1“Su dangaus karalyste yra panašiai, kaip su šeimininku, kuris anksti rytą išėjo samdytis darbininkų savo vynuogynui.
1"Ufalme wa mbinguni unafanana na mtu mwenye shamba la mizabibu, ambaye alitoka asubuhi na mapema kuwaajiri wafanyakazi katika shamba lake.
2Susiderėjęs su darbininkais po denarą dienai, jis nusiuntė juos į savo vynuogyną.
2Akapatana nao kuwalipa dinari moja kwa siku, kisha akawapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3Išėjęs apie trečią valandą, jis pamatė kitus, stovinčius aikštėje be darbo.
3Akatoka mnamo saa tatu asubuhi, akaona watu wengine wamesimama sokoni, hawana kazi.
4Jis tarė jiems: ‘Eikite ir jūs į mano vynuogyną, ir, kas bus teisinga, aš jums užmokėsiu!’ Jie nuėjo.
4Akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu, nami nitawapeni haki yenu.
5Ir vėl išėjęs apie šeštą ir devintą valandą, jis taip pat padarė.
5Basi, wakaenda. Huyo mwenye shamba akatoka tena mnamo saa sita na saa tisa, akafanya vivyo hivyo.
6Išėjęs apie vienuoliktą, jis rado dar kitus stovinčius be darbo ir sako jiems: ‘Ko čia stovite visą dieną be darbo?’
6Hata mnamo saa kumi na moja jioni, akatoka tena; akakuta watu wengine wamesimama pale sokoni. Basi, akawauliza, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
7Jie atsakė: ‘Kad niekas mūsų nepasamdė’. Jis tarė jiems: ‘Eikite ir jūs į vynuogyną, ir, kas bus teisinga, jūs gausite’.
7Wakamjibu: Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Yeye akawaambia, Nendeni nanyi mkafanye kazi katika shamba la mizabibu.
8Atėjus vakarui, vynuogyno šeimininkas liepė ūkvedžiui: ‘Pašauk darbininkus ir išmokėk jiems atlyginimą, pradėdamas nuo paskutiniųjų ir baigdamas pirmaisiais!’
8"Kulipokuchwa, huyo mwenye shamba alimwambia mtunza hazina wake, Waite wafanyakazi ukawalipe mshahara wao, ukianzia na wale walioajiriwa mwisho, na kumalizia na wale wa kwanza.
9Atėję pasamdytieji apie vienuoliktą valandą kiekvienas gavo po denarą.
9Basi, wakaja wale walioajiriwa mnamo saa kumi na moja, wakapokea kila mmoja dinari moja.
10Prisiartinę pirmieji manė daugiau gausią, bet irgi gavo po denarą.
10Wale wa kwanza walipofika, walikuwa wanadhani watapewa zaidi; lakini hata wao wakapewa kila mmoja dinari moja.
11Paėmę jie murmėjo prieš šeimininką,
11Wakazipokea fedha zao, wakaanza kumnung'unikia yule bwana.
12sakydami: ‘Šitie paskutinieji tedirbo vieną valandą, o tu sulyginai juos su mumis, nešusiais dienos ir kaitros naštą’.
12Wakasema, Watu hawa walioajiriwa mwisho walifanya kazi kwa muda wa saa moja tu, mbona umetutendea sawa na wao hali sisi tumevumilia kazi ngumu kutwa na jua kali?
13Bet jis vienam iš jų atsakė: ‘Bičiuli, aš tavęs neskriaudžiu! Argi ne už denarą susiderėjai su manimi?
13"Hapo yule bwana akamjibu mmoja wao, Rafiki, sikukupunja kitu! Je, hukupatana nami mshahara wa denari moja?
14Imk, kas tavo, ir eik sau. Aš noriu ir šitam paskutiniam duoti tiek, kiek tau.
14Chukua haki yako, uende zako. Napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
15Argi aš neturiu teisės daryti ką noriu su tuo, kas mano? Ar todėl tavo akis pikta, kad aš geras?’
15Je, sina haki ya kufanya na mali yangu nipendavyo? Je, unaona kijicho kwa kuwa mimi ni mwema?"
16Taip paskutinieji bus pirmi, o pirmiejipaskutiniai; nes daug yra pašauktų, bet maža išrinktų”.
16Yesu akamaliza kwa kusema, "Hivyo, walio wa mwisho watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho."
17Išvykdamas į Jeruzalę, Jėzus pasiėmė skyrium dvylika mokinių ir kelyje kalbėjo jiems:
17Yesu alipokuwa anakwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani, na njiani akawaambia,
18“Štai einame į Jeruzalę, ir Žmogaus Sūnus bus išduotas aukštiesiems kunigams bei Rašto žinovams. Jie nuteis Jį mirti,
18"Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe.
19atiduos pagonims tyčiotis, nuplakti ir nukryžiuoti, ir trečią dieną Jis prisikels”.
19Watamkabidhi kwa watu wa mataifa mengine ili adhihakiwe, apigwe viboko na kusulubiwa; lakini siku ya tatu atafufuliwa."
20Tada prie Jėzaus priėjo Zebediejaus sūnų motina kartu su savo sūnumis ir, pagarbinusi Jį, ėmė kažko prašyti.
20Hapo mama yao wana wa Zebedayo alimjia Yesu pamoja na wanawe, akapiga magoti mbele yake na kumwomba kitu.
21Jis paklausė jos: “Ko nori?” Toji atsakė: “Leisk, kad šitie abu mano sūnūs Tavo karalystėje sėdėtų vienas Tavo dešinėje, o kitas kairėje”.
21Yesu akamwuliza, "Unataka nini?" Huyo mama akamwambia, "Ahidi kwamba katika Ufalme wako, hawa wanangu wawili watakaa mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto."
22Jėzus atsakė: “Nežinote, ko prašote. Ar galite gerti taurę, kurią Aš gersiu, ir būti krikštijami krikštu, kuriuo Aš krikštijamas?” Jie atsakė: “Galime”.
22Yesu akajibu, "Hamjui mnaomba nini. Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa mimi?" Wakamjibu, "Tunaweza."
23Tuomet Jis tarė: “Mano taurę, tiesa, gersite, ir krikštu, kuriuo Aš krikštijamas, būsite pakrikštyti, bet vietą mano dešinėje ar kairėje ne Aš duodu; tai bus tiems, kuriems mano Tėvo paruošta”.
23Yesu akawaambia, "Kweli mtakunywa kikombe changu, lakini kuketi kulia au kushoto kwangu si kazi yangu kupanga; jambo hilo watapewa wale waliowekewa tayari na Baba yangu."
24Tai išgirdę, kiti dešimt mokinių supyko ant dviejų brolių.
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakawakasirikia hao ndugu wawili.
25O Jėzus, pasikvietęs juos pas save, tarė: “Jūs žinote, kad pagonių valdovai jiems viešpatauja ir didieji juos valdo.
25Hivyo Yesu akawaita, akawaambia, "Mnajua kwamba watawala wa mataifa hutawala watu wao kwa mabavu na wakuu hao huwamiliki watu wao.
26Bet tarp jūsų taip neturi būti. Kas iš jūsų nori būti didžiausias, tebūnie jūsų tarnas,
26Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu sharti awe mtumishi wa wote;
27ir kas nori būti pirmas tarp jūsų, tebūnie jūsų vergas.
27na anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu sharti awe mtumishi wenu.
28Ir Žmogaus Sūnus atėjo, ne kad Jam tarnautų, bet pats tarnauti ir savo gyvybės atiduoti kaip išpirkos už daugelį”.
28Jinsi hiyohiyo, Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, bali kutumikia na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
29Jiems išeinant iš Jericho, paskui Jį sekė didelė minia.
29Yesu alipokuwa anaondoka mjini Yeriko, umati wa watu ulimfuata.
30Ir štai pakelėje sėdėjo du neregiai. Išgirdę praeinantį Jėzų, jie ėmė šaukti: “Viešpatie, Dovydo Sūnau, pasigailėk mūsų!”
30Basi, kulikuwa na vipofu wawili wameketi kando ya njia, na waliposikia kwamba Yesu alikuwa anapitia hapo, walipaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
31Minia draudė juos, kad tylėtų, bet anie dar garsiau šaukė: “Viešpatie, Dovydo Sūnau, pasigailėk mūsų!”
31Ule umati wa watu ukawakemea na kuwaambia wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaaza sauti: "Mheshimiwa, Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
32Jėzus sustojo, pašaukė juos ir paklausė: “Ko norite, kad jums padaryčiau?”
32Yesu akasimama, akawaita na kuwauliza, "Mnataka niwafanyie nini?"
33Neregiai Jam atsakė: “Viešpatie, kad atsivertų mūsų akys”.
33Wakamjibu, "Mheshimiwa, tunaomba macho yetu yafumbuliwe."
34Pasigailėjęs Jėzus palietė jų akis; jie tučtuojau praregėjo ir nusekė paskui Jį.
34Basi, Yesu akawaonea huruma, akawagusa macho yao, na papo hapo wakaweza kuona, wakamfuata.