1Išėjęs iš šventyklos, Jėzus ėjo tolyn. Priėjo Jo mokiniai, rodydami Jam šventyklos pastatus.
1Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
2O Jis jiems tarė: “Ar matote visa tai? Iš tiesų sakau jums: čia neliks akmens ant akmens, viskas bus išgriauta!”
2Yesu akawaambia, "Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa."
3Kai Jis sėdėjo Alyvų kalne, priėjo vieni mokiniai ir klausė: “Pasakyk mums, kada tai įvyks? Ir koks Tavo atėjimo ir pasaulio pabaigos ženklas?”
3Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?"
4Jėzus jiems atsakė: “Žiūrėkite, kad niekas jūsų nesuklaidintų.
4Yesu akawajibu, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5Daug kas ateis mano vardu ir sakys: ‘Aš esu Kristus!’, ir daugelį suklaidins.
5Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
6Girdėsite apie karus ir karų gandus. Žiūrėkite, kad neišsigąstumėte, nes visa tai turi įvykti. Bet tai dar ne galas.
6Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7Tauta sukils prieš tautą ir karalystė prieš karalystę. Įvairiose vietose bus badmečių, marų ir žemės drebėjimų.
7Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
8Tačiau visa taigimdymo skausmų pradžia.
8Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9Tada jus atiduos kankinti ir žudyti. Jūs būsite visų tautų nekenčiami dėl mano vardo.
9"Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
10Daugelis pasipiktins, vieni kitus išdavinės ir vieni kitų nekęs.
10Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
11Atsiras daug netikrų pranašų, kurie daugelį suvedžios.
11Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
12Kadangi įsigalės neteisumas, daugelio meilė atšals.
12Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
13Bet kas ištvers iki galo, tas bus išgelbėtas.
13Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.
14Ir bus paskelbta ši karalystės Evangelija visame pasaulyje paliudyti visoms tautoms. Ir tada ateis galas”.
14Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
15“Todėl, kai pamatysite per pranašą Danielių paskelbtą naikinimo bjaurastį, stovinčią šventoje vietoje (kas skaito, teišmano),
15"Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
16tada, kas bus Judėjoje, tebėga į kalnus,
16hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.
17kas ant stogo, tenelipa žemėn pasiimti ko nors iš savo namų,
17Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
18o kas laukuose, tenegrįžta pasiimti apsiausto.
18Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
19Vargas nėščioms ir žindančioms tomis dienomis!
19Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
20Bet melskitės, kad jums netektų bėgti žiemą ar per sabatą.
20Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
21Tuomet bus didelis suspaudimas, kokio nėra buvę nuo pasaulio pradžios iki dabar ir kokio daugiau nebebus.
21Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
22Ir jeigu tos dienos nebūtų sutrumpintos, neišsigelbėtų nė vienas kūnas. Bet dėl išrinktųjų tos dienos bus sutrumpintos.
22Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23Jei tada kas nors jums sakys: ‘Štai čia Kristus’, arba: ‘Jis tenai!’,netikėkite,
23"Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
24nes atsiras netikrų kristų ir netikrų pranašų, ir jie darys didelių ženklų bei stebuklų, kad suklaidintų, jei įmanoma, net išrinktuosius.
24Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
25Štai Aš jums iš anksto tai pasakiau!”
25Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.
26“Todėl, jeigu jums sakytų: ‘Štai Jis dykumoje!’, neikite, ‘Štai Jis kambariuose!’, netikėkite.
26Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
27Kaip žaibas tvyksteli iš rytų ir nušvinta iki vakarų, toks bus ir Žmogaus Sūnaus atėjimas.
27maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
28Kur tik bus lavonų, ten sulėks ir maitvanagiai.
28Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29Tuoj pat po tų suspaudimo dienų saulė užtems, mėnulis nebeduos šviesos, žvaigždės kris iš dangaus, ir dangaus jėgos bus sudrebintos.
29"Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
30Tada danguje pasirodys Žmogaus Sūnaus ženklas, ir visos žemės giminės raudos ir pamatys Žmogaus Sūnų, ateinantį dangaus debesyse su galybe ir didžia šlove.
30Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
31Jis pasiųs savo angelus su skardžiais trimitų garsais, ir jie surinks Jo išrinktuosius iš keturių žemės pusių, nuo vieno dangaus pakraščio iki kito.
31Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
32Pasimokykite iš palyginimo su figmedžiu: kai jo šaka suminkštėja ir sprogsta lapai, jūs žinote, jog artėja vasara.
32"Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33Taip pat, visa šita išvydę, žinokite, jog tai arti, prie durų.
33Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
34Iš tiesų sakau jums: ši karta nepraeis, iki visa tai įvyks.
34Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
35Dangus ir žemė praeis, bet mano žodžiai nepraeis.
35Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36Tačiau tos dienos ir valandos niekas nežino, nė dangaus angelai, o vien tik mano Tėvas”.
36"Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
37“Kaip buvo Nojaus dienomis, taip bus ir tada, kai ateis Žmogaus Sūnus.
37Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
38Kaip dienomis prieš tvaną žmonės valgė, gėrė, tuokėsi ir tuokė iki tos dienos, kurią Nojus įžengė į laivą,
38Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
39nieko nenumanydami, kol užėjo tvanas ir visus nusinešė; taip bus ir tada, kai ateis Žmogaus Sūnus.
39Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
40Tada du bus kartu lauke, ir vienas bus paimtas, o kitas paliktas.
40Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
41Dvi mals girnomis, ir viena bus paimta, o kita palikta.
41Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
42Todėl budėkite, nes nežinote, kurią valandą ateis jūsų Viešpats.
42Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
43Supraskite ir tai: jeigu šeimininkas žinotų, kurią nakties valandą ateis vagis, jis budėtų ir neleistų jam įsilaužti į namus.
43Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
44Todėl ir jūs būkite pasiruošę, nes Žmogaus Sūnus ateis tą valandą, kurią nemanote”.
44Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
45“Kas yra tas ištikimas bei protingas tarnas, kurį šeimininkas paskyrė tarnauti savo šeimynai, kad ją maitintų deramu laiku?
45Yesu akaendelea kusema, "Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
46Palaimintas tarnas, kurį sugrįžęs šeimininkas ras taip darantį.
46Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47Iš tiesų sakau jums: jį paskirs valdyti visų savo turtų.
47Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48Bet jei blogas tarnas tartų savo širdyje: ‘Mano šeimininkas neskuba grįžti’,
48Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
49ir pradėtų mušti savo tarnybos draugus, valgyti ir gerti su girtuokliais,
49kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50to tarno šeimininkas sugrįš tą dieną, kai jis nelaukia, ir tą valandą, kurią jis nemano.
50bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51Jis perkirs jį pusiau ir paskirs jam dalį su veidmainiais. Ten bus verksmas ir dantų griežimas”.
51Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.