1Atvykęs Jėzus ėjo per Jerichą.
1Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2Ir štai žmogus, vardu Zachiejus, muitininkų viršininkas ir turtuolis,
2Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3troško pamatyti Jėzų, kas Jis esąs, bet negalėjo per minią, nes buvo žemo ūgio.
3Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4Zachiejus užbėgo priekin ir įlipo į šilkmedį, kad galėtų Jį pamatyti, nes Jis turėjo ten praeiti.
4Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5Kai Jėzus atėjo į tą vietą, pažvelgė aukštyn ir, pamatęs jį, tarė: “Zachiejau, greit lipk žemyn, nes šiandien turiu apsistoti tavo namuose”.
5Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako."
6Šis skubiai nulipo ir su džiaugsmu priėmė Jį.
6Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7Tai matydami, visi murmėjo: “Pas nusidėjėlį užėjo į svečius!”
7Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi."
8O Zachiejus atsistojęs prabilo į Viešpatį: “Štai, Viešpatie, pusę savo turto atiduodu vargšams ir, jei ką nors nuskriaudžiau, grąžinsiu keturgubai”.
8Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
9Jėzus tarė: “Šiandien į šiuos namus atėjo išgelbėjimas, nes ir jis yra Abraomo sūnus.
9Yesu akamwambia, "Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10Juk Žmogaus Sūnus atėjo ieškoti ir gelbėti, kas buvo pražuvę”.
10Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea."
11Jiems klausantis, Jis tęsė ir pasakė palyginimą. Mat Jis buvo netoli Jeruzalės, ir žmonės manė, jog tuojau pat turi pasirodyti Dievo karalystė.
11Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12Tad Jis kalbėjo: “Vienas aukštos kilmės žmogus iškeliavo į tolimą šalį, kad gautų karalystę ir sugrįžtų.
12Hivyo akawaambia, "Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13Pasišaukęs dešimt savo tarnų, padalijo jiems dešimt minų ir tarė: ‘Verskitės, kol sugrįšiu’.
13Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14Piliečiai nekentė jo ir nusiuntė iš paskos pasiuntinius pareikšti: ‘Mes nenorime, kad šitas mums viešpatautų’.
14Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15Gavęs karalystę, jis sugrįžo ir liepė pašaukti tarnus, kuriems buvo davęs pinigų, norėdamas sužinoti, kiek kuris uždirbo.
15"Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16Atėjo pirmasis ir tarė: ‘Valdove, tavo mina pelnė dešimt minų’.
16Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17Jis atsakė: ‘Gerai, stropusis tarne! Kadangi pasirodei ištikimas mažuose dalykuose, tu gauni valdyti dešimtį miestų’.
17Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18Atėjo antrasis ir pareiškė: ‘Valdove, tavo mina pelnė penkias minas’.
18Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19Ir šitam jis pasakė: ‘Tu valdyk penkis miestus’.
19Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20Atėjo dar vienas ir tarė: ‘Valdove, štai tavo mina, kurią laikiau suvyniotą į skepetą.
20"Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21Aš bijojau tavęs, nes esi griežtas žmogus: imi tai, ko nepadėjai, ir pjauni tai, ko nepasėjai’.
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22Jis atsiliepė: ‘Tavo paties žodžiais teisiu tave, netikęs tarne. Tu žinojai, kad aš griežtas žmogus: imu, ko nepadėjau, ir pjaunu, ko nesėjau.
22Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23Tai kodėl neleidai mano pinigų apyvarton, kad sugrįžęs išreikalaučiau su palūkanomis?’
23Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24Šalia stovėjusiems jis tarė: ‘Atimkite iš jo miną ir atiduokite tam, kuris turi dešimt minų’.
24Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25Tie atsakė: ‘Valdove, bet anas jau turi dešimt minų!’
25Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26Jis tarė: ‘Aš sakau jums: kiekvienam, kas turi, bus duota, o iš neturinčio bus atimta net ir tai, ką turi.
26Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27O tuos mano priešus, nenorėjusius, kad jiems viešpataučiau, atveskite čia ir nužudykite mano akyse!’ ”
27Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."
28Tai pasakęs, Jėzus visų priešakyje nukreipė žingsnius į Jeruzalę.
28Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29Prisiartinęs prie Betfagės ir Betanijos, prie vadinamojo Alyvų kalno, Jis pasiuntė du mokinius,
29Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30sakydamas jiems: “Eikite į priešais esantį kaimą ir įėję rasite pririštą asilaitį, kuriuo dar joks žmogus nėra jojęs. Atriškite jį ir atveskite.
30akawaambia: "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31O jeigu kas klaustų: ‘Kodėl jį atrišate?’, atsakykite: ‘Jo reikia Viešpačiui’ ”.
31Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye."
32Pasiųstieji nuėjo ir rado, kaip jiems buvo pasakyta.
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33Atrišant asilaitį, savininkai klausė: “Kodėl atrišate asilaitį?”
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, "Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?"
34Tie atsakė: “Jo reikia Viešpačiui”.
34Nao wakawajibu, "Bwana anamhitaji."
35Jie atvedė asilaitį pas Jėzų, apdengė savo apsiaustais ir užsodino Jėzų ant viršaus.
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36Jam jojant, žmonės tiesė ant kelio savo drabužius.
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37Besiartinant prie Alyvų kalno šlaito, visas mokinių būrys pradėjo džiaugsmingai ir garsiai šlovinti Dievą už visus stebuklus, kuriuos jie buvo regėję.
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38Jie šaukė: “ ‘Palaimintas karalius, kuris ateina Viešpaties vardu!’ Ramybė danguje, šlovė aukštybėse!”
38wakawa wanasema: "Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!"
39Kai kurie fariziejai iš minios Jam sakė: “Mokytojau, sudrausk savo mokinius!”
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, "Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!"
40Jis jiems atsakė: “Sakau jums, jei šie tylėsakmenys šauks!”
40Yesu akawajibu, "Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti."
41Prisiartinęs prie Jeruzalės ir išvydęs miestą, Jėzus verkė dėl jo ir sakė:
41Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42“O kad tu nors šiandien suprastum, kas tau atneša ramybę! Deja, tai paslėpta nuo tavo akių.
42akisema: "Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43Tu sulauksi dienų, kai tavo priešai apjuos tave pylimu, apguls iš visų pusių ir suspaus tave;
43Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44jie parblokš ant žemės tave ir tavo vaikus ir nepaliks tavyje akmens ant akmens, nes tu nepažinai savo aplankymo meto”.
44Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa."
45Įėjęs į šventyklą, Jis pradėjo varyti laukan parduodančius ir perkančius.
45Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46Jis sakė jiems: “Parašyta: ‘Mano namai yra maldos namai’, o jūs pavertėte juos ‘plėšikų lindyne’ ”.
46akisema, "Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
47Ir Jis kasdien mokė šventykloje. O aukštieji kunigai ir Rašto žinovai bei tautos vyresnieji troško Jį pražudyti,
47Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48tačiau neišmanė, ką galėtų padaryti, nes visi žmonės apgulę Jį klausėsi.
48lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.