1Jie priplaukė ežero krantą gadariečių krašte.
1Basi, wakafika katika nchi ya Wagerase, ng'ambo ya ziwa.
2Jam išlipus iš valties, tuojau prieš Jį iš kapinių atbėgo vyras, turintis netyrąją dvasią.
2Mara tu Yesu aliposhuka mashuani, mtu mmoja aliyepagawa na pepo mchafu alitoka makaburini, akakutana naye.
3Jis gyveno kapų rūsiuose, ir niekas negalėjo nė grandinėmis jo surakinti.
3Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.
4Nors jis jau daug kartų buvo pančiojamas ir grandinėmis rakinamas, bet sutrupindavo grandines, nutraukydavo pančius, ir niekas negalėdavo jo suvaldyti.
4Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.
5Per kiauras naktis ir dienas jis bastydavosi po kalnus ir kapines, klykdamas ir daužydamas save akmenimis.
5Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.
6Iš tolo pamatęs Jėzų, atbėgo, parpuolė prieš Jį
6Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akamwinamia
7ir ėmė garsiai šaukti: “Ko Tau reikia iš manęs, Jėzau, aukščiausiojo Dievo Sūnau? Saikdinu tave Dievu, nekankink manęs!”
7akisema kwa sauti kubwa, "Una shauri gani nami, wewe Yesu Mwana wa Mungu aliye juu? Kwa jina la Mungu, nakusihi usinitese!"
8Jėzus mat buvo paliepęs: “Išeik, netyroji dvasia, iš žmogaus!”
8(Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, "Pepo mchafu, mtoke mtu huyu.")
9Jėzus dar paklausė: “O kaip tu vadiniesi?” Ji atsakė: “Mano vardasLegionas, nes mūsų daug”.
9Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Naye akajibu, "Jina langu ni Jeshi, maana sisi tu wengi."
10Ir pradėjo labai prašytis nevaryti jų iš to krašto.
10Kisha akamsihi Yesu asiwafukuze hao pepo katika nchi ile.
11Ten pat, atkalnėje, ganėsi didžiulė kiaulių banda.
11Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe malishoni kwenye mteremko wa mlima.
12Visi demonai maldavo Jį, sakydami: “Pasiųsk mus į tas kiaules, kad į jas sueitume!”
12Basi, hao pepo wakamsihi, "Utupeleke kwa hao nguruwe, tuwaingie."
13Jėzus iškart jiems leido. Išėjusios netyrosios dvasios apniko kiaules, ir visa banda, apie du tūkstančius kiaulių, metėsi nuo skardžio į ežerą ir prigėrė.
13Naye akawaruhusu. Basi, hao pepo wachafu wakatoka, wakawaingia wale nguruwe. Kundi lote la nguruwe wapatao elfu mbili likaporomoka kwenye ule mteremko mkali mpaka ziwani, likatumbukia majini.
14Tie, kurie jas ganė, išbėgiojo ir pranešė apie įvykį mieste ir kaimuose. Žmonės išėjo pažiūrėti, kas atsitiko.
14Wachungaji wa hao nguruwe walikimbia, wakatangaza jambo hilo mjini na mashambani. Watu wakafika kuona yaliyotukia.
15Atėję prie Jėzaus, pamatė sėdintį demonų apsėstąjįtą, kuriame buvo Legionas,apsirengusį ir sveiko proto, ir juos apėmė baimė.
15Wakamwendea Yesu, wakamwona na mtu yuleyule aliyekuwa amepagawa na jeshi la pepo ameketi chini, amevaa nguo na ana akili yake sawa, wakaogopa.
16Mačiusieji papasakojo jiems, kas nutiko su apsėstuoju, ir apie kiaules.
16Watu walishuhudia tukio hilo wakaeleza wengine mambo yaliyompata huyo mtu aliyekuwa amepagawa na pepo na juu ya wale nguruwe.
17Tada žmonės ėmė Jėzų maldauti, kad Jis pasišalintų iš jų krašto.
17Basi, wakaanza kumwomba aondoke katika nchi yao.
18Jėzui lipant į valtį, buvęs demonų apsėstasis prašė leisti pasilikti su Juo,
18Yesu alipokuwa anapanda mashuani, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo akamwomba amruhusu kwenda naye.
19bet Jėzus nesutiko ir pasakė: “Eik namo pas saviškius ir papasakok, kokių didžių dalykų Viešpats tau padarė ir kaip tavęs pasigailėjo”.
19Lakini Yesu akamkatalia. Badala yake akamwambia, "Nenda nyumbani kwa jamaa yako, ukawaambie mambo yote Bwana aliyokutendea na jinsi alivyokuonea huruma."
20Tada jis nuėjo savo keliu ir Dekapolyje ėmė skelbti, kokių didžių dalykų Jėzus jam padarė, ir visi stebėjosi.
20Basi, huyo mtu akaenda, akaanza kutangaza huko Dekapoli mambo yote Yesu aliyomtendea; watu wote wakashangaa.
21Jėzui vėl persikėlus valtimi į kitą pusę, prie Jo susirinko didžiulė minia, ir Jis buvo paežerėje.
21Yesu alivukia tena upande wa pili wa ziwa kwa mashua. Umati mkubwa wa watu ukakusanyika mbele yake, naye akawa amesimama kando ya ziwa.
22Štai ateina vienas iš sinagogos vyresniųjų, vardu Jayras, ir, pamatęs Jį, puola Jam po kojų,
22Hapo akaja mmojawapo wa maofisa wa sunagogi, jina lake Yairo. Alipomwona Yesu, akajitupa mbele ya miguu yake,
23karštai maldaudamas: “Mano dukrelė miršta! Ateik ir uždėk ant jos rankas, kad pagytų ir gyventų”.
23akamsihi akisema, "Binti yangu mdogo ni mgonjwa karibu kufa. Twende tafadhali, ukamwekee mikono yako, apate kupona na kuishi."
24Jėzus nuėjo su juo. Paskui Jį sekė didžiulė minia ir Jį spauste spaudė.
24Basi, Yesu akaondoka pamoja naye. Watu wengi sana wakamfuata, wakawa wanamsonga kila upande.
25Ten buvo viena moteris, dvylika metų serganti kraujoplūdžiu.
25Mmojawapo alikuwa mwanamke mwenye ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili.
26Nemaža iškentėjusi nuo daugelio gydytojų ir išleidusi visa, ką turėjo, ji nė kiek nepasitaisė, bet ėjo vis blogyn.
26Mwanamke huyo alikuwa amekwisha sumbuka sana kuwaendea waganga wengi. Na ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote, hakupata nafuu bali hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27Išgirdusi apie Jėzų, ji prasispraudė iš minios galo ir prisilietė prie Jo apsiausto.
27Alikuwa amesikia habari za Yesu, na hivyo akaupenya msongamano wa watu kutoka nyuma, akagusa vazi lake.
28Mat ji kalbėjo: “Jeigu paliesiu bent Jo drabužįišgysiu!”
28Alifanya hivyo, maana alijisemea, "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
29Tuojau kraujas nustojo jai plūdęs, ir ji pajuto kūnu, kad yra pasveikusi nuo savo ligos.
29Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, akajisikia mwilini mwake kwamba ameponywa ugonjwa wake.
30Ir Jėzus iš karto pajuto, kad iš Jo išėjo jėga, ir, atsigręžęs į minią, paklausė: “Kas prisilietė prie mano apsiausto?”
30Yesu alitambua mara kwamba nguvu imemtoka. Basi akaugeukia ule umati wa watu, akauliza, "Nani aliyegusa mavazi yangu?"
31Jo mokiniai Jam atsakė: “Matai, kaip minia Tave spaudžia, o Tu klausi: ‘Kas mane palietė?’ ”
31Wanafunzi wake wakamjibu, "Unaona jinsi watu wanavyokusonga; mbona wauliza nani aliyekugusa?"
32Bet Jis dairėsi tos, kuri taip buvo padariusi.
32Lakini Yesu akaendelea kutazama amwone huyo aliyefanya hivyo.
33Moteris išėjo į priekį išsigandusi ir virpėdama, nes žinojo, kas jai atsitiko, ir, puolusi prieš Jį, papasakojo visą tiesą.
33Hapo huyo mwanamke, akifahamu yaliyompata, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa chini mbele ya Yesu na kusema ukweli wote.
34O Jis tarė jai: “Dukra, tavo tikėjimas išgydė tave, eik rami ir būk sveika nuo savo ligos”.
34Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako."
35Jam dar tebekalbant, atėjo sinagogos vyresniojo žmonės ir pranešė: “Tavo duktė numirė, kam dar vargini Mokytoją?”
35Yesu alipokuwa bado anaongea, watu walifika kutoka nyumbani kwa yule ofisa wa sunagogi, wakamwambia, "Binti yako amekwisha kufa. Ya nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?"
36Išgirdęs tuos žodžius, Jėzus tarė sinagogos vyresniajam: “Nebijok, vien tik tikėk!”
36Lakini, bila kujali walichosema, Yesu akamwambia mkuu wa sunagogi, "Usiogope, amini tu."
37Ir Jis niekam neleido eiti kartu, išskyrus Petrą, Jokūbą ir Jokūbo brolį Joną.
37Wala hakumruhusu mtu yeyote kufuatana naye ila Petro, Yakobo na Yohane nduguye Yakobo.
38Atėjęs į sinagogos vyresniojo namus, Jėzus pamatė sujudimą ir garsiai verkiančius bei raudančius.
38Wakafika nyumbani kwa ofisa wa sunagogi naye Yesu akasikia makelele, kilio na maombolezo mengi.
39Įžengęs vidun, Jis tarė: “Kam tas triukšmas ir verksmas?! Vaikas nėra miręs, o miega”.
39Akaingia ndani, akawaambia, "Mbona mnapiga kelele na kulia? Msichana hakufa, amelala tu."
40Žmonės šaipėsi iš Jo. Tada, išvaręs juos visus, Jis pasiėmė vaiko tėvą ir motiną, taip pat savo palydovus ir įėjo ten, kur vaikas gulėjo.
40Lakini wao wakamcheka. Basi, akawaondoa wote nje, akawachukua baba na mama ya huyo msichana na wale wanafunzi wake, wakaingia chumbani alimokuwa huyo msichana.
41Paėmęs mergaitę už rankos, pasakė jai: “Talitį kum”; išvertus reiškia: “Mergaite, sakau tau, kelkis!”
41Kisha akamshika mkono, akamwambia, "Talitha, kumi," maana yake, "Msichana, nakwambia, amka!"
42Mergaitė tuojau atsikėlė ir ėmė vaikščioti. Jai buvo dvylika metų. Jie nustėro iš nuostabos.
42Mara msichana akasimama, akaanza kutembea. (Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.) Hapo watu wakashangaa kupita kiasi.
43Jis griežtai įsakė, kad niekas to nežinotų, ir liepė duoti mergaitei valgyti.
43Yesu akawakataza sana wasimjulishe mtu jambo hilo. Kisha akawaambia wampe huyo msichana chakula.