Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

5

1Kartą, kai minios veržėsi prie Jo klausytis Dievo žodžio, Jis stovėjo prie Genezareto ežero
1Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2ir pamatė dvi valtis, stovinčias prie ežero kranto. Žvejai buvo išlipę iš jų ir plovė tinklus.
2Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3Įlipęs į vieną valtį, kuri buvo Simono, Jis paprašė truputį atsistumti nuo kranto ir atsisėdęs mokė minias iš valties.
3Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4Baigęs kalbėti, Jis tarė Simonui: “Irkis į gilumą ir išmeskite tinklus valksmui”.
4Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, "Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki."
5Simonas Jam atsakė: “Mokytojau, visą naktį vargę, mes nieko nesugavome, bet dėl Tavo žodžio užmesiu tinklą”.
5Simoni akamjibu, "Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu."
6Tai padarę, jie užgriebė didelę daugybę žuvų, kad net jų tinklas pradėjo trūkinėti.
6Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7Jie pamojo savo bendrininkams, buvusiems kitoje valtyje, atplaukti į pagalbą. Tie atplaukė ir pripildė žuvų abi valtis, kad jos beveik skendo.
7Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8Tai matydamas, Simonas Petras puolė Jėzui po kojų, sakydamas: “Pasitrauk nuo manęs, Viešpatie, nes aš­nusidėjėlis!”
8Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!"
9Mat jį ir visus draugus apėmė nuostaba dėl to valksmo žuvų, kurias jie sugavo;
9Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10taip pat Zebediejaus sūnus Jokūbą ir Joną, kurie buvo Petro bendrai. O Jėzus tarė Simonui: “Nebijok! Nuo šiol žmones žvejosi”.
10Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, "Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu."
11Išvilkę į krantą valtis, jie viską paliko ir nusekė paskui Jį.
11Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12Jam esant viename mieste, atėjo vyras, visas raupsuotas. Pamatęs Jėzų, jis parpuolė ant žemės ir maldavo: “Viešpatie, jei nori, gali mane apvalyti!”
12Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: "Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa."
13Jėzus, ištiesęs ranką, palietė raupsuotąjį ir tarė: “Noriu, būk švarus!” Ir iškart raupsai pranyko.
13Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, "Nataka, takasika!" Mara ule ukoma ukamwacha.
14Jėzus jam liepė niekam šito nepasakoti: “Tik nueik, pasirodyk kunigui ir atiduok auką už pagijimą, kaip Mozės įsakyta, jiems paliudyti”.
14Yesu akamwamuru: "Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
15Tačiau garsas apie Jį sklido vis plačiau, ir didelės minios rinkdavosi Jo pasiklausyti bei pagyti nuo savo ligų.
15Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16O Jis pasitraukdavo į dykvietes melstis.
16Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17Vieną dieną, kai Jis mokė žmones, ten sėdėjo fariziejų bei Įstatymo mokytojų, susirinkusių iš visų Galilėjos ir Judėjos kaimų bei Jeruzalės. Ir ten buvo Viešpaties jėga, kad gydytų žmones.
17Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18Štai vyrai neštuvais atnešė paralyžiuotą žmogų. Jie bandė jį įnešti į vidų ir paguldyti priešais Jėzų.
18Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19Nerasdami pro kur įnešti dėl žmonių gausybės, jie užlipo ant stogo ir, praardę jį, nuleido ligonį kartu su neštuvais žemyn ties Jėzumi.
19Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20Matydamas jų tikėjimą, Jis tarė: “Žmogau, tavo nuodėmės tau atleistos!”
20Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, "Rafiki, umesamehewa dhambi zako."
21Tada Rašto žinovai ir fariziejai pradėjo svarstyti: “Kas per vienas šitas piktžodžiaujantis? Kas gali atleisti nuodėmes, jei ne vienas Dievas?”
21Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: "Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!"
22Jėzus, supratęs jų mintis, prabilo: “Kodėl taip svarstote savo širdyse?
22Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, "Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23Kas lengviau­ar pasakyti: ‘Tavo nuodėmės tau atleistos’, ar pasakyti: ‘Kelkis ir vaikščiok’?
23Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24O kad žinotumėte Žmogaus Sūnų turint žemėje valdžią atleisti nuodėmes,­čia Jis tarė paralyžiuotajam,­sakau tau: kelkis, imk savo gultą ir eik namo!”
24Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani."
25Tas tuojau atsikėlė jų akivaizdoje, pasiėmė neštuvus ir, šlovindamas Dievą, nuėjo namo.
25Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26Visi didžiai stebėjosi ir šlovino Dievą. Apimti baimės, jie kalbėjo: “Šiandien matėme stebinančių dalykų!”
26Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: "Tumeona maajabu leo."
27Po to išėjęs Jis pastebėjo muitininką, vardu Levį, sėdintį muitinėje, ir jam tarė: “Sek paskui mane!”
27Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, "Nifuate!"
28Tas atsikėlė ir, viską palikęs, nusekė paskui Jį.
28Lawi akaacha yote, akamfuata.
29Levis savo namuose iškėlė Jam didelį pokylį. Prie stalo susirinko gausus būrys muitininkų ir kitų svečių.
29Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30Rašto žinovai ir fariziejai murmėjo ir prikaišiojo Jėzaus mokiniams: “Kodėl jūs valgote ir geriate su muitininkais ir nusidėjėliais?”
30Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: "Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
31Jėzus jiems atsakė: “Ne sveikiesiems reikia gydytojo, bet ligoniams.
31Yesu akawajibu, "Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32Aš atėjau šaukti ne teisiųjų, bet nusidėjėlių atgailai”.
32Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu."
33Tada jie sakė Jam: “Kodėl Jono mokiniai dažnai pasninkauja ir meldžiasi, taip pat ir fariziejų mokiniai, o Tavieji valgo ir geria?”
33Watu wengine wakamwambia Yesu, "Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa."
34Jėzus jiems atsakė: “Argi galite versti pasninkauti vestuvininkus, kol su jais yra jaunikis?
34Yesu akawajibu, "Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35Ateis dienos, kai jaunikis bus iš jų atimtas, ir tada, tomis dienomis, jie pasninkaus”.
35Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga."
36Jėzus dar pasakė jiems palyginimą: “Niekas neplėšia lopo iš naujo drabužio ir nesiuva jo ant seno. Nes ir naująjį jis suplėšytų, ir senajam netiktų lopas iš naujojo.
36Yesu akawaambia mfano huu: "Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37Taip pat niekas nepila jauno vyno į senus vynmaišius. Jaunas vynas suplėšytų vynmaišius, pats ištekėtų, ir vynmaišiai niekais nueitų.
37Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38Jauną vyną reikia pilti į naujus vynmaišius, ir tada abeji išsilaiko.
38Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39Ir niekas, gėręs seno vyno, nenori jauno; jis sako: ‘Senasis geresnis!’ ”
39Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi."