1Anomis dienomis pasirodė Jonas Krikštytojas ir pamokslavo Judėjos dykumoje,
1Siku hizo Yohane Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea:
2skelbdamas: “Atgailaukite, nes prisiartino dangaus karalystė”.
2"Tubuni, maana Ufalme wa mbinguni umekaribia."
3O jis buvo tas, apie kurį pranašas Izaijas yra pasakęs: “Dykumoje šaukiančiojo balsas: ‘Paruoškite Viešpačiui kelią! Ištiesinkite Jam takus!’ ”
3Huyu Yohane ndiye yule ambaye nabii Isaya alinena juu yake aliposema: "Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni vijia vyake."
4Pats Jonas vilkėjo kupranugario vilnų apdaru, o strėnas buvo susijuosęs odiniu diržu. Jis maitinosi skėriais ir lauko medumi.
4Yohane alivaa vazi lililoshonwa kwa manyoya ya ngamia, na ukanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
5Tuomet Jeruzalė, visa Judėja ir visa Pajordanė ėjo pas jį.
5Basi, watu kutoka Yerusalemu, kutoka mkoa wote wa Yudea na sehemu zote za kandokando ya mto Yordani, walimwendea,
6Žmonės buvo jo krikštijami Jordano upėje ir išpažindavo savo nuodėmes.
6wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
7Pamatęs daug fariziejų ir sadukiejų, einančių pas jį krikštytis, jis jiems sakė: “Angių išperos, kas perspėjo jus bėgti nuo ateinančios rūstybės?
7Lakini alipowaona Mafarisayo wengi na Masadukayo wanamjia ili awabatize, aliwaambia, "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mnaweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8Duokite vaisių, vertų atgailos!
8Onyesheni basi kwa matendo, kwamba mmetubu kweli.
9Ir nebandykite ramintis: ‘Mūsų tėvasAbraomas’. Aš jums sakau, kad Dievas gali pažadinti Abraomui vaikų iš šitų akmenų.
9Msidhani kwamba mtaweza kujitetea kwa kusema, Baba yetu ni Abrahamu! Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyafanya mawe haya yawe watoto wa Abrahamu.
10Štai kirvis jau prie medžių šaknų, ir kiekvienas medis, kuris neduoda gerų vaisių, yra nukertamas ir įmetamas į ugnį.
10Basi, shoka liko tayari kuikata mizizi ya miti; hivyo, kila mti usiozaa matunda mazuri, utakatwa na kutupwa motoni.
11Aš jus krikštiju vandeniu atgailai, bet Tas, kuris ateina po manęs,galingesnis už mane, aš nevertas net Jo sandalų nuauti. Jis krikštys jus Šventąja Dvasia ir ugnimi.
11Mimi ninawabatizeni kwa maji kuonyesha kwamba mmetubu. Lakini yule anayekuja baada yangu ana uwezo kuliko mimi. Mimi sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
12Jo rankoje vėtyklė, ir Jis kruopščiai išvalys savo kluoną. Kviečius surinks į klėtį, o pelus sudegins neužgesinama ugnimi”.
12Yeye anashika mkononi chombo cha kupuria nafaka, ili aipure nafaka yake; akusanye ngano ghalani, na makapi ayachome kwa moto usiozimika."
13Tuomet Jėzus iš Galilėjos atėjo prie Jordano pas Joną krikštytis.
13Wakati huo Yesu alitoka Galilaya akafika katika mto Yordani, akamwendea Yohane ili abatizwe naye.
14Jonas Jį atkalbinėjo: “Aš turėčiau būti Tavo pakrikštytas, o Tu ateini pas mane!”
14Lakini Yohane alijaribu kumzuia akisema, "Je, wewe unakuja kwangu? Mimi hasa ndiye ninayehitaji kubatizwa nawe."
15Bet Jėzus jam atsakė: “Šį kartą paklausyk! Taip mudviem dera įvykdyti visą teisumą”. Tada Jonas sutiko.
15Lakini Yesu akamjibu, "Acha tu iwe hivyo kwa sasa, maana kwa namna hii inafaa tuyatekeleze yale yote Mungu anayotaka." Hapo Yohane akakubali.
16Pakrikštytas Jėzus tuoj išbrido iš vandens. Ir štai Jam atsivėrė dangus, ir Jis pamatė Dievo Dvasią, sklendžiančią žemyn it balandį ir nusileidžiančią ant Jo.
16Mara tu Yesu alipokwisha batizwa, alitoka majini; na ghafla mbingu zikafunguka, akaona Roho wa Mungu akishuka kama njiwa na kutua juu yake.
17Ir štai balsas iš dangaus prabilo: “Šitas yra mano mylimas Sūnus, kuriuo Aš gėriuosi”.
17Sauti kutoka mbinguni ikasema, "Huyu ndiye Mwanangu mpendwa, nimependezwa naye."