1Vieną iš tų dienų Jėzui mokant žmones šventykloje ir skelbiant Evangeliją, atėjo aukštųjų kunigų ir Rašto žinovų su vyresniaisiais
1Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2ir klausė Jį: “Pasakyk mums, kokią teisę turi taip daryti? Kas Tau davė šitą valdžią?”
2wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
3Jis jiems tarė: “Aš irgi paklausiu jus vieno dalyko, ir atsakykite man:
3Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
4ar Jono krikštas buvo iš dangaus, ar iš žmonių?”
4mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
5Jie svarstė tarpusavyje: “Jei pasakysimeiš dangaus, Jis mus klaus: ‘Tai kodėl juo netikėjote?’
5Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6O jei sakysimeiš žmonių, visa minia užmėtys mus akmenimis, nes žmonės įsitikinę, kad Jonas buvo pranašas”.
6Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
7Ir jie atsakė, kad nežino iš kur.
7Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
8Tada Jėzus jiems tarė: “Tai ir Aš jums nesakysiu, kokia valdžia tai darau”.
8Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
9Jis pradėjo pasakoti žmonėms tokį palyginimą: “Vienas žmogus pasodino vynuogyną, išnuomojo jį vynininkams ir ilgesniam laikui iškeliavo svetur.
9Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10Atėjus metui, jis nusiuntė pas vynininkus tarną, kad tie jam duotų vynuogyno derliaus dalį. Tačiau vynininkai sumušė jį ir paleido tuščiomis.
10Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11Jis vėl nusiuntė kitą tarną, bet ir tą jie sumušė, išjuokė ir paleido jį tuščiomis.
11Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12Tuomet jis pasiuntė dar trečią, bet jie ir šitą sužeidę išvarė.
12Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13Tada vynuogyno šeimininkas tarė: ‘Ką man daryti? Pasiųsiu savo mylimąjį sūnų, gal pamatę jie gerbs jį?’
13Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14Bet, išvydę sūnų, vynininkai ėmė tartis tarpusavyje: ‘Tai paveldėtojas. Užmuškime jį, kad mums atitektų palikimas’.
14Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15Jie išmetė jį iš vynuogyno ir nužudė. Ką gi su jais darys vynuogyno savininkas?
15Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16Jis ateis ir išžudys tuos vynininkus, o vynuogyną atiduos kitiems”. Tai girdėjusieji tarė: “Tenebūna šitaip!”
16Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
17Bet Jėzus, pažvelgęs į juos, paklausė: “O ką reiškia Rašto posakis: ‘Akmuo, kurį statytojai atmetė, tapo kertiniu akmeniu?’
17Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18Kas tiktai kris ant šito akmens, suduš, o ant ko tas akmuo užgrius, tą sutriuškins”.
18Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
19Aukštieji kunigai ir Rašto žinovai norėjo dar tą pačią valandą Jį suimti, bet bijojo žmonių. Mat jie suprato, kad šis palyginimas buvo jiems taikomas.
19Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20Jie patys atidžiai Jėzų stebėjo ir siuntinėjo šnipus, apsimetančius teisuoliais, kad, nutvėrę kokį Jo žodį, galėtų Jį atiduoti valdytojui nuteisti ir nubausti.
20Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21Taigi jie klausė Jį: “Mokytojau, mes žinome, kad Tu kalbi ir mokai teisingai. Tu neatsižvelgi į asmenis, bet mokai Dievo kelio, kaip reikalauja tiesa.
21Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22Ar reikia mums mokėti ciesoriui mokesčius, ar ne?”
22Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
23Suprasdamas jų klastą, Jis tarė jiems: “Kodėl spendžiate man pinkles?
23Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24Parodykite man denarą. Kieno atvaizdas ir įrašas jame?” Jie atsakė: “Ciesoriaus”.
24"Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
25Tada Jis jiems tarė: “Kas ciesoriaus, atiduokite ciesoriui, o kas DievoDievui”.
25Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
26Taip jie nesugebėjo žmonių akivaizdoje sugauti Jo kalboje. Stebėdamiesi Jo atsakymu, jie nutilo.
26Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27Pas Jį atėjo sadukiejų, kurie neigia mirusiųjų prisikėlimą, ir paklausė:
27Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28“Mokytojau, Mozė mums parašė: jei kieno brolis, turėdamas žmoną, mirtų bevaikis, tada jo brolis tegul veda jo žmoną ir pažadina savo broliui palikuonių.
28"Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29Taigi buvo septyni broliai. Pirmasis vedė žmoną ir mirė bevaikis.
29Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30Ją vedė antrasis ir taip pat mirė bevaikis.
30Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31Paskui ją vedė trečiasis ir paeiliui visi septyni, ir jie mirė, nepalikdami vaikų.
31na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
32Po jų visų numirė ir ta moteris.
32Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33Kurio gi žmona ji bus prisikėlime? Juk ji buvo visų septynių žmona!”
33Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
34Jėzus jiems atsakė: “Šio pasaulio vaikai veda ir teka,
34Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
35o kurie pasirodys verti pasiekti aną pasaulį ir mirusiųjų prisikėlimą, tie neves ir netekės.
35lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
36Jie taip pat nebegalės ir mirti, nes, būdami prisikėlimo vaikai, bus lygūs angelams ir bus Dievo vaikai.
36Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37O kad mirusieji prisikels, nurodė ir Mozė pasakojime apie krūmą, kur jis Viešpatį vadina ‘Abraomo Dievu, Izaoko Dievu ir Jokūbo Dievu’.
37Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38Taigi Dievas nėra mirusiųjų Dievas, bet gyvųjų, nes visi Jam gyvena”.
38Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
39Tada kai kurie Rašto žinovai atsiliepė: “Mokytojau, Tu gerai pasakei!”
39Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
40Ir daugiau jie nedrįso nieko Jo klausti.
40Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41Jis paklausė jų: “Kodėl sakoma, jog Kristus esąs Dovydo Sūnus?
41Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42Juk pats Dovydas Psalmių knygoje sako: ‘Viešpats tarė mano Viešpačiui: sėskis mano dešinėje,
42Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43kol patiesiu Tavo priešus tarsi pakojį po Tavo kojų’.
43mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44Taigi Dovydas vadina Jį Viešpačiu,kaip tada Jis gali būti jo Sūnus?”
44Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?"
45Visiems žmonėms girdint, Jėzus tarė savo mokiniams:
45Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46“Saugokitės Rašto žinovų, kurie mėgsta vaikščioti ilgais drabužiais, būti sveikinami aikštėse, užimti pirmuosius krėslus sinagogose bei garbės vietas pokyliuose.
46"Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47Jie suryja našlių namus ir dedasi kalbą ilgas maldas. Jie gaus dar didesnį pasmerkimą”.
47Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"