1Anomis dienomis, susirinkus gausiai miniai ir žmonėms neturint ko valgyti, Jėzus, pasišaukęs savo mokinius, tarė:
1Wakati huo umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena, na hawakuwa na chakula. Basi, Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia,
2“Gaila man minios! Jau trys dienos žmonės yra su manimi ir neturi ko valgyti.
2"Nawahurumia watu hawa kwa sababu wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu, wala hawana chakula.
3Jei paleisiu juos namo alkanus, jie nusilps kelyje, nes kai kurie yra atėję iš toli”.
3Nikiwaacha waende nyumbani wakiwa na njaa watazimia njiani, maana baadhi yao wametoka mbali."
4Mokiniai Jam atsakė: “Iš kur dykumoje gauti duonos jiems pavalgydinti?”
4Wanafunzi wake wakamwuliza, "Hapa nyikani itapatikana wapi mikate ya kuwashibisha watu hawa wote?"
5Jėzus paklausė: “Kiek kepalų turite?” Jie atsakė: “Septynis”.
5Yesu akawauliza, "Mnayo mikate mingapi?" Nao wakamjibu, "Saba."
6Tada Jis liepė žmonėms susėsti ant žemės. Paėmęs septynis kepalus, palaimino, laužė ir davė mokiniams dalyti, ir tie padalijo miniai.
6Basi, akawaamuru watu wakae chini. Akaitwaa ile mikate saba, akamshukuru Mungu, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu, nao wakawagawia.
7Jie dar turėjo kelias žuveles. Jis palaimino jas ir taip pat liepė dalyti.
7Walikuwa pia na visamaki vichache. Yesu akavibariki, akaamuru vigawiwe watu vilevile.
8Žmonės pavalgė iki soties, ir jie surinko dar septynias pintines likučių.
8Watu wakala, wakashiba. Wakaokota mabaki yaliyosalia wakajaza makapu saba.
9O valgytojų buvo apie keturis tūkstančius. Jėzus paleido juos
9Nao waliokula walikuwa watu wapatao elfu nne. Yesu akawaaga,
10ir tuojau, įsėdęs su mokiniais į valtį, nuplaukė į Dalmanutos sritį.
10na mara akapanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda wilaya ya Dalmanutha.
11Čia priėjo fariziejų ir pradėjo su Juo ginčytis. Mėgindami Jį, jie reikalavo ženklo iš dangaus.
11Mafarisayo walikuja, wakaanza kujadiliana na Yesu. Kwa kumjaribu, wakamtaka awafanyie ishara kuonyesha anayo idhini kutoka mbinguni.
12Atsidusęs iš dvasios gilumos, Jis tarė: “Ir kam šita karta reikalauja ženklo? Iš tiesų sakau jums: ženklo šiai kartai nebus duota!”
12Yesu akahuzunika rohoni, akasema, "Mbona kizazi hiki kinataka ishara? Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakitapewa ishara yoyote!"
13Ir, palikęs juos, Jis vėl sėdo į valtį ir nuplaukė į kitą krantą.
13Basi, akawaacha, akapanda tena mashua, akaanza safari kwenda ng'ambo ya pili ya ziwa.
14Mokiniai buvo pamiršę pasiimti duonos. Jie teturėjo su savim valtyje vieną kepalą.
14Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate; walikuwa na mkate mmoja tu katika mashua.
15Jėzus juos įspėjo: “Žiūrėkite, saugokitės fariziejų raugo ir Erodo raugo”.
15Yesu akawaonya, "Angalieni sana! Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode."
16Jie svarstė tarpusavy, sakydami: “Tai todėl, kad nepasiėmėme duonos”.
16Wanafunzi wakaanza kujadiliana wao kwa wao, "Anasema hivyo kwa kuwa hatuna mikate."
17Tai supratęs, Jėzus tarė: “Kam jūs tariatės neturį duonos? Argi vis dar neišmanote ir nesuprantate ir jūsų širdys vis dar užkietėjusios?
17Yesu alitambua hayo, akawaambia, "Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate? Je, bado hamjafahamu, wala hamjaelewa? Je, mioyo yenu imeshupaa?
18Turite akis, ir nematote; turite ausis, ir negirdite? Argi neatsimenate,
18Je, Mnayo macho na hamwoni? Mnayo masikio na hamsikii? Je, hamkumbuki
19jog penkis kepalus Aš sulaužiau penkiems tūkstančiams? O kiek pilnų pintinių trupinių pririnkote?” Jie atsakė: “Dvylika”.
19wakati ule nilipoimega ile mikate mitano na kuwapa watu elfu tano? Mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki ya makombo?" Wakamjibu, "Kumi na viwili."
20“O kai septynis kepalus sulaužiau keturiems tūkstančiams, kiek pilnų pintinių trupinių pririnkote?” Jie atsakė: “Septynias”.
20"Na nilipoimega ile mikate saba na kuwapa watu elfu nne, mlikusanya makapu mangapi ya makombo?" Wakamjibu, "Saba."
21Tada Jis tarė: “Tai kaipgi vis dar nesuprantate?!”
21Basi, akawaambia, "Na bado hamjaelewa?"
22Jie ateina į Betsaidą. Ten atveda pas Jėzų neregį ir prašo jį palytėti.
22Yesu alifika Bethsaida pamoja na wanafunzi wake. Huko watu wakamletea kipofu mmoja, wakamwomba amguse.
23Jis paėmė neregį už rankos ir nusivedė už kaimo. Ten spjovė jam į akis, uždėjo ant jo rankas ir paklausė: “Ar ką nors matai?”
23Yesu akamshika mkono huyo kipofu, akampeleka nje ya kijiji. Akamtemea mate machoni, akamwekea mikono, akamwuliza, "Je, unaweza kuona kitu?"
24Šis apsižvalgęs tarė: “Regiu žmones. Lyg kokius medžius matau juos vaikščiojančius”.
24Huyo kipofu akatazama, akasema, "Ninawaona watu wanaoonekana kama miti inayotembea."
25Jis vėl rankomis palietė jo akis ir liepė apsižvalgyti. Ir šis tapo sveikas ir viską aiškiai matė.
25Kisha Yesu akamwekea tena mikono machoni, naye akakaza macho, uwezo wake wa kuona ukamrudia, akaona kila kitu sawasawa.
26Jėzus išsiuntė jį namo, sakydamas: “Neužeik į kaimą ir niekam ten nepasakok!”
26Yesu akamwambia aende zake nyumbani na kumwamuru, "Usirudi kijijini!"
27Jėzus su savo mokiniais išėjo į Pilypo Cezarėjos kaimus. Kelyje klausė mokinius: “Kuo mane žmonės laiko?”
27Kisha Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika vijiji vya Kaisarea Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu aliwauliza wanafunzi wake, "Watu wanasema mimi ni nani?"
28Jie atsakė: “VieniJonu Krikštytoju, kitiEliju, tretivienu iš pranašų”.
28Wakamjibu, "Wengine wanasema wewe ni Yohane Mbatizaji, wengine Eliya na wengine mmojawapo wa manabii."
29Tada Jis paklausė: “O jūs kuo mane laikote?” Petras Jam atsakė: “Tu esi Kristus”.
29Naye akawauliza, "Na ninyi je, mnasema mimi ni nani?" Petro akamjibu, "Wewe ndiwe Kristo."
30Tada Jėzus griežtai įsakė niekam apie Jį nekalbėti.
30Kisha Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
31Jis pradėjo juos mokyti, jog Žmogaus Sūnus turės daug iškentėti, būti vyresniųjų, aukštųjų kunigų bei Rašto žinovų atmestas, nužudytas ir po trijų dienų prisikelti.
31Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake: "Ni lazima Mwana wa Mtu apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Atauawa na baada ya siku tatu atafufuka."
32Jis tai kalbėjo visiškai atvirai. Tada Petras, pasivadinęs Jį į šalį, ėmė Jį drausti.
32Yesu aliwaambia jambo hilo waziwazi. Basi, Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea.
33Jėzus atsigręžęs pažiūrėjo į mokinius ir sudraudė Petrą: “Eik šalin, šėtone, nes tu mąstai ne apie tai, kas Dievo, o kas žmonių!”
33Lakini Yesu akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro akisema, "Ondoka mbele yangu, Shetani! Fikira zako si za kimungu ila ni za kibinadamu!"
34Pasišaukęs minią ir savo mokinius, Jėzus prabilo: “Jei kas nori eiti paskui mane, teišsižada pats savęs, teima savo kryžių ir teseka manimi.
34Kisha akauita umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
35Kas nori išgelbėti savo gyvybę, tas ją praras; o kas praras savo gyvybę dėl manęs ir dėl Evangelijos, tas ją išgelbės.
35Maana mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza, lakini mtu atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema, atayaokoa.
36Kokia gi žmogui nauda, jeigu jis laimėtų visą pasaulį, o pakenktų savo sielai?
36Je, kuna faida gani mtu kuupata ulimwengu wote na kuyapoteza maisha yake?
37Arba kuo žmogus galėtų išsipirkti savo sielą?!
37Ama mtu atatoa kitu gani badala ya maisha yake?
38Jei kas gėdisi manęs ir mano žodžių šios svetimaujančios ir nuodėmingos kartos akivaizdoje, to gėdysis ir Žmogaus Sūnus, kai Jis ateis savo Tėvo šlovėje su šventaisiais angelais”.
38Mtu yeyote katika kizazi hiki kiovu na kisichomjali Mungu anayenionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu."