Lithuanian

Swahili: New Testament

Mark

9

1Jis jiems kalbėjo: “Iš tiesų sakau jums: tarp čia stovinčių yra tokių, kurie neragaus mirties, kol išvys Dievo karalystę, ateinančią su galybe”.
1Yesu akaendelea kuwaambia, "Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi."
2Po šešių dienų Jėzus pasiėmė Petrą, Jokūbą ir Joną ir užsivedė juos vienus nuošaliai į aukštą kalną. Ten Jis atsimainė jų akivaizdoje.
2Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
3Jo drabužiai pradėjo spindėti tarsi sniegas, kaip jų išbalinti negalėtų joks skalbėjas žemėje.
3mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
4Jiems pasirodė Elijas ir Mozė, ir jie kalbėjosi su Jėzumi.
4Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
5Petras tarė Jėzui: “Rabi, gera mums čia būti. Pastatykime tris palapines: vieną Tau, kitą Mozei, trečią Elijui”.
5Petro akamwambia Yesu, "Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
6Jis nežinojo, ką sakyti, nes jie buvo labai persigandę.
6Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
7Užėjo debesis ir uždengė juos, o iš debesies nuskambėjo balsas: “Šitas yra mano mylimasis Sūnus. Jo klausykite!”
7Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, "Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni."
8Ir tuojau apsižvalgę, jie nieko prie savęs nebematė, tik vieną Jėzų.
8Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
9Besileidžiant nuo kalno, Jėzus liepė niekam nepasakoti, ką jie matė, kol Žmogaus Sūnus neprisikels iš numirusių.
9Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
10Jie įsidėmėjo šį pasakymą ir svarstė, ką reiškia “prisikelti iš numirusių”.
10Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
11Jie klausė Jį: “Kodėl Rašto žinovai sako, jog pirmiau turįs ateiti Elijas?”
11Wakamwuliza Yesu, "Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?"
12Jėzus jiems atsakė: “Tikrai, Elijas ateina pirmas ir viską atstato. Bet kaipgi parašyta apie Žmogaus Sūnų, jog Jis daug iškentėsiąs ir būsiąs paniekintas?
12Naye akawajibu, "Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
13Todėl sakau jums: Elijas buvo atėjęs, ir jie pasielgė su juo kaip norėjo­taip, kaip apie jį parašyta”.
13Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake."
14Sugrįžęs pas mokinius, Jis pamatė apie juos susirinkusią didelę minią ir besiginčijančius su jais Rašto žinovus.
14Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
15Vos pastebėjusi Jėzų, minia labai nustebo, ir visi bėgo Jį pasveikinti.
15Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
16Jis paklausė Rašto žinovų: “Apie ką ginčijatės su jais?”
16Yesu akawauliza, "Mnajadiliana nini nao?"
17Vienas iš minios Jam atsakė: “Mokytojau, aš atvedžiau pas Tave savo sūnų, kuris turi nebylę dvasią.
17Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, "Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
18Kur tik sugriebusi, dvasia jį tąso, iš burnos jam eina putos, jis griežia dantimis ir pastyra. Aš prašiau Tavo mokinius išvaryti dvasią, bet jie nepajėgė”.
18Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza."
19Tada Jėzus tarė: “O netikinti karta! Kiek dar man reikės su jumis būti? Kaip ilgai jus kęsti? Atveskite jį pas mane!”
19Yesu akawaambia, "Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu."
20Jie atvedė. Vos Jį pamačiusi, dvasia pradėjo tąsyti berniuką; šis parpuolė ant žemės ir apsiputojęs raičiojosi.
20Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
21Jėzus paklausė tėvą: “Ar seniai jam taip darosi?” Šis atsakė: “Nuo pat vaikystės.
21"Amepatwa na mambo hayo tangu lini?" Naye akamjibu, "Tangu utoto wake.
22Dvasia dažnai įstumdavo jį į vandenį ir į ugnį, norėdama nužudyti. Bet, jei ką gali padaryti, pasigailėk mūsų ir padėk mums!”
22Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!"
23Jėzus jam atsakė: “Jei gali tikėti, viskas įmanoma tikinčiam!”
23Yesu akamwambia, "Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani."
24Tučtuojau vaiko tėvas verkdamas sušuko: “Tikiu, Viešpatie! Padėk mano netikėjimui!”
24Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, "Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!"
25Matydamas susibėgančią minią, Jėzus sudraudė netyrąją dvasią, sakydamas jai: “Nebyle ir kurčia dvasia, įsakau tau, išeik iš jo ir daugiau nebegrįžk!”
25Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, "Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!"
26Dvasia, klykdama ir smarkiai jį purtydama, išėjo. O jis liko tarsi negyvas, ir daugelis sakė: “Jis mirė”.
26Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, "Amekufa!"
27Bet Jėzus paėmė jį už rankos, pakėlė, ir šis atsistojo.
27Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28Kai Jis sugrįžo namo, mokiniai, pasilikę su Juo vieni, klausė: “Kodėl mes negalėjome jos išvaryti?”
28Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?"
29Jis atsakė: “Ta veislė neišvaroma nieku kitu, tik malda ir pasninku”.
29Naye akawaambia, "Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu."
30Iš ten išėję, jie keliavo per Galilėją. Jėzus nenorėjo, kad kas apie tai žinotų.
30Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
31Mokydamas savo mokinius, Jis sakė jiems: “Žmogaus Sūnus bus atiduotas į žmonių rankas, ir jie nužudys Jį. Nužudytas Jis po trijų dienų prisikels”.
31kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka."
32Mokiniai nesuprato tų žodžių, bet bijojo Jį klausti.
32Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
33Jie atėjo į Kafarnaumą. Namie Jėzus juos paklausė: “Apie ką kalbėjotės kelyje?”
33Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, "Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?"
34Jie tylėjo. Mat kelyje jie ginčijosi, kuris iš jų didžiausias.
34Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
35Atsisėdęs Jis pasišaukė dvylika ir tarė: “Jei kas trokšta būti pirmas, tebūnie paskutinis ir visų tarnas!”
35Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, "Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote."
36Paėmęs mažą vaiką, pastatė tarp jų ir, apsikabinęs jį, pasakė jiems:
36Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
37“Kas priima tokį vaiką mano vardu, tas priima mane, o kas priima mane, tas ne mane priima, bet Tą, kuris mane siuntė”.
37"Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma."
38Jonas Jam tarė: “Mokytojau, mes matėme vieną, kuris nevaikščioja su mumis, bet Tavo vardu išvarinėja demonus. Mes jam draudėme, nes jis mūsų neseka”.
38Yohane akamwambia, "Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
39Jėzus atsakė: “Nedrauskite jam! Nėra tokio, kuris mano vardu darytų stebuklus ir galėtų čia pat blogai apie mane kalbėti.
39Lakini Yesu akasema, "Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
40Kas ne prieš mus, tas už mus.
40Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
41Kas duos jums atsigerti taurę vandens mano vardu dėl to, kad priklausote Kristui, iš tiesų sakau jums, tas nepraras savo atlygio”.
41Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
42“Kas pastūmėtų į nuodėmę vieną iš šitų mažutėlių, kurie tiki manimi, tam būtų geriau, jeigu jam užkabintų ant kaklo girnų akmenį ir įmestų į jūrą.
42"Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
43Jei tavo ranka traukia tave nusidėti,­nukirsk ją! Tau geriau sužalotam įeiti į amžinąjį gyvenimą, negu su abiem rankom patekti į pragarą, į negęstančią ugnį,
43Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu.
44kur ‘jų kirminas nemiršta ir ugnis negęsta’.
44Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
45Ir jei tavo koja traukia tave į nuodėmę, nukirsk ją, nes tau geriau luošam įžengti į amžinąjį gyvenimą, negu su abiem kojom būti įmestam į pragarą, į negęstančią ugnį,
45Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
46kur ‘jų kirminas nemiršta ir ugnis negęsta’.
46Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
47Ir jei tavo akis traukia tave nusidėti,­išlupk ją, nes geriau tau vienakiui įeiti į Dievo karalystę, negu su abiem akim būti įmestam į ugnies pragarą,
47Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
48kur ‘jų kirminas nemiršta ir ugnis negęsta’.
48Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
49Kiekvienas bus pasūdytas ugnimi, ir kiekviena auka bus druska pasūdyta.
49"Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
50Druska­geras daiktas, bet jeigu ji netektų sūrumo, kuo ją pasūdyti? Turėkite savyje druskos ir taikiai gyvenkite tarpusavy”.
50Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu."