Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

23

1Tuomet Jėzus ėmė kalbėti minioms ir savo mokiniams:
1Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2“Į Mozės krasę atsisėdo Rašto žinovai ir fariziejai.
2"Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
3Todėl visko, ko jie liepia jums laikytis, laikykitės ir vykdykite, tačiau nesielkite, kaip jie elgiasi, nes jie kalba, bet nedaro.
3Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4Jie riša sunkias, nepanešamas naštas ir krauna žmonėms ant pečių, o patys nenori jų nė pirštu pajudinti.
4Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5Jie viską daro, kad būtų žmonių matomi. Jie pasiplatina maldos diržus ir pasididina apsiaustų kutus.
5Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
6Jie mėgsta garbės vietas pokyliuose bei pirmuosius krėslus sinagogose,
6Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
7mėgsta sveikinimus aikštėse ir, kad žmonės juos vadintų ‘Rabi, Rabi’.
7Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
8Bet jūs nesivadinkite ‘Rabi’, nes vienas yra jūsų Mokytojas­Kristus, o jūs visi esate broliai.
8Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
9Ir nė vieno žemėje nevadinkite tėvu, nes vienas jūsų Tėvas, kuris yra danguje.
9Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
10Taip pat nesivadinkite mokytojais, nes vienas jūsų Mokytojas­ Kristus.
10Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
11Kas iš jūsų didžiausias, tebūna jums tarnas.
11Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12Ir kas save aukština, bus pažemintas, o kas save žemina, bus išaukštintas.
12Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
13Bet vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs užrakinate žmonėms dangaus karalystę ir nei patys neinate, nei į ją einantiems neleidžiate įeiti.
13"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
14Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs suryjate našlių namus ir dedatės kalbą ilgas maldas, todėl gausite dar didesnį pasmerkimą.
14Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs keliaujate per jūrą ir sausumą, kad laimėtumėte vieną naujatikį, ir kai jis tokiu tampa, jūs padarote iš jo pragaro vaiką, dvigubai blogesnį už jus pačius.
15"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe.
16Vargas jums, aklieji vadai, kurie sakote: ‘Jei kas prisiektų šventykla, tai nieko, o jei kas prisiektų šventyklos auksu, tai jis įsipareigoja’.
16"Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
17Kvaili jūs ir akli! Kas gi didesnis­auksas ar šventykla, kuri pašventina auksą?
17Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18Arba vėl sakote: ‘Jei kas prisiektų aukuru, tai nieko, o jei kas prisiektų atnaša ant aukuro, tai jis įsipareigoja’.
18Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19Kvaili ir akli! Kas gi didesnis­ atnaša ar aukuras, kuris pašventina atnašą?
19Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20Todėl, kas prisiekia aukuru, prisiekia juo ir viskuo, kas ant jo padėta,
20Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
21o kas prisiekia šventykla, prisiekia ja ir Tuo, kuris joje gyvena.
21Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
22Ir kas prisiekia dangumi, prisiekia Dievo sostu ir Tuo, kuris jame sėdi.
22Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
23Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs duodate dešimtinę nuo mėtų, krapų ir kmynų, o paliekate, kas Įstatyme svarbiau,­teisingumą, gailestingumą ir tikėjimą. Tai turite daryti ir ano nepalikti!
23Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24Akli vadai, jūs iškošiate uodą, o praryjate kupranugarį.
24Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
25Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs valote taurės bei dubens išorę, o viduje esate pilni gobšumo ir nesusilaikymo.
25"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
26Aklas fariziejau! Pirmiau išvalyk taurės ir dubens vidų, kad būtų švari ir išorė!
26Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
27Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs panašūs į pabaltintus kapus, kurie iš paviršiaus atrodo gražiai, o viduje pilni numirėlių kaulų ir visokių nešvarumų.
27"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28Taip ir jūs iš paviršiaus atrodote žmonėms teisūs, o viduje esate pilni veidmainystės ir nedorumo.
28Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29Vargas jums, veidmainiai Rašto žinovai ir fariziejai! Nes jūs statote pranašams antkapius, puošiate teisiųjų kapus
29"Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30ir sakote: ‘Jei būtume gyvenę savo protėvių dienomis, nebūtume kartu su jais susitepę pranašų krauju’.
30Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
31Taigi jūs patys prieš save liudijate, jog esate pranašų žudytojų vaikai.
31Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
32Pripildykite tad savo tėvų saiką!
32Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33Gyvatės! Angių išperos! Kaip jūs ištrūksite nuo pasmerkimo į pragarą?!
33Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu?
34Todėl štai siunčiu pas jus pranašų, išminčių ir Rašto žinovų. Vienus iš jų užmušite ir nukryžiuosite, kitus plaksite savo sinagogose ir persekiosite nuo miesto iki miesto,
34Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35kad ant jūsų kristų visas teisus kraujas, pralietas žemėje, pradedant teisiojo Abelio krauju ir baigiant krauju Barachijo sūnaus Zacharijo, kurį nužudėte tarp šventyklos ir aukuro.
35Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36Iš tiesų sakau jums: visa tai ištiks šitą kartą”.
36Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
37“Jeruzale, Jeruzale! Tu žudai pranašus ir užmėtai akmenimis tuos, kurie pas tave siųsti. Kiek kartų norėjau surinkti tavo vaikus, kaip višta surenka savo viščiukus po sparnais, o tu nenorėjai!
37"Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
38Štai jūsų namai jums paliekami tušti.
38Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39Ir sakau jums: nuo dabar jūs manęs nebematysite, kol tarsite: ‘Palaimintas Tas, kuris ateina Viešpaties vardu!’ ”
39Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."