Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

19

1Baigęs tai kalbėti, Jėzus pasitraukė iš Galilėjos ir atėjo į Judėjos sritį, anapus Jordano.
1Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, alitoka Galilaya, akaenda katika mkoa wa Yudea, ng'ambo ya mto Yordani.
2Paskui Jį sekė didelės minios žmonių, ir Jis ten juos išgydė.
2Watu wengi walimfuata huko, naye akawaponya.
3Fariziejai taip pat atėjo pas Jį ir, mėgindami Jį, klausė: “Ar galima vyrui dėl kokios nors priežasties atleisti savo žmoną?”
3Mafarisayo kadhaa walimjia, wakamwuliza kwa kumtega, "Je, ni halali mume kumpa talaka mkewe kwa kisa chochote?"
4Jis atsakė: “Argi neskaitėte, jog Kūrėjas iš pradžių ‘sukūrė juos, vyrą ir moterį’,
4Yesu akawajibu, "Je, hamkusoma katika Maandiko Matakatifu kwamba Mungu aliyemuumba mtu tangu mwanzo alimfanya mwanamume na mwanamke,
5ir pasakė: ‘Todėl žmogus paliks tėvą ir motiną ir susijungs su savo žmona, ir du taps vienu kūnu’.
5na akasema: Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?
6Taigi jie jau nebėra du, o vienas kūnas. Todėl ką Dievas sujungė, žmogus teneperskiria”.
6Kwa hiyo wao si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asikitenganishe."
7Tada jie paklausė Jo: “O kodėl Mozė įsakė duoti skyrybų raštą, atleidžiant žmoną?”
7Lakini wao wakamwuliza, "Kwa nini basi, Mose alituagiza mwanamke apewe hati ya talaka na kuachwa?"
8Jis atsakė: “Mozė leido jums atleisti savo žmonas dėl jūsų širdies kietumo, bet pradžioje taip nebuvo.
8Yesu akawajibu, "Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
9Ir Aš jums sakau: kas atleidžia savo žmoną,­jei ne dėl ištvirkavimo,­ir veda kitą, svetimauja. Ir kas atleistąją veda, svetimauja”.
9Lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo. Basi nawaambieni, yeyote atakayemwacha mke wake isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, akaoa mke mwingine, anazini."
10Jo mokiniai pasakė Jam: “Jei tokie vyro ir žmonos reikalai, tai geriau nevesti”.
10Wanafunzi wake wakamwambia, "Ikiwa mambo ya mume na mkewe ni hivyo, ni afadhali kutooa kabisa."
11Jis jiems atsakė: “Ne visi gali išmanyti tuos žodžius, o tik tie, kuriems duota.
11Yesu akawaambia, "Si wote wanaoweza kulipokea fundisho hili, isipokuwa tu wale waliojaliwa na Mungu.
12Nes yra eunuchų, kurie gimė tokie iš motinos įsčių. Yra eunuchų, kuriuos tokius padarė žmonės. Ir yra eunuchų, kurie patys save tokius padarė dėl dangaus karalystės. Kas pajėgia išmanyti, teišmano”.
12Maana kuna sababu kadhaa za kutoweza kuoa: wengine ni kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine kwa sababu wamefanywa hivyo na watu, na wengine wameamua kutooa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee."
13Tuomet atvedė pas Jį vaikučių, kad Jis uždėtų rankas ant jų ir pasimelstų, o mokiniai draudė jiems.
13Kisha watu wakamletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono na kuwaombea. Lakini wanafunzi wakawakemea.
14Bet Jėzus tarė: “Leiskite mažutėlius ir nedrauskite jiems ateiti pas mane, nes tokių yra dangaus karalystė”.
14Yesu akasema, "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie; maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu walio kama watoto hawa."
15Ir, uždėjęs ant jų rankas, Jis iš ten išėjo.
15Basi, akawawekea mikono, kisha akaondoka mahali hapo.
16Ir štai vienas, prie Jo priėjęs, klausė: “Gerasis Mokytojau, ką gero turiu daryti, kad turėčiau amžinąjį gyvenimą?”
16Mtu mmoja alimjia Yesu, akamwuliza, "Mwalimu, nifanye kitu gani chema ili niupate uzima wa milele?"
17Jis jam atsakė: “Kodėl vadini mane geru? Nė vieno nėra gero, tik vienas Dievas. O jei nori įeiti į gyvenimą, laikykis įsakymų”.
17Yesu akamwambia, "Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema. Ukitaka kuingia katika uzima, shika amri."
18Tas paklausė Jo: “Kokių?” Jėzus atsakė: “Nežudyk, nesvetimauk, nevok, melagingai neliudyk;
18Yule mtu akamwuliza, "Amri zipi?" Yesu akasema, "Usiue, usizini, usiibe, usitoe ushahidi wa uongo,
19gerbk savo tėvą ir motiną; mylėk savo artimą kaip save patį”.
19waheshimu baba yako na mama yako; na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe."
20Jaunuolis Jam tarė: “Viso to laikausi nuo savo jaunystės. Ko dar man trūksta?”
20Huyo kijana akamwambia, "Hayo yote nimeyazingatia tangu utoto wangu; sasa nifanye nini zaidi?"
21Jėzus atsakė: “Jei nori būti tobulas, eik, parduok, ką turi, išdalink vargšams, ir turėsi turtą danguje. Tada ateik ir sek paskui mane”.
21Yesu akamwambia, "Kama unapenda kuwa mkamilifu, nenda ukauze mali yako uwape maskini hiyo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni, kisha njoo unifuate."
22Išgirdęs tuos žodžius, jaunuolis nuliūdęs pasitraukė, nes turėjo daug turto.
22Huyo kijana aliposikia hayo, alienda zake akiwa mwenye huzuni, maana alikuwa na mali nyingi.
23Tada Jėzus tarė savo mokiniams: “Iš tiesų sakau jums: turtingas sunkiai įeis į dangaus karalystę.
23Hapo Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kweli nawaambieni, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.
24Ir dar kartą jums sakau: lengviau kupranugariui išlįsti pro adatos ausį, negu turtingam įeiti į Dievo karalystę”.
24Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni."
25Tai išgirdę, Jo mokiniai labai nustebo ir klausė: “Kas tada gali būti išgelbėtas?”
25Wale wanafunzi waliposikia hivyo walishangaa, wakamwuliza, "Ni nani basi, awezaye kuokoka?"
26Jėzus pažvelgė į juos ir tarė: “Žmonėms tai neįmanoma, bet Dievui viskas įmanoma”.
26Yesu akawatazama, akasema, "Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu mambo yote huwezekana."
27Tada Petras Jį paklausė: “Štai mes viską palikome ir sekame paskui Tave. Kas mums bus už tai?”
27Kisha Petro akasema, "Na sisi je? Tumeacha yote tukakufuata; tutapata nini basi?"
28Jėzus jiems atsakė: “Iš tiesų sakau jums: atgimime, kai Žmogaus Sūnus sėdės savo šlovės soste, jūs, mano sekėjai, irgi sėdėsite dvylikoje sostų, teisdami dvylika Izraelio giminių.
28Yesu akawaambia, "Nawaambieni kweli, Mwana wa Mtu atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake katika ulimwengu mpya, ninyi mlionifuata mtaketi katika viti kumi na viwili mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
29Ir kiekvienas, kas paliko namus ar brolius, ar seseris, ar tėvą, ar motiną, ar žmoną, ar vaikus, ar laukus dėl mano vardo, gaus šimteriopai ir paveldės amžinąjį gyvenimą.
29Na kila aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi, na kupata uzima wa milele.
30Tačiau daug pirmųjų bus paskutiniai, ir paskutiniai­pirmi”.
30Lakini walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.