1Prisiartinęs prie Jeruzalės pro Betfagę ir Betaniją, ties Alyvų kalnu, Jėzus pasiuntė du savo mokinius,
1Walipokuwa wanakaribia Yerusalemu walifika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni. Hapo aliwatuma wawili wa wanafunzi wake,
2liepdamas: “Eikite į priešais esantį kaimą ir, vos įžengę į jį, rasite pririštą asilaitį, kuriuo dar niekas iš žmonių nėra jojęs. Atriškite jį ir atveskite”.
2akawaambia, "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia humo, mtakuta mwana punda amefungwa ambaye bado hajatumiwa na mtu. Mfungueni mkamlete.
3Jeigu kas nors paklaustų: ‘Ką čia darote?’, atsakykite: ‘Jo reikia Viešpačiui’, ir iš karto jį paleis.
3Kama mtu akiwauliza, Mbona mnafanya hivyo? Mwambieni, Bwana anamhitaji na atamrudisha hapa mara."
4Nuėję jiedu rado pakelėje asilaitį, pririštą prie vartų, ir atrišo jį.
4Basi, wakaenda, wakamkuta mwana punda barabarani amefungwa mlangoni. Walipokuwa wakimfungua,
5Kai kurie iš ten stovinčių jų paklausė: “Ką darote, kam atrišate asilaitį?”
5baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo wakawauliza "Kwa nini mnamfungua huyo mwana punda?"
6O jie atsakė taip, kaip Jėzus buvo jiems liepęs, ir tie leido jį vestis.
6Wanafunzi wakajibu kama Yesu alivyokuwa amewaambia; nao wakawaacha waende zao.
7Jie atvedė asilaitį pas Jėzų, apdengė jį savo apsiaustais, ir Jėzus užsėdo ant jo.
7Wakampelekea Yesu huyo mwana punda. Wakatandika mavazi yao juu ya huyo mwana punda, na Yesu akaketi juu yake.
8Daugelis tiesė ant kelio savo drabužius, kiti kirto ir klojo ant kelio medžių šakas.
8Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani; wengine wakatandaza matawi ya miti waliyoyakata mashambani.
9Iš priekio ir iš paskos einantys šaukė: “Osana! Palaimintas, kuris ateina Viešpaties vardu!
9Watu wote waliotangulia na wale waliofuata wakapaaza sauti zao wakisema, "Hosana! Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!
10Palaiminta mūsų tėvo Dovydo karalystė, ateinanti Viešpaties vardu! Osana aukštybėse!”
10Ubarikiwe Ufalme ujao wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni!"
11Taip Jėzus įžengė į Jeruzalę ir į šventyklą. Viską apžiūrėjęs, kadangi buvo jau vakaro valanda,Jis su dvylika išėjo į Betaniją.
11Yesu aliingia mjini Yerusalemu akaenda moja kwa moja mpaka Hekaluni, akatazama kila kitu kwa makini. Lakini kwa vile ilikwisha kuwa jioni, akaenda Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
12Rytojaus dieną, jiems keliaujant iš Betanijos, Jėzus išalko.
12Kesho yake, walipokuwa wanatoka Bethania, Yesu aliona njaa.
13Pamatęs iš tolo sulapojusį figmedį, Jis priėjo pažiūrėti, gal ką ant jo ras. Tačiau, atėjęs prie medžio, Jis nerado nieko, tiktai lapus, nes dar nebuvo figų metas.
13Basi, akaona kwa mbali mtini wenye majani mengi. Akauendea ili aone kama ulikuwa na tunda lolote. Alipoufikia, aliukuta bila tunda lolote ila majani matupu, kwa vile hayakuwa majira ya mtini kuzaa matunda.
14Atsakydamas Jėzus tarė medžiui: “Tegul per amžius niekas nebevalgys tavo vaisiaus!” Jo mokiniai tai girdėjo.
14Hapo akauambia mtini, "Tangu leo hata milele mtu yeyote asile matunda kwako." Nao wanafunzi wake walisikia maneno hayo.
15Jie atėjo į Jeruzalę. Įėjęs į šventyklą, Jėzus ėmė varyti laukan parduodančius ir perkančius šventykloje. Jis išvartė pinigų keitėjų stalus bei karvelių pardavėjų suolus
15Basi, wakafika Yerusalemu. Yesu akaingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza nje watu waliokuwa wanauza na kununua vitu humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilishana fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
16ir neleido nešti prekių per šventyklą.
16Hakumruhusu mtu yeyote kupitia Hekaluni akichukua kitu.
17Jis mokė, sakydamas jiems: “Argi neparašyta: ‘Mano namai vadinsis maldos namai visoms tautoms’? O jūs pavertėte juos ‘plėšikų lindyne’ ”.
17Kisha akawafundisha, "Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote! Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi!"
18Tai išgirdę, aukštieji kunigai ir Rašto žinovai tarėsi, kaip Jį pražudyti. Jie mat bijojo Jėzaus, nes visi žmonės buvo didžiai nustebinti Jo mokymo.
18Makuhani wakuu na walimu wa Sheria waliposikia hayo, walianza kutafuta njia ya kumwangamiza. Lakini walimwogopa kwa sababu umati wa watu ulishangazwa na mafundisho yake.
19Atėjus vakarui, Jėzus su mokiniais išėjo iš miesto.
19Ilipokuwa jioni, Yesu na wanafunzi wake waliondoka mjini.
20Rytą eidami pro šalį, jie pamatė, kad figmedis nudžiūvęs iš pat šaknų.
20Asubuhi na mapema, walipokuwa wanapita, waliuona ule mtini umenyauka wote, hata mizizi.
21Prisiminęs Petras tarė Jėzui: “Rabi, žiūrėk! Figmedis, kurį prakeikei, nudžiūvo!”
21Petro aliukumbuka, akamwambia Yesu, "Mwalimu, tazama! Ule mtini ulioulaani, umenyauka!"
22Jėzus, atsakydamas jiems, tarė: “Turėkite tikėjimą Dievu!
22Yesu akawaambia, "Mwaminini Mungu.
23Iš tiesų sakau jums: kas pasakytų šitam kalnui: ‘Pasikelk ir meskis į jūrą’, ir savo širdyje neabejotų, bet tikėtų, kad įvyks tai, ką sako,jis turės, ką besakytų.
23Nawaambieni kweli, mtu akiuambia mlima huu: Ng'oka ukajitose baharini bila kuona shaka moyoni mwake, ila akaamini kwamba mambo yote anayosema yanafanyika, atafanyiwa jambo hilo.
24Todėl sakau jums: ko tik prašote melsdamiesi, tikėkite, kad gaunate, ir jūs turėsite.
24Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu, aminini kwamba mmekipokea, nanyi mtapewa.
25Kai stovite melsdamiesi, atleiskite, jei turite ką nors prieš kitus, kad ir jūsų Tėvas, kuris danguje, galėtų jums atleisti jūsų nusižengimus.
25Mnaposimama kusali, sameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu.
26Bet jeigu jūs neatleisite, nė jūsų Tėvas, kuris danguje, neatleis jūsų nusižengimų”.
26Lakini msipowasamehe wengine, hata Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu."
27Jie vėl sugrįžo į Jeruzalę. Jam vaikščiojant po šventyklą, prie Jo priėjo aukštųjų kunigų, Rašto žinovų bei vyresniųjų
27Basi, wakafika tena Yerusalemu. Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walimwendea,
28ir klausė: “Kokią teisę turi taip daryti? Kas Tau davė valdžią tai daryti?”
28wakamwuliza, "Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Nani aliyekupa mamlaka ya kufanya mambo haya?"
29Jėzus jiems atsakė: “Aš irgi paklausiu jus vieno dalyko, o jūs atsakykite man, tada ir Aš jums pasakysiu, kokia valdžia tai darau.
29Lakini Yesu akawaambia, "Nitawaulizeni swali moja; mkinijibu, na pia nitawaambieni ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
30Jono krikštas buvo iš dangaus ar iš žmonių? Atsakykite man!”
30Je, mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka mbinguni ama kwa watu? Nijibuni."
31Jie samprotavo tarpusavy: “Jei pasakysimeiš dangaus, Jis mums sakys: ‘Tai kodėl juo netikėjote?’
31Wakaanza kujadiliana, "Tukisema, Yalitoka mbinguni, atatuuliza, Basi, mbona hamkumsadiki?
32O jei pasakysimeiš žmonių...” Jie bijojo minios, nes visi buvo įsitikinę, kad Jonas tikrai buvo pranašas.
32Na tukisema, Yalitoka kwa watu..." (Waliogopa umati wa watu maana wote waliamini kwamba Yohane alikuwa kweli nabii.)
33Todėl jie atsakė Jėzui: “Mes nežinome”. Tada Jėzus tarė: “Tai ir Aš jums nesakysiu, kokia valdžia tai darau”.
33Basi, wakamjibu Yesu, "Sisi hatujui." Naye Yesu akawaambia, "Nami pia sitawaambieni ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."