1Tą dieną, išėjęs iš namų, Jėzus atsisėdo ant ežero kranto.
1Siku hiyohiyo, Yesu alitoka katika ile nyumba, akaenda na kuketi kando ya ziwa.
2Prie Jo susirinko didžiulė minia; todėl Jis įlipo į valtį ir atsisėdo, o žmonės stovėjo pakrantėje.
2Makundi makubwa ya watu yalimzunguka hata Yesu akapanda mashua, akaketi. Hao watu walisimama kwenye ukingo wa ziwa,
3Jis daug jiems kalbėjo palyginimais: “Štai sėjėjas išėjo sėti.
3naye Yesu akawaambia mambo mengi kwa mifano. "Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4Jam besėjant, vieni grūdai nukrito palei kelią, ir atskridę paukščiai juos sulesė.
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5Kiti nukrito uolėtoj vietoj, kur buvo nedaug žemės. Jie greit sudygo, nes neturėjo gilesnio žemės sluoksnio.
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6Saulei patekėjus, daigai išdegė ir, neturėdami šaknų, sudžiūvo.
6Jua lilipochomoza, zilichomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7Kiti nukrito tarp erškėčių. Erškėčiai išaugo ir nusmelkė juos.
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.
8Dar kiti nukrito į gerą žemę ir davė derlių: vieni šimteriopą, kiti šešiasdešimteriopą, dar kiti trisdešimteriopą.
8Lakini nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: nyingine punje mia moja, nyingine sitini na nyingine thelathini.
9Kas turi ausis klausytiteklauso!”
9Mwenye masikio na asikie!"
10Priėję mokiniai paklausė Jo: “Kodėl jiems kalbi palyginimais?”
10Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, "Kwa nini unasema na watu kwa mifano?"
11Jėzus atsakė: “Jums duota pažinti dangaus karalystės paslaptis, o jiems neduota.
11Yesu akawajibu, "Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za Ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.
12Mat, kas turi, tam bus duota, ir jis turės su pertekliumi, o iš neturinčio bus atimta ir tai, ką jis turi.
12Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
13Aš jiems kalbu palyginimais todėl, kad jie žiūrėdami nemato, klausydami negirdi ir nesupranta.
13Ndiyo maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14Jiems pildosi Izaijo pranašystės žodžiai: ‘Girdėti girdėsite, bet nesuprasite, žiūrėti žiūrėsite, bet nematysite.
14Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya: Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa; Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.
15Šitų žmonių širdys aptuko. Jie prastai girdėjo ausimis ir užmerkė akis, kad nepamatytų akimis, neišgirstų ausimis, nesuprastų širdimi ir neatsiverstų, ir Aš jų nepagydyčiau’.
15Maana akili za watu hawa zimepumbaa, wameyaziba masikio yao, wameyafumba macho yao. La sivyo, wangeona kwa macho yao. wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa akili zao, na kunigeukia, asema Bwana, nami ningewaponya.
16Bet palaimintos jūsų akys, nes mato, ir jūsų ausys, nes girdi.
16"Lakini heri yenu ninyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.
17Iš tiesų sakau jums: daugelis pranašų ir teisiųjų troško išvysti, ką jūs matote, bet neišvydo, ir girdėti, ką jūs girdite, bet neišgirdo”.
17Kweli nawaambieni, manabii na watu wengi wema walitamani kuyaona yale mnayoyaona, wasiyaone, na kuyasikia yale mnayoyasikia, wasiyasikie.
18“Tad pasiklausykite palyginimo apie sėjėją.
18"Basi, ninyi sikilizeni maana ya mfano huo wa mpanzi.
19Pas kiekvieną, kuris girdi karalystės žodį ir nesupranta, ateina piktasis ir išplėšia, kas buvo pasėta jo širdyje. Tai yra pasėlis prie kelio.
19Yeyote asikiaye ujumbe wa ufalme bila kuuelewa, ni kama zile mbegu zilizoanguka njiani; yule Mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake.
20Pasėlis uolėtoje vietojetai tas, kuris, girdėdamas žodį, tuojau su džiaugsmu jį priima.
20Ile mbegu iliyopandwa penye mawe ni mfano wa mtu asikiaye ujumbe huo na mara akaupokea kwa furaha.
21Tačiau jis be šaknųnepastovus žmogus. Kilus kokiam sunkumui ar persekiojimui dėl žodžio, jis tuoj pat pasipiktina.
21Lakini haumwingii na kuwa na mizizi ndani yake; huendelea kuuzingatia ujumbe huo kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya ujumbe huo, anakata tamaa mara.
22Pasėlis tarp erškėčiųtai tas, kuris klauso žodžio, bet šio pasaulio rūpesčiai ir turtų apgaulė nustelbia žodį, ir jis lieka nevaisingas.
22Ile mbegu iliyoanguka kati ya miti ya miiba, ni mfano wa mtu asikiaye huo ujumbe, lakini wasiwasi wa ulimwengu huu na anasa za mali huusonga ujumbe huo, naye hazai matunda.
23O pasėlis geroje žemėjetas, kuris girdi ir supranta žodį; tas ir neša vaisių: kas duoda šimteriopą, kas šešiasdešimteriopą, o kas trisdešimteriopą”.
23Ile mbegu iliyopandwa katika udongo mzuri ni mfano wa mtu ausikiaye ujumbe huo na kuuelewa, naye huzaa matunda; mmoja mia, mwingine sitini na mwingine thelathini."
24Jis pateikė jiems kitą palyginimą: “Su dangaus karalyste yra kaip su žmogumi, kuris pasėjo dirvoje gerą sėklą.
24Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25Žmonėms bemiegant, atėjo jo priešas, pasėjo kviečiuose raugių ir nuėjo.
25Lakini watu wakiwa wamelala, adui yake akaja akapanda magugu kati ya ngano, akaenda zake.
26Kai želmuo paūgėjo ir subrandino vaisių, pasirodė ir raugės.
26Basi, mimea ilipoota na kuanza kuchanua, magugu pia yakaanza kuonekana.
27Šeimininko tarnai atėję klausė: ‘Šeimininke, argi ne gerą sėklą pasėjai savo lauke? Iš kurgi atsirado raugių?’
27Watumishi wa yule mwenye shamba wakamwendea, wakamwambia, Mheshimiwa, bila shaka ulipanda mbegu nzuri katika shamba lako. Sasa magugu yametoka wapi?
28Jis atsakė: ‘Tai padarė priešas’. Tarnai pasiūlė: ‘Jei nori, eisime ir jas išravėsime’.
28Yeye akawajibu, Adui ndiye aliyefanya hivyo. Basi, watumishi wake wakamwuliza, Je, unataka twende tukayang'oe
29Jis atsakė: ‘Ne, kad kartais, ravėdami rauges, neišrautumėte kartu su jomis ir kviečių.
29Naye akawajibu, La, msije labda mnapokusanya magugu, mkang'oa na ngano pia.
30Palikite abejus augti iki pjūties. Pjūties metu pasakysiu pjovėjams: ‘Pirmiau išrinkite rauges ir suriškite į pėdelius sudeginti, o kviečius sukraukite į mano kluoną’ ”.
30Acheni vikue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji: kusanyeni kwanza magugu mkayafunge mafungumafungu ya kuchomwa. Lakini ngano ikusanyeni mkaiweke ghalani mwangu."
31Jis pateikė jiems dar vieną palyginimą: “Dangaus karalystė yra kaip garstyčios grūdelis, kurį žmogus ėmė ir pasėjo savo dirvoje.
31Yesu akawaambia watu mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja, akaipanda katika shamba lake.
32Nors jis mažiausias iš visų sėklų, bet užaugęs būna didesnis už visus augalus ir tampa medeliu; net padangių paukščiai atskridę susisuka lizdus jo šakose”.
32Yenyewe ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini ikishaota huwa kubwa kuliko mimea yote. Hukua ikawa mti, na ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake."
33Jis pasakė ir dar kitą palyginimą: “Dangaus karalystė yra kaip raugas, kurį moteris įmaišė trijuose saikuose miltų, ir nuo jo viskas įrūgo”.
33Yesu akawaambia mfano mwingine: "Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyotwaa mama mmoja, akaichanganya na unga pishi tatu, hata unga wote ukaumuka."
34Visa tai Jėzus kalbėjo minioms palyginimais, ir be palyginimų Jis jiems nekalbėjo,
34Yesu aliwaambia watu hayo yote kwa mifano. Hakuwaambia chochote bila kutumia mifano,
35kad išsipildytų, kas buvo per pranašą pasakyta: “Aš atversiu savo burną palyginimais, skelbsiu nuo pasaulio sukūrimo paslėptus dalykus”.
35ili jambo lililonenwa na nabii litimie: "Nitasema kwa mifano; nitawaambia mambo yaliyofichika tangu kuumbwa ulimwengu."
36Paleidęs minias, Jėzus parėjo namo. Prie Jo priėjo mokiniai ir prašė: “Išaiškink mums palyginimą apie rauges dirvoje”.
36Kisha Yesu aliwaaga wale watu, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwambia, "Tufafanulie ule mfano wa magugu shambani."
37Jis jiems atsakė: “Sėjantysis gerą sėklą yra Žmogaus Sūnus.
37Yesu akawaambia, "Mpanzi wa zile mbegu nzuri ni Mwana wa Mtu.
38Dirvatai pasaulis. Gera sėklakaralystės vaikai, o raugės piktojo vaikai.
38Lile shamba ni ulimwengu. Zile mbegu nzuri ni watu wale ambao Ufalme ni wao. Lakini yale magugu ni wale watu wa yule Mwovu.
39Jas pasėjęs priešasvelnias. Pjūtispasaulio pabaiga, o pjovėjai angelai.
39Adui aliyepanda yale magugu ni Ibilisi. Mavuno ni mwisho wa nyakati na wavunaji ni malaika.
40Taigi, kaip surenkamos ir sudeginamos ugnyje raugės, taip bus ir pasaulio pabaigoje.
40Kama vile magugu yanavyokusanywa kuchomwa moto, ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati;
41Žmogaus Sūnus išsiųs savo angelus, tie išrankios iš Jo karalystės visus papiktinimus bei piktadarius
41Mwana wa Mtu atawatuma malaika wake wawakusanye kutoka katika Ufalme wake wale wote wenye kusababisha dhambi, na wote wenye kutenda maovu,
42ir įmes juos į ugnies krosnį. Ten bus verksmas ir dantų griežimas.
42na kuwatupa katika tanuru ya moto, na huko watalia na kusaga meno.
43Tada teisieji spindės kaip saulė savo Tėvo karalystėje. Kas turi ausis klausytiteklauso!”
43Kisha, wale wema watang'ara kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Sikieni basi, kama mna masikio!
44“Dangaus karalystė yra kaip dirvoje paslėptas lobis. Atradęs jį, žmogus tai nuslepia; iš to džiaugsmo eina, parduoda visa, ką turi, ir perka tą dirvą.
44"Ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyofichika shambani. Mtu mmoja aliigundua, akaificha tena. Alifurahi sana hata akaenda kuuza yote aliyokuwa nayo, akalinunua shamba lile.
45Vėl su dangaus karalyste yra kaip su pirkliu, ieškančiu gerų perlų.
45"Tena, Ufalme wa mbinguni umefanana na mfanyabiashara mmoja mwenye kutafuta lulu nzuri.
46Atradęs vieną brangų perlą, jis eina, parduoda visa, ką turi, ir nusiperka jį”.
46Alipopata lulu moja ya thamani kubwa, alienda akauza yote aliyokuwa nayo, akainunua lulu ile.
47“Ir vėl su dangaus karalyste yra kaip su jūron metamu tinklu, užgriebiančiu įvairiausių žuvų.
47"Tena, Ufalme wa mbinguni unafanana na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina.
48Kai jis pilnas, jį išvelka į krantą, susėda ir surenka gerąsias į indus, o blogąsias išmeta.
48Ulipojaa, watu waliuvuta pwani, wakaketi, wakachagua samaki wazuri wakawaweka ndani ya vikapu vyao, na wabaya wakawatupa.
49Taip bus ir pasaulio pabaigoje: išeis angelai, išrankios bloguosius iš gerųjų
49Ndivyo itakavyokuwa mwishoni mwa nyakati: malaika watatokea, watawatenganisha watu wabaya na watu wema,
50ir įmes juos į ugnies krosnį. Ten bus verksmas ir dantų griežimas”.
50na kuwatupa hao wabaya katika tanuru ya moto. Huko watalia na kusaga meno."
51Jėzus paklausė jų: “Ar supratote visa tai?” Jie atsakė: “Taip, Viešpatie”.
51Yesu akawauliza, "Je, mmeelewa mambo haya yote?" Wakamjibu, "Naam."
52Tada Jis jiems tarė: “Todėl kiekvienas Rašto žinovas, tapęs dangaus karalystės mokiniu, panašus į šeimininką, kuris iškelia iš savo lobyno naujų ir senų daiktų”.
52Naye akawaambia, "Hivyo basi, kila mwalimu wa Sheria aliye mwanafunzi wa Ufalme wa mbinguni anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale."
53Baigęs sakyti tuos palyginimus, Jėzus iškeliavo iš ten.
53Yesu alipomaliza kusema mifano hiyo alitoka mahali hapo,
54Jis parėjo į savo tėviškę ir mokė žmones jų sinagogoje taip, kad jie stebėjosi ir klausinėjo: “Iš kur šitam tokia išmintis ir stebuklingi darbai?
54akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, "Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu?
55Argi Jis ne dailidės sūnus?! Argi Jo motina nesivadina Marija, o Jokūbas, Jozė, Simonas ir Judas argi ne Jo broliai?
55Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56Ir Jo seserysargi jos ne visos yra pas mus? Iš kur Jam visa tai?”
56Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?"
57Ir jie ėmė piktintis Juo. O Jėzus jiems atsakė: “Pranašas nebūna be pagarbos, nebent savo tėviškėje ir savo namuose”.
57Basi, wakawa na mashaka naye. Lakini Yesu akawaambia, "Nabii hakosi kuheshimiwa, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani mwake!"
58Ir Jis ten nedarė daug stebuklų dėl jų netikėjimo.
58Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu ya kutoamini kwao.