1“Žiūrėkite, jog nedarytumėte savo gailestingumo darbų žmonių akyse, kad būtumėte jų matomi, kitaip negausite atlygio iš savo Tėvo, kuris danguje.
1"Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
2Todėl, duodamas išmaldą, netrimituok sinagogose ir gatvėse, kaip daro veidmainiai, kad būtų žmonių giriami. Iš tiesų sakau jums: jie jau atsiėmė savo atlygį.
2"Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
3Kai aukoji, tenežino tavo kairė, ką daro dešinė,
3Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
4kad tavo gailestingumo auka būtų slaptoje, o tavo Tėvas, regintis slaptoje, tau atlygins viešai”.
4Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
5“Kai meldžiatės, nebūkite kaip veidmainiai, kurie mėgsta melstis, stovėdami sinagogose ir gatvių kampuose, kad būtų žmonių matomi. Iš tiesų sakau jums: jie jau atsiėmė savo atlygį.
5"Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
6Kai meldiesi, eik į savo kambarėlį ir, užsirakinęs duris, melskis savo Tėvui, kuris yra slaptoje, o tavo Tėvas, regintis slaptoje, tau atlygins viešai.
6Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
7Melsdamiesi nedaugiažodžiaukite kaip pagonys: jie mano būsią išklausyti dėl žodžių gausumo.
7"Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
8Nebūkite panašūs į juos, nes jūsų Tėvas žino, ko jums reikia, dar prieš jums prašant Jo.
8Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
9Todėl melskitės taip: ‘Tėve mūsų, kuris esi danguje, teesie šventas Tavo vardas,
9Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
10teateinie Tavo karalystė, tebūnie Tavo valia kaip danguje, taip ir žemėje.
10Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
11Kasdienės mūsų duonos duok mums šiandien
11Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
12ir atleisk mums mūsų kaltes, kaip ir mes atleidžiame savo kaltininkams.
12Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
13Ir nevesk mūsų į pagundymą, bet gelbėk mus nuo pikto; nes Tavo yra karalystė, jėga ir šlovė per amžius. Amen’.
13Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
14Jeigu jūs atleisite žmonėms jų nusižengimus, tai ir jūsų dangiškasis Tėvas atleis jums,
14"Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15o jeigu jūs neatleisite žmonėms jų nusižengimų, tai ir jūsų Tėvas neatleis jūsų nusižengimų”.
15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16“Kai pasninkaujate, nebūkite paniurę kaip veidmainiai: jie perkreipia veidus, kad žmonės matytų juos pasninkaujant. Iš tiesų sakau jums: jie jau atsiėmė savo atlygį.
16"Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
17O tu, kai pasninkauji, pasitepk galvą ir nusiprausk veidą,
17Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
18kad ne žmonėms rodytumeis pasninkaująs, bet savo Tėvui, kuris yra slaptoje. Ir tavo Tėvas, regintis slaptoje, tau atlygins viešai”.
18ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
19“Nekraukite sau turtų žemėje, kur kandys ir rūdys ėda, kur vagys įsilaužia ir vagia.
19"Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
20Bet kraukite sau turtus danguje, kur nei kandys, nei rūdys neėda, kur vagys neįsilaužia ir nevagia,
20Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
21nes kur tavo turtas, ten ir tavo širdis”.
21Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
22“Kūno žiburys yra akis. Todėl, jei tavo akis sveika, visas tavo kūnas bus šviesus.
22"Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
23O jei tavo akis pikta, visas tavo kūnas bus tamsus. Taigi, jei tavyje esanti šviesa yra tamsa, tai kokia baisi toji tamsa!”
23Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
24“Niekas negali tarnauti dviems šeimininkams: arba jis vieno nekęs, o kitą mylės, arba vienam bus atsidavęs, o kitą nieku vers. Negalite tarnauti Dievui ir Mamonai”.
24"Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
25“Todėl sakau jums: nesirūpinkite savo gyvybe, ką valgysite ar ką gersite, nei savo kūnu, kuo vilkėsite. Argi gyvybė ne daugiau už maistą ir kūnas už drabužį?
25"Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
26Pažvelkite į padangių paukščius: nei jie sėja, nei pjauna, nei į kluonus krauna, o jūsų dangiškasis Tėvas juos maitina. Argi jūs ne daug vertesni už juos?
26Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
27O kas iš jūsų gali savo rūpesčiu bent per sprindį pridėti sau ūgio?
27Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
28Ir kam gi rūpinatės drabužiu? Žiūrėkite, kaip auga lauko lelijos. Jos nesidarbuoja ir neverpia,
28"Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
29bet sakau jums: nė Saliamonas visoje savo šlovėje nebuvo taip pasipuošęs, kaip kiekviena iš jų.
29Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
30Jeigu Dievas taip aprengia laukų žolę, kuri šiandien žaliuoja, o rytoj metama į krosnį, tai argi Jis dar labiau nepasirūpins jumis, mažatikiai?
30Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
31Todėl nesirūpinkite ir neklausinėkite: ‘Ką valgysime?’, arba: ‘Ką gersime?’, arba: ‘Kuo vilkėsime?’
31"Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
32Visų tų dalykų ieško pagonys. Jūsų dangiškasis Tėvas juk žino, kad viso to jums reikia.
32Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
33Pirmiausia ieškokite Dievo karalystės ir Jo teisumo, o visa tai bus jums pridėta.
33Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
34Taigi nesirūpinkite rytdiena, nes rytojus pats pasirūpins savimi. Kiekvienai dienai užtenka savo vargo”.
34Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.