Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

21

1Pažvelgęs Jis pamatė turtinguosius, dedančius savo dovanas į iždinę.
1Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
2Jis pamatė ir vieną beturtę našlę, kuri įmetė du smulkius pinigėlius.
2akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
3Ir Jis tarė: “Iš tiesų sakau jums, ši beturtė našlė įmetė daugiau už visus.
3Basi, akasema, "Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
4Nes anie visi iš savo pertekliaus aukojo dovanų Dievui, o ji iš savo nepritekliaus įmetė viską, ką turėjo pragyvenimui”.
4Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."
5Kai kuriems kalbant apie šventyklą, kad ji išpuošta gražiais akmenimis bei dovanomis, Jėzus prabilo:
5Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
6“Ateis dienos, kai iš to, ką matote, neliks akmens ant akmens, viskas bus išgriauta”.
6"Haya yote mnayoyaona--zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
7Jie paklausė: “Mokytojau, kada tai įvyks? Ir koks bus ženklas, kai visa tai pradės pildytis?”
7Basi, wakamwuliza, "Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?"
8Jis pasakė: “Žiūrėkite, kad nebūtumėte suklaidinti, nes daugelis ateis mano vardu, ir sakys: ‘Tai Aš!’ ir: ‘Atėjo metas!’ Neikite paskui juos!
8Yesu akawajibu, "Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
9O kai išgirsite apie karus ir maištus, nenusigąskite, nes visa tai turi pirmiau įvykti, bet dar negreit galas”.
9Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado."
10Ir dar jiems sakė: “Tauta sukils prieš tautą ir karalystė prieš karalystę.
10Halafu akaendelea kusema: "Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
11Įvairiose vietose bus didelių žemės drebėjimų, badmečių, marų, bus baisių įvykių ir didelių ženklų iš dangaus.
11Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
12Bet prieš tai jie pakels prieš jus rankas ir dėl mano vardo jus persekios, tempdami į sinagogas ir kalėjimus, ves pas karalius ir valdytojus.
12Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
13Tai bus jums proga liudyti.
13Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
14Taigi įsidėkite sau į širdis iš anksto negalvoti, kaip ginsitės,
14Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
15nes Aš jums duosiu tokios iškalbos ir išminties, kad nė vienas jūsų priešininkas negalės nei atsispirti, nei prieštarauti.
15kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
16Jus išdavinės tėvai, broliai, giminės ir draugai; kai kuriuos iš jūsų jie žudys.
16Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
17Būsite visų nekenčiami dėl mano vardo.
17Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
18Tačiau nė plaukas nuo jūsų galvos nenukris.
18Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
19Savo ištverme išlaikykite savo sielas”.
19Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
20“Kai pamatysite Jeruzalę supamą kariuomenės, žinokite, jog prisiartino jos sunaikinimas.
20"Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
21Tada, kas bus Judėjoje, tebėga į kalnus, kas mieste­teišeina iš jo, kas apylinkėse­tenegrįžta.
21Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
22Nes tai bus bausmės dienos, kad išsipildytų visa, kas parašyta.
22Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
23Vargas nėščioms ir žindančioms tomis dienomis! Nes baisi nelaimė ir rūstybė ištiks šitą tautą.
23Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
24Žmonės kris nuo kalavijo ašmenų ir bus išvaryti nelaisvėn į visas tautas, o Jeruzalę mindžios pagonys, kol baigsis pagonių laikai”.
24Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
25“Bus ženklų saulėje, mėnulyje ir žvaigždėse, o žemėje blaškysis sielvarto slegiamos tautos, jūrai baisiai šniokščiant ir šėlstant.
25"Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
26Žmonės sustings iš baimės, laukdami to, kas turės ištikti pasaulį, nes dangaus galybės bus sudrebintos.
26Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27Tada jie išvys Žmogaus Sūnų, ateinantį debesyje su jėga ir didžia šlove.
27Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
28Kai tai prasidės, atsitieskite ir pakelkite galvas, nes artėja jūsų atpirkimas”.
28Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
29Ir Jis jiems pasakė palyginimą: “Stebėkite figmedį bei visus kitus medžius.
29Kisha akawaambia mfano: "Angalieni mtini na miti mingine yote.
30Kai jie ima sprogti, jūs patys matote ir žinote, kad vasara jau arti.
30Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
31Taip pat pamatę visa tai vykstant, žinokite, kad arti yra Dievo karalystė.
31Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
32Iš tiesų sakau jums: ši karta nepraeis, iki visa tai įvyks.
32Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
33Dangus ir žemė praeis, o mano žodžiai nepraeis.
33Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
34Saugokitės, kad jūsų širdys nebūtų apsunkintos nesaikingumo, girtavimo ir gyvenimo rūpesčių, kad toji diena neužkluptų jūsų netikėtai.
34"Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
35It žabangai ji užgrius visus žemės gyventojus.
35Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
36Todėl visą laiką budėkite ir melskitės, kad būtumėt palaikyti vertais išvengti visko, kas įvyks, ir stoti prieš Žmogaus Sūnų”.
36Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu."
37Taip Jėzus dienomis mokydavo šventykloje, o naktis praleisdavo vadinamajame Alyvų kalne.
37Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
38Ir nuo ankstyvo ryto visi žmonės rinkdavosi Jo pasiklausyti šventykloje.
38Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.