1Atėjo fariziejų ir sadukiejų ir mėgindami prašė Jį parodyti jiems ženklą iš dangaus.
1Mafarisayo na Masadukayo walimwendea Yesu, na kwa kumjaribu, wakamwomba afanye ishara itokayo mbinguni.
2Jis jiems atsakė: “Atėjus vakarui, jūs sakote: ‘Bus giedra, nes dangus raudonas’,
2Lakini Yesu akawajibu, "Wakati wa jioni ukifika ninyi husema: Hali ya hewa itakuwa nzuri kwa maana anga ni jekundu!
3ir rytmetį: ‘Šiandien bus lietaus, nes rausta apsiniaukęs dangus’. Veidmainiai! Jūs mokate atpažinti dangaus veidą, o laiko ženklų ne.
3Na alfajiri mwasema: Leo hali ya hewa itakuwa ya dhoruba, maana anga ni jekundu na tena mawingu yametanda! Basi, ninyi mnajua sana kusoma majira kwa kuangalia anga, lakini kutambua dalili za nyakati hizi hamjui.
4Pikta ir svetimaujanti karta ieško ženklo, tačiau jai nebus duota kito ženklo, kaip tik pranašo Jonos ženklas”. Ir, palikęs juos, nuėjo šalin.
4Kizazi kiovu kisicho na uaminifu! Mnataka ishara, lakini hamtapewa ishara yoyote isipokuwa tu ile ya Yona." Basi, akawaacha, akaenda zake.
5Keldamiesi į kitą ežero pusę, mokiniai buvo užmiršę pasiimti duonos.
5Wanafunzi wake walipokwisha vukia upande wa pili wa ziwa, walijikuta wamesahau kuchukua mikate.
6Jėzus jiems tarė: “Būkite atidūs ir saugokitės fariziejų bei sadukiejų raugo”.
6Yesu akawaambia, "Muwe macho na mjihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!"
7O jie tarpusavy svarstė: “Tai todėl, kad nepasiėmėme duonos”.
7Lakini wao wakawa wanajadiliana: "Anasema hivyo kwa kuwa hatukuchukua mikate."
8Tai supratęs, Jėzus tarė: “Mažatikiai! Kodėl svarstote, kad nepasiėmėte duonos?
8Yesu alijua mawazo yao, akawaambia, "Enyi watu wenye imani haba! Mbona mnajadiliana juu ya kutokuwa na mikate?
9Argi dar nesuprantate? Ar neprisimenate penkių kepalų penkiems tūkstančiams ir kiek pintinių surinkote trupinių?
9Je, hamjaelewa bado? Je, hamkumbuki nilipoimega ile mikate mitano kwa ajili ya wale watu elfu tano? Je, mlijaza vikapu vingapi vya makombo?
10Arba septynių kepalų keturiems tūkstančiams ir kiek pintinių surinkote trupinių?!
10Au, ile mikate saba waliyogawiwa wale watu elfu nne, je, mlikusanya vikapu vingapi vya mabaki?
11Tad kaip nesuprantate, jog kalbėjau jums ne apie duoną. Fariziejų ir sadukiejų raugo saugokitės!”
11Inawezekanaje hamwelewi ya kwamba sikuwa nikisema juu ya mikate? Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo!"
12Tada jie suprato, kad Jis liepė saugotis ne duonos raugo, bet fariziejų ir sadukiejų mokslo.
12Hapo wanafunzi wakafahamu kwamba aliwaambia wajihadhari siyo na chachu ya mikate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
13Atėjęs į Pilypo Cezarėjos apylinkes, Jėzus paklausė savo mokinius: “Kuo žmonės mane, Žmogaus Sūnų, laiko?”
13Yesu alipofika pande za Kaisarea Filipi, aliwauliza wanafunzi wake, "Watu wanasema Mwana wa Mtu kuwa ni nani?"
14Jie atsakė: “Vieni Jonu Krikštytoju, kiti Eliju, kiti Jeremiju ar dar kuriuo iš pranašų”.
14Wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa ni Yohane mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii."
15Jis vėl paklausė: “O kuo jūs mane laikote?”
15Yesu akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?"
16Tada Simonas Petras atsakė: “Tu esi Kristus, gyvojo Dievo Sūnus”.
16Simoni Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai."
17Jėzus jam atsakė: “Palaimintas tu, Simonai, Jonos sūnau, nes ne kūnas ir kraujas tau tai apreiškė, bet mano Tėvas, kuris yra danguje.
17Yesu akasema, "Heri wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana si binadamu aliyekufunulia ukweli huu, ila Baba yangu aliye mbinguni.
18Ir Aš tau sakau: tu esi Petras, ir ant šios uolos Aš pastatysiu savo bažnyčią, ir pragaro vartai jos nenugalės.
18Nami nakwambia: wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala kifo chenyewe hakitaweza kulishinda.
19Tau duosiu dangaus karalystės raktus; ką tu suriši žemėje, bus surišta ir danguje, ir ką tu atriši žemėje, bus atrišta ir danguje”.
19Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni; kila utakachofunga duniani, kitafungwa pia mbinguni; kila utakachofungua duniani, kitafunguliwa pia mbinguni."
20Tada Jis griežtai įsakė savo mokiniams niekam neskelbti, kad Jis yra JėzusKristus.
20Kisha akawaonya wanafunzi wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
21Nuo tada Jėzus pradėjo aiškinti savo mokiniams, kad Jis turįs eiti į Jeruzalę ir daug iškentėti nuo vyresniųjų, aukštųjų kunigų ir Rašto žinovų, būti nužudytas ir trečią dieną prisikelti.
21Tangu wakati huo Yesu alianza kuwajulisha waziwazi wanafunzi wake: "Ni lazima mimi niende Yerusalemu, na huko nikapate mateso mengi yatakayosababishwa na wazee, makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Nitauawa, na siku ya tatu nitafufuliwa."
22Tada Petras, pasivadinęs Jį į šalį, ėmė drausti: “Jokiu būdu, Viešpatie, Tau neturi taip atsitikti!”
22Hapo Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea: "Isiwe hivyo Bwana! Jambo hili halitakupata!"
23Bet Jis atsisukęs pasakė Petrui: “Eik šalin, šėtone! Tu man papiktinimas, nes mąstai ne apie tai, kas Dievo, o kas žmonių”.
23Lakini Yesu akageuka, akamwambia Petro, "Ondoka mbele yangu Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Mawazo yako si ya mungu bali ni ya kibinadamu!"
24Tuomet Jėzus savo mokiniams pasakė: “Jei kas nori eiti paskui mane, teišsižada pats savęs, teima savo kryžių ir teseka manimi.
24Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kama mtu yeyote anataka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
25Nes, kas nori išgelbėti savo gyvybę, tas ją praras; o kas praras savo gyvybę dėl manęs, tas ją atras.
25Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza;
26Kokia gi žmogui nauda, jeigu jis laimėtų visą pasaulį, o pakenktų savo sielai? Arba kuo žmogus galėtų išsipirkti savo sielą?
26lakini mtu anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata. Je, mtu atafaidi nini akiupata utajiri wote wa ulimwengu na hali amepoteza maisha yake? Au, mtu atatoa kitu gani kiwe badala ya maisha yake?
27Nes Žmogaus Sūnus ateis savo Tėvo šlovėje su savo angelais, ir tuomet Jis atlygins kiekvienam pagal jo darbus.
27Maana, Mwana wa Mtu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika wake, na hapo ndipo atakapomlipa kila mtu kadiri ya matendo yake.
28Iš tiesų sakau jums: kai kurie iš čia stovinčių neragaus mirties, kol pamatys Žmogaus Sūnų, ateinantį savo karalystėje”.
28Kweli nawaambieni, wako wengine papahapa ambao hawatakufa kabla ya kumwona Mwana wa Mtu akija katika Ufalme wake."