Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

18

1Jėzus pasakė jiems palyginimą, kaip reikia visuomet melstis ir neprarasti ryžto,
1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2tardamas: “Viename mieste buvo teisėjas, kuris nebijojo Dievo ir nesidrovėjo žmonių.
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3Tame pačiame mieste gyveno našlė, kuri vis eidavo pas jį ir prašydavo: ‘Apgink mane nuo mano priešininko!’
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4Jis kurį laiką nenorėjo, bet po to tarė sau: ‘Nors aš Dievo nebijau nei žmonių nesidroviu,
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5vis dėlto, kai šita našlė neduoda man ramybės, apginsiu jos teises, kad ji, vienąkart atėjusi, man akių neišdraskytų’ ”.
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
6Ir Viešpats tarė: “Įsidėmėkite, ką pasakė tas neteisusis teisėjas.
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7Tad nejaugi Dievas neapgins savo išrinktųjų, kurie Jo šaukiasi dieną ir naktį, ir dels jiems padėti?
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8Sakau jums: Jis apgins jų teises labai greitai. Bet ar atėjęs Žmogaus Sūnus beras žemėje tikėjimą?”
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
9Tiems, kurie pasitikėjo savo teisumu, o kitus niekino, Jėzus pasakė palyginimą:
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10“Du žmonės atėjo į šventyklą melstis: vienas­fariziejus, o kitas­muitininkas.
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11Fariziejus stovėdamas taip sau vienas meldėsi: ‘Dėkoju Tau, Dieve, kad nesu toks, kaip kiti žmonės­plėšikai, sukčiai, svetimautojai­arba kaip šis va muitininkas.
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12Aš pasninkauju du kartus per savaitę, duodu dešimtinę iš visko, ką įsigyju’.
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13O muitininkas, atokiai stovėdamas, nedrįso nė akių pakelti į dangų, tik, mušdamasis į krūtinę, maldavo: ‘Dieve, būk gailestingas man, nusidėjėliui!’
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14Sakau jums: šitas nuėjo į namus išteisintas, o ne anas. Kiekvienas, kuris save aukština, bus pažemintas, o kuris save žemina, bus išaukštintas”.
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
15Jėzui atnešdavo kūdikių, kad Jis juos paliestų. Mokiniai, tai matydami, draudė.
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16Bet Jėzus, pasišaukęs vaikučius, tarė: “Leiskite mažutėliams ateiti pas mane ir netrukdykite jiems, nes tokių yra Dievo karalystė.
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17Iš tiesų sakau jums: kas nepriims Dievo karalystės kaip kūdikis, niekaip neįeis į ją!”
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
18Vienas valdininkas Jį paklausė: “Gerasis Mokytojau, ką turiu daryti, kad paveldėčiau amžinąjį gyvenimą?”
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
19Jėzus jam atsakė: “Kodėl vadini mane geru? Nė vieno nėra gero, tik vienas Dievas.
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20Įsakymus žinai: ‘Nesvetimauk, nežudyk, nevok, melagingai neliudyk, gerbk savo tėvą ir motiną’ ”.
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
21Tas atsakė: “Viso šito laikausi nuo savo jaunystės”.
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
22Tai išgirdęs, Jėzus jam tarė: “Tau trūksta vieno dalyko: parduok visa, ką turi, išdalink vargšams, ir turėsi turtą danguje. Tada ateik ir sek paskui mane!”
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
23Tai išgirdęs, jis nusiminė, nes buvo labai turtingas.
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24Matydamas jį nuliūdusį, Jėzus prabilo: “Kaip sunkiai turintieji turtų įeis į Dievo karalystę!
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25Lengviau kupranugariui išlįsti pro adatos ausį, negu turtingam įeiti į Dievo karalystę!”
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
26Girdėjusieji tai paklausė: “Kas tada gali būti išgelbėtas?”
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
27Jis atsakė: “Kas neįmanoma žmonėms, įmanoma Dievui”.
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
28Tada Petras tarė: “Štai mes viską palikome ir nusekėme paskui Tave”.
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
29Jėzus atsakė jiems: “Iš tiesų sakau jums: nėra nė vieno, kuris paliko namus ar tėvus, ar brolius, ar žmoną, ar vaikus dėl Dievo karalystės
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30ir kuris jau šiuo metu negautų nepalyginamai daugiau, o būsimajame pasaulyje­amžinojo gyvenimo”.
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
31Jėzus pasišaukė dvylika ir tarė: “Štai mes einame į Jeruzalę, ir ten išsipildys visa, kas per pranašus parašyta apie Žmogaus Sūnų.
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32Jis bus atiduotas pagonims, išjuoktas, paniekintas ir apspjaudytas.
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33Tie nuplaks Jį ir nužudys, bet trečią dieną Jis prisikels”.
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
34Tačiau jie nieko nesuprato; tų žodžių prasmė jiems liko paslėpta, ir jie nesuvokė, kas buvo sakoma.
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35Jam artinantis prie Jericho, šalia kelio sėdėjo neregys elgeta.
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36Išgirdęs praeinančią minią, jis paklausė, kas tai būtų.
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
37Jam atsakė, kad praeinąs Jėzus iš Nazareto.
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
38Tada jis ėmė šaukti: “Jėzau, Dovydo Sūnau, pasigailėk manęs!”
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
39Ėję priekyje draudė jį, kad tylėtų, bet tas dar garsiau šaukė: “Dovydo Sūnau, pasigailėk manęs!”
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
40Jėzus sustojo ir liepė jį atvesti. Jam prisiartinus, paklausė jo:
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41“Ko nori, kad tau padaryčiau?”
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
42Šis atsakė: “Viešpatie, kad praregėčiau!” Jėzus tarė: “Regėk! Tavo tikėjimas išgydė tave”.
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
43Tas iškart praregėjo ir nusekė paskui Jį, garbindamas Dievą. Tai matydami, visi žmonės šlovino Dievą.
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.