1Matydamas minias, Jėzus užkopė į kalną ir atsisėdo. Prie Jo priėjo mokiniai.
1Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda mlimani, akaketi. Wanafunzi wake wakamwendea,
2Atvėręs lūpas, Jis ėmė mokyti:
2naye akaanza kuwafundisha:
3“Palaiminti vargšai dvasia, nes jų yra dangaus karalystė.
3"Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
4Palaiminti, kurie liūdi, nes jie bus paguosti.
4Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa.
5Palaiminti romieji, nes jie paveldės žemę.
5Heri walio wapole, maana watairithi nchi.
6Palaiminti, kurie alksta ir trokšta teisumo, nes jie bus pasotinti.
6Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa.
7Palaiminti gailestingieji, nes jie susilauks gailestingumo.
7Heri walio na huruma, maana watahurumiwa.
8Palaiminti tyraširdžiai, nes jie regės Dievą.
8Heri wenye moyo safi, maana watamwona Mungu.
9Palaiminti taikdariai, nes jie bus vadinami Dievo vaikais.
9Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu.
10Palaiminti, kurie persekiojami dėl teisumo, nes jų yra dangaus karalystė.
10Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11Palaiminti jūs, kai dėl manęs jus šmeižia ir persekioja bei meluodami visaip piktžodžiauja.
11"Heri yenu ninyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu.
12Būkite linksmi ir džiūgaukite, nes didelis jūsų atlygis danguje. Juk lygiai taip persekiojo ir iki jūsų buvusius pranašus”.
12Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Hivyo ndivyo walivyowadhulumu manabii waliokuwako kabla yenu.
13“Jūs esate žemės druska. Jei druska netenka sūrumo, kuo gi ją reikėtų pasūdyti? Ji niekam netinka, ir belieka ją išberti žmonėms sumindžioti.
13"Ninyi ni chumvi ya dunia! Lakini chumvi ikipoteza ladha yake itakolezwa na nini? Haifai kitu tena, ila hutupwa nje na kukanyagwa na watu.
14Jūs esate pasaulio šviesa. Neįmanoma nuslėpti miesto, pastatyto ant kalno.
14"Ninyi ni mwanga wa ulimwengu! Mji uliojengwa juu ya mlima hauwezi kufichika.
15Ir niekas, uždegęs žiburį, nevožia jo indu, bet stato į žibintuvą, kad šviestų visiems, kas yra namuose.
15Wala watu hawawashi taa na kuifunika kwa chungu, ila huiweka juu ya kinara ili iwaangazie wote waliomo nyumbani.
16Taip tešviečia ir jūsų šviesa žmonių akivaizdoje, kad jie matytų jūsų gerus darbus ir šlovintų jūsų Tėvą, kuris danguje”.
16Vivyo hivyo, ni lazima mwanga wenu uangaze mbele ya watu, ili wayaone matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni."
17“Nemanykite, jog Aš atėjau panaikinti Įstatymo ar Pranašų. Ne panaikinti jų atėjau, bet įvykdyti.
17"Msidhani ya kuwa nimekuja kutangua Sheria ya Mose na mafundisho ya manabii. Sikuja kutangua bali kukamilisha.
18Iš tiesų sakau jums: kol dangus ir žemė nepraeis, nė viena raidelė ir nė vienas brūkšnelis neišnyks iš Įstatymo, kol viskas išsipildys.
18Kweli nawaambieni, mpaka hapo mbingu na dunia zitakapopita, hakuna hata nukta moja au sehemu ndogo kabisa ya Sheria itakayoondolewa, mpaka yote yametimia.
19Todėl, kas sulaužytų bent vieną iš mažiausių įsakymų ir taip mokytų žmones, tas bus vadinamas mažiausiu dangaus karalystėje. O kas juos vykdys ir jų mokys, bus vadinamas didžiu dangaus karalystėje.
19Basi, yeyote atakayevunja hata amri moja ndogo kuliko zote, na kuwafundisha wengine wafanye hivyo, huyo atakuwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbiguni. Lakini yule atakayezishika na kuwafundisha wengine, huyo atakuwa mkubwa katika Ufalme wa mbinguni.
20Taigi sakau jums: jeigu jūsų teisumas nepranoks Rašto žinovų ir fariziejų teisumo,neįeisite į dangaus karalystę”.
20Ndiyo maana nawaambieni, wema wenu usipozidi ule wa Mafarisayo na walimu wa Sheria, hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.
21“Jūs girdėjote, kad protėviams buvo pasakyta: ‘Nežudyk’; o kas nužudo, turės atsakyti teisme.
21"Mmekwisha sikia ya kuwa watu wa kale waliambiwa: Usiue! Atakayeua lazima ahukumiwe.
22O Aš jums sakau: kas be reikalo pyksta ant savo brolio, turės atsakyti teisme. Kas sako savo broliui: ‘Pusgalvi’, turės stoti prieš sinedrioną. O kas sako: ‘Beproti’, tas smerktinas į pragaro ugnį.
22Lakini mimi nawaambieni, yeyote anayemkasirikia ndugu yake, lazima ahukumiwe. Anayemdharau ndugu yake atapelekwa mahakamani. Anayemwita ndugu yake: Pumbavu atastahili kuingia katika moto wa Jehanamu.
23Todėl jei neši dovaną prie aukuro ir ten prisimeni, jog tavo brolis turi šį tą prieš tave,
23Basi, ukipeleka sadaka yako mbele ya madhabahu na hapo ukakumbuka kwamba ndugu yako ana ugomvi nawe,
24palik savo dovaną ten prie aukuro, eik pirmiau susitaikinti su savo broliu, ir tik tada sugrįžęs aukok savo dovaną.
24iache sadaka yako mbele ya madhabahu, nenda kwanza ukapatane na ndugu yako, ndipo urudi ukatoe sadaka yako.
25Greitai susitark su savo kaltintoju, dar kelyje į teismą, kad kaltintojas neįduotų tavęs teisėjui, o teisėjasteismo vykdytojui ir kad nepakliūtum į kalėjimą.
25"Patana na mshtaki wako upesi mkiwa bado njiani, kwenda mahakamani. La sivyo, mshtaki wako atakukabidhi kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa askari, nawe utafungwa gerezani.
26Iš tiesų sakau tau: neišeisi iš ten, kol neatsiteisi iki paskutinio skatiko”.
26Kweli nakwambia, hutatoka humo mpaka umemaliza kulipa senti ya mwisho.
27“Jūs girdėjote, jog protėviams buvo pasakyta: ‘Nesvetimauk!’
27"Mmesikia ya kuwa watu waliambiwa: Usizini!
28O Aš jums sakau: kiekvienas, kuris geidulingai žiūri į moterį, jau svetimauja savo širdyje.
28Lakini mimi nawaambieni, atakayemtazama mwanamke kwa kumtamani, amekwisha zini naye moyoni mwake.
29Jeigu tavo dešinioji akis skatina tave nusidėti, išlupk ją ir mesk šalin. Geriau tau netekti vieno nario, negu kad visas kūnas būtų įmestas į pragarą.
29Basi, kama jicho lako la kulia linakukosesha, ling'oe ukalitupe mbali. Afadhali zaidi kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako, kuliko mwili wako wote kutupwa katika moto wa Jehanamu.
30Ir jeigu tavo dešinioji ranka skatina tave nusidėti, nukirsk ją ir mesk šalin. Geriau tau netekti vieno nario, negu kad visas kūnas būtų įmestas į pragarą”.
30Na kama mkono wako wa kulia unakukosesha, ukate ukautupe mbali. Afadhali zaidi kupoteza kiungo kimoja cha mwili, kuliko mwili wako wote uende katika moto wa Jehanamu.
31“Taip pat buvo pasakyta: ‘Kas atleidžia savo žmoną, teišduoda jai skyrybų raštą’.
31"Ilikwisha semwa pia: Anayemwacha mke wake, yampasa ampe hati ya talaka.
32O Aš jums sakau: kiekvienas, kuris atleidžia savo žmoną,jei ne ištvirkavimo atveju,skatina ją svetimauti; ir jeigu kas atleistąją vedasvetimauja”.
32Lakini mimi nawaambieni, anayempa mkewe talaka, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, anamfanya azini; na mtu akimwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
33“Taip pat girdėjote, jog protėviams buvo pasakyta: ‘Neprisiek melagingai, bet ištesėk Viešpačiui savo priesaikas’.
33"Tena mmesikia kuwa watu wa kale waliambiwa: Usivunje kiapo chako, bali ni lazima utimize kiapo chako kwa Bwana.
34O Aš jums sakau: iš viso neprisiekinėkite nei dangumi, nes jis Dievo sostas,
34Lakini mimi nawaambieni, msiape kamwe; wala kwa mbingu, maana ni kiti cha enzi cha Mungu;
35nei žeme, nes jiJo pakojis, nei Jeruzale, nes jididžiojo Karaliaus miestas.
35wala kwa dunia, maana ni kiti chake cha kuwekea miguu; wala kwa Yerusalemu, maana ni mji wa Mfalme mkuu.
36Neprisiek nei savo galva, nes negali nė vieno plauko padaryti balto ar juodo.
36Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.
37Verčiau jūs sakykite: ‘Taip’, jei taip, ‘Ne’, jei ne, o kas viršaus, tai iš pikto”.
37Ukisema, Ndiyo, basi iwe Ndiyo; ukisema Siyo, basi iwe kweli Siyo. Chochote kinachozidi hayo hutoka kwa yule Mwovu.
38“Jūs girdėjote, jog buvo pasakyta: ‘Akis už akį’ ir ‘dantis už dantį’.
38"Mmesikia kwamba ilisemwa: Jicho kwa jicho, jino kwa jino.
39O Aš jums sakau: nesipriešinkite piktam, bet, jei kas tave muštų per dešinį skruostą, atsuk jam ir kitą.
39Lakini mimi nawaambieni, usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la pili.
40Jei kas nori su tavimi bylinėtis ir paimti tavo tuniką, atiduok jam ir apsiaustą.
40Mtu akikupeleka mahakamani kutaka kukuchukulia shati lako, mwache achukue pia koti lako.
41Jei kas verstų tave nueiti mylią, nueik su juo dvi.
41Mtu akikulazimisha kubeba mzigo wake kilomita moja, ubebe kilomita mbili.
42Prašančiam duok ir nuo norinčio iš tavęs pasiskolinti nenusigręžk.
42Akuombaye mpe, na mtu akitaka kukukopa kitu usimnyime.
43Jūs girdėjote, jog buvo pasakyta: ‘Mylėk savo artimą’ ir nekęsk savo priešo.
43"Mmesikia kwamba ilisemwa: Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.
44O Aš jums sakau: mylėkite savo priešus, laiminkite jus keikiančius, darykite gera tiems, kurie nekenčia jūsų, ir melskitės už savo skriaudėjus ir persekiotojus,
44Lakini mimi nawaambieni, wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi
45kad būtumėte vaikai savo Tėvo, kuris danguje; Jis juk leidžia savo saulei tekėti blogiesiems ir geriesiems, siunčia lietų ant teisiųjų ir neteisiųjų.
45ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu wabaya na wema, na kuwanyeshea mvua watu wanyofu na waovu.
46Jei mylite tuos, kurie jus myli, kokį gi atlygį turite? Argi taip nesielgia ir muitininkai?
46Je, mtapata tuzo gani kwa kuwapenda tu wale wanaowapenda ninyi? Hakuna! Kwa maana hata watoza ushuru hufanya hivyo!
47Ir jeigu sveikinate tik savo brolius, kuo gi viršijate kitus? Argi to nedaro ir muitininkai?
47Kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je, mmefanya kitu kisicho cha kawaida? Hata watu wasiomjua Mungu nao hufanya vivyo hivyo.
48Taigi būkite tobuli, kaip ir jūsų Tėvas, kuris danguje, yra tobulas”.
48Basi, muwe wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.