1Jėzus pradėjo kalbėti jiems palyginimais: “Vienas žmogus pasodino vynuogyną, aptvėrė jį tvora, įrengė spaustuvą, pastatė bokštą, išnuomojo vynininkams ir iškeliavo į tolimą šalį.
1Yesu alianza kusema nao kwa mifano: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu. Akalizungushia ukuta, na katikati yake akachimba kisima cha kusindikia divai, akajenga mnara pia. Akalikodisha shamba hilo kwa wakulima, akasafiri hadi nchi ya mbali.
2Atėjus metui, jis nusiuntė pas vynininkus tarną atsiimti iš vynininkų savo vaisių.
2Wakati wa mavuno, alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima akamletee sehemu ya mazao ya shamba lake.
3Tie pačiupo jį, sumušė ir paleido tuščiomis.
3Wale wakulima wakamkamata, wakampiga, wakamrudisha mikono mitupu.
4Tada jis vėl nusiuntė pas juos kitą tarną, o tie, apmėtę akmenimis, sužeidė jį į galvą ir išniekinę paleido.
4Akatuma tena mtumishi mwingine; huyu wakamuumiza kichwa na kumtendea vibaya.
5Jis pasiuntė dar vieną, bet tą jie nužudė; ir dar daugelį kitų tarnų, kurių vienus jie primušė, kitus nužudė.
5Mwenye shamba akatuma mtumishi mwingine tena, na huyo wakamuua. Wengine wengi waliotumwa, baadhi yao walipigwa, na wengi wakauawa.
6Dar vieną turėjomylimąjį sūnų. Jį nusiuntė pas juos paskutinį, sakydamas sau: ‘Jie gerbs mano sūnų’.
6Alibakiwa bado na mtu mmoja, yaani mwanawe mpendwa. Mwishowe akamtuma huyo akisema, Watamheshimu mwanangu.
7Bet vynininkai tarėsi: ‘Tai paveldėtojas. Eikime, užmuškime jį, ir jo palikimas bus mūsų’.
7Lakini hao wakulima wakaambiana, Huyu ndiye mrithi, basi, tumuue ili urithi wake uwe wetu!
8Nutvėrę nužudė jį ir išmetė laukan iš vynuogyno.
8Kwa hiyo wakamkamata, wakamuua na kumtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
9Ką tada darys vynuogyno šeimininkas? Jis ateis, nužudys vynininkus ir atiduos vynuogyną kitiems.
9"Basi, mwenye shamba atafanya nini? Atakuja kuwaangamiza hao wakulima na kulikodisha hilo shamba la mizabibu kwa watu wengine.
10Ar neskaitėte, kas parašyta Raštuose: ‘Akmuo, kurį statytojai atmetė, tapo kertiniu akmeniu.
10Je, hamjasoma Maandiko haya? Jiwe walilokataa waashi sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
11Tai Viešpaties padaryta ir nuostabu mūsų akyse’?”
11Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu sana kwetu."
12Anie norėjo Jį suimti, tačiau bijojo minios. Mat suprato, kad palyginimas buvo jiems taikomas. Tad, palikę Jį, pasitraukė.
12Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na wazee walifahamu ya kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu. Kwa hiyo walijaribu kumtia nguvuni, lakini waliogopa umati wa watu. Basi, wakamwacha wakaenda zao.
13Tada jie siunčia pas Jėzų fariziejų ir erodininkų sugauti Jo kalboje.
13Basi, baadhi ya Mafarisayo na wafuasi wa kikundi cha Herode walitumwa ili wamtege Yesu kwa maneno yake.
14Šitie atėję sako Jam: “Mokytojau, žinome, jog Tu esi tiesus ir niekam nepataikauji. Tu neatsižvelgi į asmenis ir mokai Dievo kelio, kaip reikalauja tiesa. Ar reikia mokėti ciesoriui mokesčius, ar ne?
14Wakamwendea, wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwaminifu unayesema ukweli mtupu, wala humjali mtu yeyote. Wala cheo cha mtu si kitu kwako, lakini wafundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la? Tulipe au tusilipe?"
15Mokėti ar nemokėti?” Žinodamas jų veidmainystę, Jis tarė: “Kam spendžiate man pinkles? Atneškite man pažiūrėti denarą”.
15Lakini Yesu alijua unafiki wao, akawaambia, "Mbona mnanijaribu? Nionyesheni sarafu."
16Jie padavė. Jis jų klausia: “Kieno čia atvaizdas ir įrašas?” Jie atsakė: “Ciesoriaus”.
16Wakamwonyesha. Naye akawauliza, "Sura na chapa hii ni ya nani?" Wakamjibu, "Ni ya Kaisari."
17Tuomet Jėzus jiems tarė: “Kas ciesoriaus, atiduokite ciesoriui, o kas DievoDievui”. Ir jie labai Juo stebėjosi.
17Basi, Yesu akawaambia, "Mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari na Mungu yaliyo yake Mungu." Wakashangazwa sana naye.
18Pas Jėzų ateina sadukiejų, kurie neigia mirusiųjų prisikėlimą, ir klausia:
18Masadukayo wasemao kwamba hakuna ufufuo walimwendea Yesu, wakamwuliza,
19“Mokytojau, Mozė mums parašė: ‘Jei kieno brolis mirtų ir paliktų žmoną, o nepaliktų vaikų, tuomet jo brolis tegul veda našlę ir pažadina savo broliui palikuonių’.
19"Mwalimu, Mose alituagiza hivi: Mtu akifa na kuacha mke bila mtoto, ndugu yake lazima amchukue huyo mama mjane amzalie watoto ndugu yake marehemu.
20Ir štai buvo septyni broliai. Pirmasis vedė žmoną ir mirdamas nepaliko vaikų.
20Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto.
21Vedė ją antrasis, bet ir šis mirė bevaikis. Taip atsitiko ir su trečiuoju,
21Ndugu wa pili akamwoa huyo mjane, naye pia akafa bila kuacha mtoto; na ndugu watatu hali kadhalika.
22ir visi septyni nepaliko vaikų. Po jų visų numirė ir ta moteris.
22Wote saba walikufa bila kuacha mtoto. Mwishowe yule mama mjane naye akafa.
23Taigi prisikėlime, kai jie prisikels, kurio iš jų žmona ji bus? Juk ji buvo visų septynių žmona”.
23Basi, siku watu watakapofufuka, mama huyo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa."
24Jėzus jiems atsakė: “Argi ne todėl klystate, kad nepažįstate nei Raštų, nei Dievo jėgos?
24Yesu akawaambia, "Ninyi mmekosea sana, kwa sababu hamjui Maandiko Matakatifu wala nguvu ya Mungu.
25Kai prisikels iš numirusiųjų, jie nei ves, nei tekės, bet bus kaip angelai danguje.
25Maana wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa; watakuwa kama malaika wa mbinguni.
26O kad mirusieji keliasi,ar neskaitėte Mozės knygoje, kaip Mozei Dievas pasakė iš krūmo: ‘Aš esu Abraomo Dievas, Izaoko Dievas ir Jokūbo Dievas!’?
26Lakini kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamjasoma kitabu cha Mose katika sehemu inayohusu kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto? Mungu alimwambia Mose, Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.
27Jis nėra mirusiųjų Dievas, bet gyvųjų Dievas. Taigi jūs labai klystate”.
27Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Ninyi mmekosea sana!"
28Vienas iš Rašto žinovų, girdėjęs juos besiginčijant ir supratęs, kaip puikiai Jėzus jiems atsakinėjo, priėjo ir paklausė Jį: “Koks yra visų pirmasis įsakymas?”
28Mmojawapo wa walimu wa Sheria alifika, akasikia mabishano yao. Alipoona kwamba Yesu aliwajibu vyema, akajitokeza akamwuliza, "Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?"
29Jėzus jam atsakė: “Pirmasis yra šis: ‘Klausyk, Izraeli,Viešpats, mūsų Dievas, yra vienintelis Viešpats;
29Yesu akamjibu, "Ya kwanza ndiyo hii: Sikiliza, Israeli! Bwana Mungu wetu ndiye peke yake Bwana.
30tad mylėk Viešpatį, savo Dievą, visa savo širdimi, visa savo siela, visu savo protu ir visomis savo jėgomis’,tai pirmasis įsakymas.
30Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.
31Antrasis panašus į jį: ‘Mylėk savo artimą kaip save patį’. Nėra jokio kito įsakymo, didesnio už šiuodu”.
31Na ya pili ndiyo hii: Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi."
32Tada Rašto žinovas Jam atsakė: “Gerai, Mokytojau, Tu tiesą pasakei: yra vienas Dievas ir nėra kito, tik Jis;
32Basi, yule mwalimu wa Sheria akamwambia, "Vyema Mwalimu! Umesema kweli kwamba Mungu ni mmoja tu wala hakuna mwingine ila yeye.
33o mylėti Jį visa širdimi, visu protu ir visomis jėgomis bei mylėti savo artimą kaip save patį yra daugiau negu visos deginamosios atnašos ir aukos”.
33Na ni lazima mtu kumpenda Mungu kwa moyo wote, kwa akili yote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani yake kama anavyojipenda mwenyewe. Jambo hili ni muhimu zaidi kuliko dhabihu na sadaka zote za kuteketezwa."
34Matydamas, kaip išmintingai jis atsakė, Jėzus jam tarė: “Tu netoli nuo Dievo karalystės!” Ir niekas daugiau nebedrįso Jo klausti.
34Yesu alipoona kwamba huyu mtu alimjibu kwa ujasiri, akamwambia, "Wewe huko mbali na Ufalme wa Mungu." Baada ya hayo, hakuna mtu aliyethubutu tena kumwuliza kitu.
35Mokydamas šventykloje, Jėzus kalbėjo: “Kaip Rašto žinovai gali sakyti, jog Kristus yra Dovydo Sūnus?
35Wakati Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, aliuliza, "Mbona walimu wa Sheria wanasema ya kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
36Juk pats Dovydas Šventąja Dvasia pasakė: ‘Viešpats tarė mano Viešpačiui: sėskis mano dešinėje, kol patiesiu Tavo priešus tarsi pakojį po Tavo kojų’.
36Daudi mwenyewe akiongozwa na Roho Mtakatifu alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia, Mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako."
37Pats Dovydas vadina jį Viešpačiu, tai kaip Jis gali būti jo Sūnus?” Didelė minia džiugiai Jo klausėsi.
37"Daudi mwenyewe anamwita Kristo Bwana. Basi, Kristo atakuwaje mwanae?" Umati wa watu ulikuwa ukimsikiliza kwa furaha.
38Mokydamas Jis kalbėjo: “Saugokitės Rašto žinovų, kurie mėgsta vaikščioti su ilgais drabužiais ir būti sveikinami aikštėse,
38Katika mafundisho yake, Yesu alisema, "Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamejivalia kanzu ndefu na kusalimiwa na watu kwa heshima sokoni; hupenda kuketi mahali pa heshima katika masunagogi,
39užimti pirmuosius krėslus sinagogose ir garbingas vietas pokyliuose.
39na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
40Jie suryja našlių namus ir dedasi kalbą ilgas maldas. Jie gaus dar didesnį pasmerkimą”.
40Huwanyonya wajane huku wakijisingizia kusali sala ndefu. Siku ya hukumu watapata adhabu kali!"
41Atsisėdęs ties iždine, Jėzus stebėjo, kaip žmonės metė į ją pinigus. Daugelis turtingųjų aukojo gausiai.
41Yesu alikuwa ameketi karibu na sanduku la hazina. Akawa anatazama jinsi watu wengi walivyokuwa wakitoa fedha na kuzitia katika hazina ya Hekalu. Matajiri wengi walitoa fedha nyingi.
42Atėjo viena beturtė našlė ir įmetė du pinigėlius, tai yra skatiką.
42Hapo akaja mama mmoja mjane maskini, akatoa sarafu mbili ndogo za fedha.
43Pasišaukęs savo mokinius, Jėzus tarė jiems: “Iš tiesų sakau jums: ši beturtė našlė įmetė daugiausia iš visų, kurie dėjo į iždinę.
43Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, "Kweli nawaambieni, huyu mama mjane maskini ametoa zaidi kuliko wengine wote waliotia fedha katika sanduku la hazina.
44Visi aukojo iš savo pertekliaus, o ji iš savo nepritekliaus įmetė visa, ką turėjo, visą savo pragyvenimą”.
44Maana wote walitoa kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa yote aliyokuwa nayo, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi."