Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

6

1Vieną sabatą, Jam einant per javų lauką, mokiniai skabė varpas ir, ištrynę tarp delnų, valgė.
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2Kai kurie iš fariziejų jiems tarė: “Kodėl darote, kas per sabatą draudžiama?!”
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
3Jėzus jiems atsakė: “Nejaugi neskaitėte, ką darė Dovydas, kai buvo alkanas pats ir jo palydovai?
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4Kaip jis įėjo į Dievo namus, ėmė padėtinės duonos, valgė ir davė savo palydai, nors jos niekam neleistina valgyti, tik kunigams!”
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
5Ir Jis pridūrė: “Žmogaus Sūnus yra ir sabato Viešpats”.
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
6Kitą sabatą Jis nuėjo į sinagogą ir mokė. Ten buvo žmogus, kurio dešinė ranka buvo padžiūvusi.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7Rašto žinovai ir fariziejai stebėjo, ar Jis gydys per sabatą, kad rastų kuo Jį apkaltinti.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8Bet Jis, žinodamas jų mintis, tarė vyrui su padžiūvusia ranka: “Kelkis ir stok į vidurį”. Tas atsistojo.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9Tada Jėzus jiems pasakė: “Aš klausiu jūsų: ar per sabatą leistina gera daryti ar bloga? Gelbėti gyvybę ar pražudyti?”
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
10Ir, apžvelgęs visus aplinkui, tarė tam žmogui: “Ištiesk savo ranką!” Tas taip padarė, ir jo ranka tapo sveika kaip ir kita.
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11O jie baisiai įniršo ir tarėsi, ką galėtų Jėzui padaryti.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12Tomis dienomis Jis užkopė į kalną melstis ir ten praleido visą naktį, melsdamasis Dievui.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13Išaušus rytui, Jis pasišaukė savo mokinius ir iš jų išsirinko dvylika, kuriuos ir pavadino apaštalais:
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14Simoną, kurį praminė Petru, jo brolį Andriejų, Jokūbą, Joną, Pilypą ir Baltramiejų,
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15Matą ir Tomą, Alfiejaus sūnų Jokūbą ir Simoną, vadinamą Uoliuoju,
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16Jokūbo sūnų Judą ir Judą Iskarijotą, kuris tapo išdaviku.
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17Nusileidęs su jais žemyn, sustojo lygumoje. Ten buvo daugybė Jo mokinių ir didelės minios žmonių iš visos Judėjos ir Jeruzalės, iš Tyro ir Sidono pajūrio. Jie susirinko Jo pasiklausyti ir pagyti nuo savo ligų.
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18Buvo pagydomi kankinamieji netyrųjų dvasių.
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19Visa minia stengėsi Jį paliesti, nes iš Jo ėjo jėga ir visus gydė.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20Tada, pakėlęs akis į savo mokinius, Jis prabilo: “Palaiminti jūs, vargšai, nes jūsų yra Dievo karalystė.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21Palaiminti, kurie dabar alkstate, nes būsite pasotinti. Palaiminti, kurie dabar verkiate, nes juoksitės.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22Palaiminti jūs, kai žmonės jūsų nekęs, kai jus atskirs, šmeiš ir atmes jūsų vardą kaip blogą dėl Žmogaus Sūnaus.
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23Džiaukitės tą dieną ir linksminkitės, nes štai jūsų atlygis didelis danguje. Taip jų protėviai darė pranašams.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24Bet vargas jums, turtingieji, nes jūs jau atsiėmėte savo paguodą!
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Vargas jums, kurie dabar sotūs, nes būsite alkani! Vargas jums, kurie dabar juokiatės, nes jūs liūdėsite ir verksite!
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Vargas jums, kai visi žmonės jus giria, nes ir jų protėviai taip gyrė netikrus pranašus!”
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27“Bet jums, kurie klausotės, sakau: mylėkite savo priešus, darykite gera tiems, kurie jūsų nekenčia.
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28Laiminkite tuos, kurie jus keikia, ir melskitės už savo skriaudėjus.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29Kas trenkia tau per vieną skruostą, atsuk ir antrąjį; kas atima iš tavęs apsiaustą, atiduok jam ir tuniką.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30Duok kiekvienam, kuris prašo, ir nereikalauk atgal iš to, kuris tavo atėmė.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31Kaip norite, kad jums žmonės darytų, taip ir jūs darykite jiems.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32Jei mylite tuos, kurie jus myli, tai koks čia jūsų nuopelnas? Juk ir nusidėjėliai myli juos mylinčius.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33Jei darote gera tiems, kurie jums gera daro, tai koks jūsų nuopelnas? Juk ir nusidėjėliai taip daro.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34Jei skolinate tik tiems, iš kurių tikitės atgausią, koks jūsų nuopelnas? Juk ir nusidėjėliai skolina nusidėjėliams, kad atgautų paskolą.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35Bet mylėkite savo priešus, darykite gera ir skolinkite, nieko nesitikėdami. Tuomet jūsų atlygis bus didelis, ir jūs būsite Aukščiausiojo vaikai; nes Jis maloningas ir nedėkingiesiems, ir piktiesiems.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36Būkite gailestingi, kaip ir jūsų Tėvas yra gailestingas.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37Neteiskite ir nebūsite teisiami; nesmerkite ir nebūsite pasmerkti; atleiskite, ir jums bus atleista.
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38Duokite, ir jums bus duota; saiką gerą, prikimštą, sukratytą ir su kaupu duos jums į užantį. Kokiu saiku seikite, tokiu jums bus atseikėta”.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
39Jis pasakė jiems palyginimą: “Ar gali aklas vesti aklą? Argi ne abu įkris į duobę?!
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40Mokinys nėra viršesnis už savo mokytoją: kiekvienas mokinys, jei gerai išlavintas, bus kaip jo mokytojas.
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41Kodėl matai krislą brolio akyje, o nepastebi rąsto savojoje?
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42Ir kaip gali sakyti broliui: ‘Broli, leisk, išimsiu krislą iš tavo akies’,­pats nematydamas savo akyje rąsto?! Veidmainy, pirmiau išritink rąstą iš savo akies, o tada matysi, kaip iš brolio akies išimti krislelį.
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43Nėra gero medžio, kuris duotų blogus vaisius, ir nėra blogo, kuris duotų gerus vaisius.
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44Kiekvienas medis pažįstamas iš jo vaisių. Nuo erškėčių niekas nerenka figų, o nuo gervuogių krūmo neskina vynuogių.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45Geras žmogus iš gero savo širdies lobyno iškelia gera, o blogas iš blogo savo širdies lobyno iškelia bloga. Jo lūpos kalba tai, ko pertekusi širdis”.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46“Kodėl vadinate mane: ‘Viešpatie, Viešpatie’, o nedarote, ką sakau?
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47Kiekvienas, kuris ateina pas mane, klausosi mano žodžių ir juos vykdo,­Aš parodysiu jums, į ką jis panašus.
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48Jis panašus į namą statantį žmogų, kuris giliai iškasė žemę ir padėjo pamatus ant uolos. Užėjus potvyniui, srovė atsimušė į tą namą, bet neįstengė jo pajudinti, nes buvo pastatytas ant uolos.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49O kas klausosi, bet nevykdo, panašus į žmogų, pasistačiusį namą be pamato, ant žemės. Vos tik srovė į jį atsimušė, jis kaipmat sugriuvo, ir to namo griuvimas buvo smarkus”.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"