Lithuanian

Swahili: New Testament

Luke

7

1Baigęs visus savo pamokymus klausytojams, Jėzus sugrįžo į Kafarnaumą.
1Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
2Vieno šimtininko branginamas tarnas sirgo ir buvo arti mirties.
2Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
3Išgirdęs apie Jėzų, šimtininkas pasiuntė pas Jį kelis žydų vyresniuosius, prašydamas Jį ateiti ir išgydyti tarną.
3Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
4Atėję pas Jėzų, jie karštai prašė, sakydami: “Jis vertas, kad jam tai padarytum,
4Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: "Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
5nes jis myli mūsų tautą ir mums yra pastatęs sinagogą”.
5maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi."
6Jėzus nuėjo su jais. Kai Jis buvo netoli namų, šimtininkas atsiuntė savo draugus, kad Jam pasakytų: “Viešpatie, nesivargink! Aš nesu vertas, kad užeitum po mano stogu.
6Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: "Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
7Taip pat savęs nelaikau vertu ateiti pas Tave. Bet tark žodį, ir mano tarnas pasveiks.
7Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
8Juk ir aš, būdamas valdinys, turiu sau pavaldžių kareivių. Taigi sakau kuriam iš jų: ‘Eik’, ir jis eina; sakau kitam: ‘Ateik čia’, ir jis ateina; sakau tarnui: ‘Padaryk tai’, ir jis daro”.
8Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya."
9Tai girdėdamas, Jėzus stebėjosi juo ir, atsigręžęs į Jį lydinčią minią, tarė: “Sakau jums—net Izraelyje neradau tokio didelio tikėjimo!”
9Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, "Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli."
10Sugrįžę į namus, pasiųstieji rado tarną pasveikusį.
10Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
11Po to Jėzus ėjo į miestą, vardu Nainą. Kartu su Juo keliavo daugelis Jo mokinių ir gausi minia.
11Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
12Kai Jis prisiartino prie miesto vartų, štai nešė numirėlį­vienintelį motinos sūnų, o ji buvo našlė. Kartu su ja ėjo didelė miesto minia.
12Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
13Pamačiusiam motiną Viešpačiui pagailo jos, ir Jis tarė: “Neverk!”
13Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, "Usilie."
14Priėjęs Jis palietė neštuvus. Nešėjai sustojo, ir Jis pasakė: “Jaunuoli, sakau tau: kelkis!”
14Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, "Kijana! Nakuamuru, amka!"
15Numirėlis atsisėdo ir pradėjo kalbėti. Jėzus atidavė jį motinai.
15Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16Visus apėmė baimė, ir jie šlovino Dievą, sakydami: “Didis pranašas iškilo tarp mūsų”, ir: “Dievas aplankė savo tautą”.
16Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: "Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake."
17Ta žinia apie Jį pasklido po visą Judėją ir visą apylinkę.
17Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
18Visa tai pranešė Jonui jo mokiniai.
18Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
19Tada Jonas, pasišaukęs du savo mokinius, siuntė juos pas Jėzų paklausti: “Ar Tu esi Tas, kuris turi ateiti, ar mums laukti kito?”
19aliwatuma kwa Bwana wamwulize: "Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
20Atėję pas Jį, tie vyrai tarė: “Jonas Krikštytojas mus siuntė pas Tave, klausdamas: ‘Ar Tu esi Tas, kuris turi ateiti, ar mums laukti kito?’ ”
20Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, "Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
21Kaip tik tuo metu Jis pagydė daugelį nuo ligų bei negalių ir nuo piktųjų dvasių, daugeliui aklųjų dovanojo regėjimą.
21Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
22Tad atsakydamas, Jis tarė jiems: “Nuėję praneškite Jonui, ką matėte ir girdėjote: aklieji regi, luošieji vaikščioja, raupsuotieji apvalomi, kurtieji girdi, mirusieji prikeliami, vargšams skelbiama Geroji naujiena.
22Basi, Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
23Ir palaimintas, kas nepasipiktins manimi”.
23Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!"
24Jono pasiuntiniams nuėjus, Jis pradėjo kalbėti minioms apie Joną: “Ko išėjote į dykumą pažiūrėti? Ar vėjo linguojamos nendrės?
24Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: "Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
25Ko išėjote pamatyti? Ar švelniais drabužiais vilkinčio žmogaus? Antai tie, kurie ištaigingai vilki ir prabangiai gyvena, yra karaliaus rūmuose.
25Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
26Tai ko gi išėjote pamatyti? Ar pranašo? Taip, sakau jums, ir daug daugiau negu pranašo.
26Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
27Jis yra tas, apie kurį parašyta: ‘Štai Aš siunčiu pirma Tavęs savo pasiuntinį, kuris nuties Tau kelią’.
27Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia."
28Sakau jums: tarp gimusių iš moters nebuvo didesnio pranašo už Joną Krikštytoją, bet ir mažiausias Dievo karalystėje didesnis už jį.
28Yesu akamalizia kwa kusema, "Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye."
29Jį išgirdusi, visa tauta, taip pat ir muitininkai, pripažino Dievo teisingumą, nes leidosi krikštijami Jono krikštu.
29Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
30Tik fariziejai ir Įstatymo mokytojai atstūmė, ką Dievas jiems buvo sumanęs, nesiduodami Jono krikštijami”.
30Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
31“Su kuo galėčiau palyginti šios kartos žmones? Į ką jie panašūs?
31Yesu akaendelea kusema, "Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
32Jie panašūs į vaikus, kurie, susėdę turgavietėje, vieni kitiems šaukia: ‘Mes jums grojome, o jūs nešokote; mes giedojome raudas, o jūs neverkėte’.
32Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
33Buvo atėjęs Jonas Krikštytojas. Jis nevalgė duonos ir negėrė vyno, tai jūs sakėte: ‘Jis demono apsėstas’.
33Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
34Atėjo Žmogaus Sūnus; Jis valgo ir geria, tai jūs vėl sakote: ‘Štai rijūnas ir vyno gėrėjas, muitininkų ir nusidėjėlių bičiulis’.
34Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
35Bet išmintį pateisina visi jos vaikai”.
35Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali."
36Vienas fariziejus pakvietė Jėzų kartu valgyti. Atėjęs į fariziejaus namus, Jis sėdo prie stalo.
36Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
37Ir štai moteris, kuri buvo žinoma mieste nusidėjėlė, sužinojusi, kad Jis fariziejaus namuose, atsinešė alebastrinį indą kvapaus tepalo
37Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
38ir, verkdama priėjusi iš užpakalio prie Jo kojų, ėmė laistyti jas ašaromis, šluostyti savo galvos plaukais, bučiavo Jo kojas ir tepė jas tepalu.
38Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
39Tai matydamas, fariziejus, kuris Jėzų pasikvietė, samprotavo: “Jeigu šitas būtų pranašas, Jis žinotų, kas tokia ši moteris, kuri Jį liečia, nes ji­nusidėjėlė!”
39Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, "Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi."
40O Jėzus tarė: “Simonai, turiu tau ką pasakyti”. Tas atsiliepė: “Sakyk, Mokytojau!”
40Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, "Simoni, ninacho kitu cha kukwambia." Naye Simoni akamwambia, "Ndio Mwalimu, sema." Yesu akasema,
41“Skolintojas turėjo du skolininkus. Vienas buvo skolingas penkis šimtus denarų, o kitas­penkiasdešimt.
41"Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
42Jiems neturint iš ko atiduoti, jis dovanojo abiem. Kuris labiau jį mylės?”
42Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?"
43Simonas atsakė: “Manau, jog tas, kuriam daugiau dovanota”. Jėzus tarė: “Teisingai nusprendei”.
43Simoni akamjibu, "Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana." Yesu akamwambia, "Sawa."
44Ir, atsisukęs į moterį, Jis tarė Simonui: “Matai šitą moterį? Aš atėjau į tavo namus, tu nedavei man vandens kojoms nusimazgoti, o ji laistė jas ašaromis ir šluostė savo plaukais.
44Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, "Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
45Tu manęs nepabučiavai, o ji, vos man atėjus, nesiliauja bučiavusi mano kojų.
45Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
46Tu aliejumi man galvos nepatepei, o ji tepalu patepė man kojas.
46Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
47Todėl sakau tau: jos gausios nuodėmės jai atleidžiamos, nes ji labai pamilo. Kam mažai atleista, tas menkai myli”.
47Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo."
48Jis tarė jai: “Tavo nuodėmės atleistos”.
48Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, "Umesamehewa dhambi zako."
49Esantieji kartu su Juo už stalo ėmė svarstyti: “Kas gi Jis toks, kad net ir nuodėmes atleidžia?!”
49Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, "Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?"
50O Jis tarė moteriai: “Tavo tikėjimas išgelbėjo tave. Eik rami”.
50Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, "Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani."