešpatie, Viešpatie, atidaryk mums!’ O Jis atsakys: ‘Aš nežinau, iš kur jūs’.
25"Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
26Tada imsite sakyti: ‘Mes valgėme ir gėrėme Tavo akivaizdoje, Tu mokei mūsų gatvėse’.
26Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
27O Jis tars: ‘Sakau jums, Aš nežinau, iš kur jūs. Eikite šalin nuo manęs, visi piktadariai!’
27Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
28Ten bus verksmo ir dantų griežimo, kai pamatysite Abraomą, Izaoką, Jokūbą ir visus pranašus Dievo karalystėje, o patys būsite išmesti laukan.
28Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
29Ir ateis iš rytų ir vakarų, iš šiaurės ir pietų ir sėsis prie stalo Dievo karalystėje.
29Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
30Ir štai yra paskutinių, kurie bus pirmi, ir pirmų, kurie bus paskutiniai”.
30Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho."
31Tą pačią dieną atėjo keli fariziejai ir pasakė Jėzui: “Eik iš čia, pasišalink, nes Erodas nori Tave nužudyti”.
31Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, "Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua."
32Jis jiems atsakė: “Eikite ir pasakykite tam lapei: ‘Štai Aš išvarinėju demonus ir gydau šiandien, tai darysiu ir rytoj, o trečią dieną būsiu viską atlikęs.
32Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
33Bet šiandien ir rytoj, ir poryt turiu keliauti, nes negali taip būti, kad pranašas žūtų ne Jeruzalėje’ ”.
33Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
34“Jeruzale, Jeruzale! Tu žudai pranašus ir užmėtai akmenimis tuos, kurie pas tave siųsti. Kiek kartų norėjau surinkti tavo vaikus kaip višta savo viščiukus po sparnais, o tu nenorėjai!
34"Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
35Štai jūsų namai paliekami jums tušti. Iš tiesų sakau jums: jūs manęs nebematysite, kol ateis laikas, kada tarsite: ‘Palaimintas Tas, kuris ateina Viešpaties vardu!’ ”
35Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."