1Penkioliktais ciesoriaus Tiberijaus viešpatavimo metais, Poncijui Pilotui valdant Judėją, Erodui esant Galilėjos tetrarchu, jo broliui PilypuiIturėjos bei Trachonitidės krašto tetrarchu, LisanijuiAbilenės tetrarchu,
1Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2prie vyriausiųjų kunigų Ano ir Kajafo, buvo Viešpaties žodis Zacharijo sūnui Jonui dykumoje.
2na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3Jis apėjo visą Pajordanę, skelbdamas atgailos krikštą nuodėmėms atleisti,
3Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4kaip parašyta pranašo Izaijo žodžių knygoje: “Dykumoje šaukiančiojo balsas: ‘Paruoškite Viešpačiui kelią, ištiesinkite Jam takus!
4Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5Kiekvienas slėnis tebūna užpiltas, kiekvienas kalnas bei kalnelisnulygintas. Kreivi keliai tetampa tiesūs, o duobėtiišlyginti.
5Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6Ir kiekvienas kūnas išvys Dievo išgelbėjimą’ ”.
6Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."
7Ateinančioms pas jį krikštytis minioms Jonas sakė: “Angių išperos, kas perspėjo jus bėgti nuo besiartinančios rūstybės?
7Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8Duokite vaisių, vertų atgailos! Ir nebandykite ramintis: ‘Mūsų tėvasAbraomas’. Aš jums sakau, kad Dievas gali pažadinti Abraomui vaikų iš šitų akmenų.
8Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9Štai kirvis jau prie medžių šaknų. Kiekvienas medis, kuris neduoda gerų vaisių, yra nukertamas ir įmetamas į ugnį”.
9Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni."
10Minios jį klausė: “Ką gi mums daryti?!”
10Umati wa watu ukamwuliza, "Tufanye nini basi?"
11Jis joms atsakė: “Kas turi dvi tunikas, tepasidalina su neturinčiu, ir kas turi maisto, tegul taip pat daro”.
11Akawajibu, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."
12Ėjo ir muitininkai krikštytis ir klausė: “Mokytojau, ką mums daryti?”
12Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, "Mwalimu, tufanye nini?"
13Jis sakė jiems: “Nereikalaukite daugiau, kaip jums nustatyta”.
13Naye akawaambia, "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."
14Taip pat ir kariai klausė: “Ką mums daryti?” Jis jiems atsakė: “Nieko neskriauskite, melagingai neskųskite, tenkinkitės savo alga”.
14Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?" Naye akawajibu, "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."
15Žmonėms esant apimtiems lūkesčio ir visiems mąstant širdyse apie Joną, ar kartais jis ne Kristus,
15Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16Jonas visiems kalbėjo: “Aš, tiesa, krikštiju jus vandeniu, bet ateina už mane galingesnis, kuriam aš nevertas atrišti sandalų dirželio. Jis krikštys jus Šventąja Dvasia ir ugnimi.
16Hapo Yohane akawaambia wote, "Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17Jo rankoje vėtyklė: Jis kruopščiai išvalys savo kluoną ir surinks kviečius į klėtį, o pelus sudegins neužgesinama ugnimi”.
17Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
18Ir dar daug kitų paraginimų jis davė tautai, skelbdamas Gerąją naujieną.
18Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19Tetrarchas Erodas, Jono baramas dėl Erodiados, savo brolio žmonos, ir dėl visų piktadarybių, kurias buvo padaręs,
19Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20pridėjo prie jų dar ir tai, kad uždarė Joną į kalėjimą.
20Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21Kai, visai tautai krikštijantis, ir Jėzus pakrikštytas meldėsi, atsivėrė dangus,
21Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22ir Šventoji Dvasia kūnišku pavidalu nusileido ant Jo tarsi balandis, o balsas iš dangaus prabilo: “Tu mano mylimasis Sūnus, Tavimi Aš gėriuosi”.
22na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
23Jėzui buvo apie trisdešimt metų, kai Jis pradėjo veikti. Jis buvo laikomas sūnumi Juozapo, Helio,
23Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24Matato, Levio, Melchio, Janajo, Juozapo,
24Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25Matatijo, Amoso, Naumo, Heslio, Nagajo,
25mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26Maato, Matatijo, Semeino, Josecho, Jodos,
26mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27Joanano, Resos, Zorobabelio, Salatielio, Nerio,
27mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28Melchio, Adijo, Kosamo, Elmadamo, Ero,
28mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29Jėzaus, Eliezero, Jorimo, Matato, Levio,
29mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30Simeono, Judo, Juozapo, Jonamo, Eliakimo,
30mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31Melėjo, Menos, Matatos, Natano, Dovydo,
31mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32Jesės, Jobedo, Boozo, Salmono, Naasono,
32mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33Aminadabo, Aramo, Esromo, Faro, Judo,
33mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34Jokūbo, Izaoko, Abraomo, Taros, Nachoro,
34mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35Serucho, Ragaujo, Faleko, Ebero, Salos,
35mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36Kainamo, Arfaksado, Semo, Nojaus, Lamecho,
36mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37Matūzalio, Henocho, Jareto, Maleleelio, Kainamo,
37mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38Eno, Seto, Adomo, Dievo.
38mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.