Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

4

1Kupinas Šventosios Dvasios Jėzus grįžo nuo Jordano, ir Dvasia Jį nuvedė į dykumą
1Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
2keturiasdešimčiai dienų, ir Jis buvo velnio gundomas. Jis nieko nevalgė per tas dienas ir, joms pasibaigus, buvo alkanas.
2Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
3Tada velnias Jam tarė: “Jei Tu Dievo Sūnus, liepk, kad šitas akmuo pavirstų duona”.
3Ndipo Ibilisi akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate."
4Jėzus jam atsakė: “Parašyta: ‘Žmogus gyvens ne viena duona, bet kiekvienu Dievo žodžiu’ ”.
4Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu."
5Tada velnias, užvedęs Jį į aukštą kalną, viena akimirka parodė Jam visas pasaulio karalystes.
5Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
6Velnias Jam tarė: “Duosiu Tau visą jų valdžią ir šlovę; jos man atiduotos, ir kam noriu, tam jas duodu.
6"Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
7Todėl, jei parpuolęs pagarbinsi mane, visa bus Tavo”.
7Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
8O Jėzus jam atsakė: “Eik šalin nuo manęs, šėtone! Parašyta: ‘Viešpatį, savo Dievą, tegarbink ir Jam vienam tetarnauk!’ ”
8Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."
9Velnias nusivedė Jį į Jeruzalę, pastatė ant šventyklos šelmens ir tarė: “Jei Tu Dievo Sūnus, pulk žemyn,
9Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, "Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
10nes parašyta: ‘Jis lieps savo angelams saugoti Tave,
10kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
11ir jie nešios Tave ant rankų, kad neužsigautum kojos į akmenį’ ”.
11na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe."
12Jėzus jam atsakė: “Pasakyta: ‘Negundyk Viešpaties, savo Dievo!’ ”
12Lakini Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako."
13Baigęs visus gundymus, velnias pasitraukė nuo Jo iki laiko.
13Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
14Su Dvasios jėga Jėzus grįžo į Galilėją, ir visame krašte pasklido apie Jį garsas.
14Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
15Jis mokė jų sinagogose, visų gerbiamas.
15Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
16Jis atėjo į Nazaretą, kur buvo užaugęs. Sabato dieną, kaip pratęs, nuėjo į sinagogą ir atsistojo skaityti.
16Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
17Jam padavė pranašo Izaijo knygos ritinį. Atvyniojęs ritinį, Jis rado vietą, kur parašyta:
17Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
18“Viešpaties Dvasia ant manęs, nes Jis patepė mane skelbti Gerąją naujieną vargšams, pasiuntė mane gydyti tų, kurių širdys sudužusios, skelbti belaisviams išvadavimo, akliesiems­regėjimo, siuntė vaduoti prislėgtųjų
18"Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
19ir skelbti maloningųjų Viešpaties metų”.
19na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
20Suvyniojęs knygos ritinį, Jėzus grąžino jį patarnautojui ir atsisėdo; visų sinagogoje esančių akys buvo įsmeigtos į Jį.
20Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
21Ir Jis pradėjo jiems kalbėti: “Šiandien išsipildė ką tik jūsų girdėti Rašto žodžiai”.
21Naye akaanza kuwaambia, "Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo."
22Visi Jam pritarė ir stebėjosi maloniais žodžiais, sklindančiais iš Jo lūpų. Ir jie sakė: “Argi Jis ne Juozapo sūnus?!”
22Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, "Je, huyu si mwana wa Yosefu?"
23O Jėzus jiems atsakė: “Jūs, be abejo, man priminsite patarlę: ‘Gydytojau, pats pasigydyk’­padaryk ir čia, savo tėviškėje, darbų, kokių girdėjome buvus Kafarnaume”.
23Naye akawaambia, "Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako."
24Ir Jis tarė: “Iš tiesų sakau jums: joks pranašas nepriimamas savo tėviškėje.
24Akaendelea kusema, "Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
25Bet sakau jums tiesą: daug našlių buvo Izraelyje Elijo dienomis, kai dangus buvo uždarytas trejus metus ir šešis mėnesius ir baisus badas ištiko visą kraštą.
25Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
26Bet nė pas vieną iš jų nebuvo siųstas Elijas, o tik pas našlę Sidono mieste, Sareptoje.
26Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
27Taip pat pranašo Eliziejaus laikais daug buvo raupsuotųjų Izraelyje, bet nė vienas iš jų nebuvo išgydytas, tik siras Naamanas”.
27Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria."
28Visi, kurie buvo sinagogoje, tai išgirdę, labai užsirūstino;
28Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
29pakilę išvarė Jį iš miesto, iki šlaito to kalno, ant kurio pastatytas jų miestas, ir norėjo nustumti Jį žemyn.
29Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
30Bet Jėzus, praėjęs tarp jų, pasišalino.
30Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
31Jis nuėjo į Galilėjos miestą Kafarnaumą ir kiekvieną sabatą mokė žmones.
31Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
32Jie labai stebėjosi Jo mokymu, nes Jo žodžiai buvo su valdžia.
32Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
33Sinagogoje buvo žmogus, kuris turėjo netyrą demonišką dvasią. Jis pradėjo garsiai šaukti:
33Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
34“Šalin! Ko Tau iš mūsų reikia, Jėzau iš Nazareto?! Gal atėjai mūsų pražudyti? Aš žinau, kas Tu: Dievo Šventasis!”
34"We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!"
35Jėzus sudraudė jį: “Nutilk ir išeik iš jo!” Nubloškęs žmogų į vidurį, demonas išėjo, nė kiek jo nesužeidęs.
35Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: "Nyamaza! Mtoke mtu huyu!" Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
36Visi nustėro ir kalbėjosi: “Kas tai per žodis: Jis su valdžia ir jėga įsakinėja netyrosioms dvasioms, ir tos pasitraukia?!”
36Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, "Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!"
37Garsas apie Jį plito visose aplinkinėse vietovėse.
37Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
38Iš sinagogos Jėzus atėjo į Simono namus. Simono uošvė labai karščiavo, ir jie prašė jai pagalbos.
38Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
39Atsistojęs prie jos galvūgalio, Jis sudraudė karštligę, ir toji dingo. Ji iškart atsikėlė ir jiems patarnavo.
39Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
40Saulei leidžiantis, visi, kurie turėjo ligonių, įvairiomis ligomis sergančių, vedė juos prie Jėzaus, o Jis gydė, ant kiekvieno uždėdamas rankas.
40Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
41Iš daugelio išeidavo demonai, šaukdami: “Tu Dievo Sūnus!” Bet Jis drausdavo juos, neleisdamas jiems kalbėti, nes jie žinojo Jį esant Kristų.
41Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: "Wewe u Mwana wa Mungu!" Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
42Dienai išaušus, Jis išėjęs pasitraukė į negyvenamą vietą. Minios Jo ieškojo ir, atėjusios pas Jį, bandė sulaikyti Jį, kad jų nepaliktų.
42Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
43Jis jiems tarė: “Ir kitiems miestams turiu skelbti Gerąją naujieną apie Dievo karalystę, nes tam esu siųstas”.
43Lakini yeye akawaambia, "Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo."
44Ir Jis pamokslavo Galilėjos sinagogose.
44Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.