Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

22

1Artėjo Neraugintos duonos šventė, vadinama Pascha.
1Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2Aukštieji kunigai ir Rašto žinovai ieškojo būdo nužudyti Jėzų, nes bijojo žmonių.
2Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3O šėtonas įėjo į Judą, vadinamą Iskarijotu, vieną iš dvylikos.
3Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4Tas nuėjęs tarėsi su aukštaisiais kunigais ir sargybos viršininkais, kaip Jį išduoti.
4Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5Šie apsidžiaugė ir sutarė duoti jam pinigų.
5Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6Judas pažadėjo ir ieškojo progos išduoti jiems Jėzų, miniai nematant.
6Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7Atėjo Neraugintos duonos diena, kada reikėjo pjauti Paschos avinėlį.
7Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8Jėzus pasiuntė Petrą ir Joną, liepdamas: “Eikite ir paruoškite mums valgyti Paschą”.
8Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, "Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka."
9Jie paklausė: “Kur nori, kad paruoštume?”
9Nao wakamwuliza, "Unataka tuiandae wapi?"
10Jis atsakė: “Štai jums įeinant į miestą, jus pasitiks žmogus, vandens ąsočiu nešinas. Sekite paskui jį iki tų namų, į kuriuos jis įeis,
10Akawaambia, "Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11ir sakykite namų šeimininkui: ‘Mokytojas liepė paklausti: Kur svečių kambarys, kuriame galėčiau su mokiniais valgyti Paschą?’
11Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12Jis parodys jums didelį apstatytą aukštutinį kambarį. Ten ir paruoškite”.
12Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo."
13Nuėję jie rado viską, kaip Jis sakė, ir paruošė Paschą.
13Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14Atėjus metui, Jis sėdo prie stalo, ir dvylika apaštalų drauge su Juo.
14Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15Ir Jis tarė jiems: “Trokšte troškau valgyti su jumis šią Paschą prieš kentėdamas.
15Akawaambia, "Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16Sakau jums, nuo šiol daugiau jos nebevalgysiu, kol ji išsipildys Dievo karalystėje”.
16Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu."
17Paėmęs taurę, Jis padėkojo ir tarė: “Imkite ir dalykitės.
17Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, "Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18Sakau jums: Aš nebegersiu vynmedžio vaisiaus, kol ateis Dievo karalystė”.
18Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja."
19Ir, paėmęs duoną, Jis padėkojo, laužė ją ir davė jiems, sakydamas: “Tai yra mano kūnas, kuris už jus atiduodamas. Tai darykite mano atminimui”.
19Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, "Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
20Lygiai taip po vakarienės Jis paėmė taurę, sakydamas: “Ši taurė yra Naujoji Sandora mano kraujyje, kuris už jus išliejamas.
20Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, "Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21Bet štai mano išdavėjo ranka yra kartu su manąja ant stalo.
21"Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22Žmogaus Sūnus, tiesa, eina, kaip Jam paskirta, bet vargas tam žmogui, kuris Jį išduoda!”
22Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti."
23Tada jie pradėjo klausinėti vienas kito, kas gi iš jų yra tas, kuris tai padarys.
23Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24Tarp jų taip pat kilo ginčas, kuris iš jų turėtų būti laikomas didžiausiu.
24Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25Bet Jėzus jiems pasakė: “Pagonių karaliai viešpatauja jiems ir tie, kurie juos valdo, vadinami geradariais.
25Yesu akawaambia, "Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26Jūs taip nedarykite. Kas didžiausias tarp jūsų, tebūnie tarsi mažiausias, o vadovaujantis tebūnie kaip tarnas.
26Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27Katras yra didesnis­kuris sėdi už stalo ar kuris jam patarnauja? Argi ne tas, kuris sėdi? O Aš tarp jūsų esu kaip tas, kuris patarnauja.
27Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28Jūs ištvėrėte su manimi mano išbandymuose,
28"Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29todėl Aš jums skiriu valdyti karalystę, kaip ir man yra skyręs Tėvas,
29na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30kad mano karalystėje jūs valgytumėte ir gertumėte už mano stalo ir sėdėtumėte sostuose, teisdami dvylika Izraelio giminių”.
30Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31Ir Viešpats tarė: “Simonai, Simonai! Štai šėtonas prašė persijoti jus tarsi kviečius.
31"Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32Bet Aš meldžiau už tave, kad tavo tikėjimas nepalūžtų, ir tu atsivertęs stiprink savo brolius!”
32Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako."
33Petras atsiliepė: “Viešpatie, aš pasiruošęs kartu su Tavimi eiti ir į kalėjimą, ir į mirtį!”
33Naye Petro akamjibu, "Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa."
34Bet Jėzus atsakė: “Sakau tau, Petrai: dar šiandien, gaidžiui nepragydus, tu tris kartus išsiginsi, kad mane pažįsti”.
34Yesu akamjibu, "Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu."
35Jis paklausė juos: “Ar jums ko nors trūko, kai buvau jus išsiuntęs be piniginės, be krepšio ir be sandalų?” Jie atsakė: “Nieko”.
35Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?" Wakajibu, "La."
36Tada Jis jiems tarė: “Dabar, kas turi piniginę, tepasiima ją, taip pat ir krepšį, o kas neturi kalavijo, teparduoda apsiaustą ir tenusiperka.
36Naye akawaambia, "Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37Sakau jums, manyje privalo išsipildyti, kas parašyta: ‘Jis buvo priskaitytas prie piktadarių’; tai, kas man nustatyta, jau eina į pabaigą”.
37Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake."
38Jie tarė: “Viešpatie, štai čia du kalavijai!” Jis atsakė: “Gana!”
38Nao wakasema, "Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili." Naye akasema, "Basi!"
39Išėjęs iš ten, Jis, kaip buvo pratęs, pasuko į Alyvų kalną. Paskui Jį nuėjo ir mokiniai.
39Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40Atėjus į vietą, Jis tarė jiems: “Melskitės, kad nepakliūtumėte į pagundymą!”
40Alipofika huko akawaambia, "Salini, msije mkaingia katika kishawishi."
41Ir Jis atsitolino nuo jų maždaug per akmens metimą ir atsiklaupęs ėmė melstis:
41Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42“Tėve, jei nori, atimk šitą taurę nuo manęs, tačiau tebūna ne mano, bet Tavo valia!”
42"Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu."
43Jam pasirodė iš dangaus angelas ir Jį sustiprino.
43Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44Vidinės kovos draskomas, Jis dar karščiau meldėsi. Jo prakaitas pasidarė tarsi tiršto kraujo lašai, varvantys žemėn.
44Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45Atsikėlęs po maldos, Jis atėjo pas mokinius ir rado juos iš sielvarto užmigusius.
45Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46Jis tarė jiems: “Kodėl miegate? Kelkitės ir melskitės, kad nepakliūtumėte į pagundymą!”
46Akawaambia, "Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi."
47Jam dar tebekalbant, štai pasirodė minia, o priekyje­vienas iš dvylikos, vadinamas Judu. Jis priėjo prie Jėzaus Jo pabučiuoti.
47Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48Jėzus jam tarė: “Judai, pabučiavimu išduodi Žmogaus Sūnų?”
48Lakini Yesu akamwambia, "Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?"
49Esantieji su Juo, matydami, kas bus, paklausė: “Viešpatie, gal mums kirsti kalaviju?”
49Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, "Bwana, tutumie panga zetu?"
50Vienas iš jų smogė vyriausiojo kunigo tarnui ir nukirto jam dešinę ausį.
50Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51Bet Jėzus sudraudė: “Liaukitės! Užteks!” Ir palietęs tarno ausį, išgydė jį.
51Hapo, Yesu akasema, "Acha! Hii inatosha." Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52Atėjusiems aukštiesiems kunigams, šventyklos apsaugos viršininkams ir vyresniesiems Jis pasakė: “Kaip prieš plėšiką išėjote prieš mane su kalavijais ir vėzdais.
52Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: "Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53Kai buvau kasdien su jumis šventykloje, jūs nepakėlėte prieš mane rankos. Bet ši valanda jūsų, tamsos valdžia”.
53Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza."
54Suėmę Jėzų, jie nusivedė Jį ir atvedė į vyriausiojo kunigo namus. Petras sekė iš tolo.
54Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55Susikūrę ugnį kiemo viduryje, jie susėdo. Petras atsisėdo kartu.
55Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56Viena tarnaitė, pamačiusi jį sėdintį prieš šviesą, įsižiūrėjo ir tarė: “Ir šitas buvo kartu su Juo”.
56Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, "Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu."
57Bet jis išsigynė, sakydamas: “Moterie, nepažįstu Jo!”
57Lakini Petro akakana akisema, "Wee! simjui mimi."
58Truputį vėliau kažkas kitas, jį pamatęs, tarė: “Ir tu esi iš jų”. Petras atsakė: “Ne, žmogau, nesu!”
58Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, "Wewe ni mmoja wao." Lakini Petro akajibu "Bwana we; si mimi!"
59Maždaug po valandos dar vienas ėmė tvirtinti, sakydamas: “Tikrai šitas buvo su Juo! Juk jis galilėjietis!”
59Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, "Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati."
60Petras atsakė: “Žmogau, aš nesuprantu, ką tu sakai”. Ir tuoj pat, dar jam kalbant, pragydo gaidys.
60Lakini Petro akasema, "Bwana wee; sijui hata unachosema!" Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61Tada Viešpats atsigręžęs pažvelgė į Petrą. Ir Petras atsiminė Viešpaties žodį, kaip Jis buvo jam pasakęs: “Dar gaidžiui nepragydus, tu tris kartus manęs išsiginsi”.
61Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: "Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
62Petras išėjo laukan ir karčiai pravirko.
62Hapo akatoka nje, akalia sana.
63Jėzų saugantys vyrai tyčiojosi iš Jo ir mušė.
63Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64Uždengę akis, jie daužė Jam per veidą ir klausinėjo: “Pranašauk, kas Tave užgavo!”
64Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, "Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!"
65Ir visaip kitaip jam piktžodžiavo.
65Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66Rytui išaušus, susirinko tautos vyresnieji, aukštieji kunigai ir Rašto žinovai. Jie atvedė Jėzų į savo sinedrioną ir sakė:
66Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67“Jei Tu Kristus, tai prisipažink mums!” Jėzus atsiliepė: “Jeigu jums ir pasakysiu, vis tiek netikėsite,
67Nao wakamwambia, "Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?" Lakini Yesu akawaambia, "Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68o jei paklausiu, man neatsakysite ir nepaleisite.
68na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69Tačiau nuo šio meto Žmogaus Sūnus sėdės Dievo Galybės dešinėje”.
69Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi."
70Tuomet jie visi klausė: “Tai Tu esi Dievo Sūnus?” Jis atsakė: “Taip yra kaip sakote: Aš Esu!”
70Hapo wote wakasema, "Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?" Naye akasema, "Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye."
71Tada jie tarė: “Kam dar mums liudijimas?! Juk mes girdėjome iš Jo paties lūpų!”
71Nao wakasema, "Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe."