Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

14

1Anuo metu garsas apie Jėzų pasiekė tetrarchą Erodą,
1Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.
2ir jis savo tarnams pasakė: “Tai Jonas Krikštytojas! Jis prisikėlė iš numirusių, ir todėl jame veikia stebuklingos jėgos”.
2Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."
3Mat Erodas buvo suėmęs Joną, sukaustęs jį ir įmetęs į kalėjimą dėl savo brolio Pilypo žmonos Erodiados.
3Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni
4Nes Jonas jam sakė: “Tau nevalia jos turėti”.
4kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"
5Erodas norėjo nužudyti Joną, bet bijojo žmonių, nes jie laikė jį pranašu.
5Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.
6Erodo gimimo dieną Erodiados duktė šoko svečiams ir patiko Erodui.
6Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,
7Todėl jis su priesaika pažadėjo jai duoti, ko tik ji paprašys.
7hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.
8O ši, savo motinos primokyta, tarė: “Duok man čia dubenyje Jono Krikštytojo galvą”.
8Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."
9Karalius nuliūdo, bet dėl priesaikos ir svečių įsakė duoti.
9Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.
10Jis pasiuntė nukirsti kalėjime Jonui galvą.
10Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.
11Jo galva buvo atnešta dubenyje ir įteikta mergaitei, kuri ją nunešė motinai.
11Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.
12Jono mokiniai atėję pasiėmė kūną, palaidojo ir nuėję pranešė Jėzui.
12Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.
13Tai išgirdęs, Jėzus valtimi nuplaukė į dykvietę, į vienumą. Minios sužinojo ir iš miestų pėsčiomis nusekė paskui.
13Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.
14Išlipęs Jėzus pamatė daugybę žmonių. Jėzui pagailo jų, ir Jis išgydė jų ligonius.
14Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.
15Atėjus vakarui, priėjo mokiniai ir tarė: “Čia dykvietė, ir jau vėlus metas. Paleisk žmones, kad, nuėję į kaimus, nusipirktų maisto”.
15Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."
16Bet Jėzus jiems atsakė: “Nėra reikalo jiems iš čia eiti. Jūs duokite jiems valgyti”.
16Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."
17Jie atsiliepė: “Mes čia turime tik penkis kepalus duonos ir dvi žuvis”.
17Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."
18Jis tarė: “Atneškite juos man”.
18Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."
19Ir, liepęs miniai susėsti ant žolės, Jis paėmė penkis duonos kepalus ir dvi žuvis, pažvelgė į dangų, palaimino, laužė ir davė kepalus mokiniams, o tie dalijo žmonėms.
19Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.
20Visi valgė ir pasisotino. Ir surinko dvylika pilnų pintinių likusių trupinių.
20Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.
21O valgytojų buvo apie penkis tūkstančius vyrų, neskaičiuojant moterų ir vaikų.
21Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.
22Tuojau pat Jėzus privertė savo mokinius sėsti į valtį ir pirma Jo plaukti į kitą ežero pusę, kol Jis paleisiąs minią.
22Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng'ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.
23Paleidęs minią, Jis užkopė nuošaliai į kalną melstis. Atėjus vakarui, Jis buvo ten vienas.
23Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,
24Tuo tarpu valtis jau buvo ežero viduryje, blaškoma bangų, nes pūtė priešingas vėjas.
24na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.
25Ketvirtos nakties sargybos metu Jėzus atėjo pas juos, žengdamas ežero paviršiumi.
25Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.
26Pamatę Jį einantį ežero paviršiumi, mokiniai nusigando ir iš baimės ėmė šaukti: “Tai šmėkla!”
26Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.
27Jėzus tuojau juos prakalbino: “Drąsos! Tai Aš. Nebijokite!”
27Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"
28Petras atsiliepė: “Viešpatie, jei čia Tu, liepk man ateiti pas Tave vandeniu”.
28Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."
29Jis atsakė: “Ateik!” Petras, išlipęs iš valties, ėjo vandeniu, norėdamas ateiti pas Jėzų.
29Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.
30Bet, pamatęs vėjo smarkumą, jis išsigando ir, pradėjęs skęsti, sušuko: “Viešpatie, gelbėk mane!”
30Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"
31Tuojau ištiesęs ranką, Jėzus sugriebė jį ir tarė: “Mažatiki, ko suabejojai?”
31Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"
32Jiems įlipus į valtį, vėjas nurimo.
32Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.
33Tie, kurie buvo valtyje, prisiartinę pagarbino Jį, sakydami: “Tikrai Tu esi Dievo Sūnus!”
33Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."
34Perplaukę jie išlipo į krantą Genezarete.
34Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.
35Pažinę Jį, tos vietos gyventojai pasiuntė į visas to krašto apylinkes ir sugabeno pas Jį visus sergančius.
35Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,
36Jie maldavo Jį leisti palytėti nors Jo apsiausto apvadą. Ir kurie tik palietė­tapo visiškai sveiki.
36wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.