1Jėzui gimus Judėjos Betliejuje karaliaus Erodo dienomis, štai atkeliavo į Jeruzalę išminčiai iš Rytų ir klausinėjo:
1Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
2“Kur yra gimęs žydų karalius? Mes matėme Jo žvaigždę Rytuose ir atvykome pagarbinti Jį”.
2wakauliza, "Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu."
3Tai išgirdęs, karalius Erodas sunerimo, o su juo ir visa Jeruzalė.
3Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
4Jis sukvietė visus tautos aukštuosius kunigus bei Rašto žinovus ir teiravosi, kur turėjęs gimti Kristus.
4Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, "Kristo atazaliwa wapi?"
5Tie jam atsakė: “Judėjos Betliejuje, nes taip pranašo parašyta:
5Nao wakamjibu, "Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
6‘Ir tu, Judo žemės Betliejau, anaiptol nesi mažiausias tarp Judo valdovų, nes iš tavęs išeis Valdovas, kuris ganys mano tautą Izraelį’ ”.
6Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli."
7Tada Erodas, slapta pasikvietęs išminčius, sužinojo iš jų apie žvaigždės pasirodymo metą
7Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
8ir, siųsdamas į Betliejų, tarė: “Keliaukite ir viską kruopščiai sužinokite apie kūdikį. Radę praneškite man, kad ir aš nuvykęs Jį pagarbinčiau”.
8Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, "Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu."
9Išklausę karaliaus, išminčiai leidosi kelionėn. Ir štai žvaigždė, kurią jie matė Rytuose, traukė pirma, kol sustojo ties ta vieta, kur buvo kūdikis.
9Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
10Išvydę žvaigždę, jie labai džiaugėsi.
10Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
11Įžengę į namus, rado kūdikį su motina Marija ir, parpuolę ant žemės, Jį pagarbino. Jie atidarė savo brangenybių dėžes ir davė Jam dovanų: aukso, smilkalų ir miros.
11Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
12Sapne įspėti nebegrįžti pas Erodą, kitu keliu pasuko į savo kraštą.
12Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
13Jiems iškeliavus, štai pasirodė Juozapui sapne Viešpaties angelas ir tarė: “Kelkis, imk kūdikį, Jo motiną ir bėk į Egiptą. Pasilik ten, kol tau pasakysiu, nes Erodas ieškos kūdikio, norėdamas Jį nužudyti”.
13Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto."
14Atsikėlęs Juozapas paėmė kūdikį ir Jo motiną ir pasitraukė į Egiptą.
14Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
15Ten jis prabuvo iki Erodo mirties, kad išsipildytų, kas Viešpaties buvo pasakyta per pranašą: “Iš Egipto pašaukiau savo Sūnų”.
15Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: "Nilimwita Mwanangu kutoka Misri."
16Erodas, pamatęs, kad jį išminčiai apgavo, baisiai įniršo ir pasiuntė išžudyti Betliejuje ir jo apylinkėse visus berniukus, dvejų metų ir jaunesnius, pagal laiką, kurį buvo patyręs iš išminčių.
16Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
17Tada išsipildė, kas buvo pasakyta per pranašą Jeremiją:
17Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
18“Ramoje pasigirdo šauksmas, raudos, aimanos ir garsios dejonės: tai Rachelė rauda savo vaikų; ir niekas jos nepaguos, nes jų nebėra”.
18"Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki."
19Erodui mirus, štai Viešpaties angelas pasirodė per sapną Juozapui Egipte
19Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
20ir tarė: “Kelkis, imk kūdikį su Jo motina ir keliauk į Izraelio žemę, nes jau mirė tie, kurie ieškojo kūdikio gyvybės”.
20akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa."
21Tuomet Juozapas atsikėlė, paėmė kūdikį ir Jo motiną ir sugrįžo į Izraelio žemę.
21Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
22Bet, išgirdęs, jog Archelajas valdo Judėją po savo tėvo Erodo, pabūgo ten vykti. Įspėtas sapne, nukeliavo į Galilėjos sritį
22Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
23ir apsigyveno Nazareto mieste, kad išsipildytų, kas buvo pranašų pasakyta: “Jį vadins Nazariečiu”.
23akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: "Ataitwa Mnazare."